Watanzania mmekuwa na hasira sana

Watanzania mmekuwa na hasira sana

Vhagar

JF-Expert Member
Joined
Jun 8, 2015
Posts
20,550
Reaction score
39,949
Utafiti wangu usio rasmi nimekuja gundua kwa miaka inavyozidi kwenda watanzania wamekuwa watu wa kughadhibika sana. Jambo dogo tu hata lisilohitaji kutumia hasira mtu anaweza kukuwakia ukikaa vibaya anaweza tamani amuweke mtu vibao.

Ni ugumu wa maisha au tatizo nini? Ndugu zangu matatizo hayatatuliki kwa kuwaka hasira. Zaidi jazba zitafanya ushindwe kuchukua hatua sahihi.

Nawapa sana pole watu ambao shughuli zao kutwa nzima washughulika na watu tofauti tofauti kama makondakta hawa kazi yao ngumu sana.

Yaani hata humu kwenye nyuzi swala dogo tu mtu anapandwa na jazba. Huyo unayemkasirikia huenda si chanzo cha yanakusibu tuishi kwa upendo tonatofautiana uelewa usitake kila mtu awaze kama wewe.

Unamkasirikia nani na maisha umeyakosea mwenyewe?
 
Barabarani ndo kabisa balaa.. Unamuona mtu anaendesha gari anataka agonge hata watu kwa hasira😀. Ugumu wa maisha ndo tatizo
 
Oyaaaa mnatukatisha tamaa kurudi nchini kwetu, wengine tunataka tukirudi tu tuowe tuanze family ila kwa mambo hayo inawezekana tukakosa kuowa huko, ila yote juu ya yote Mungu mkubwa na haya maisha ni yakupita
 
watanzania wengi wanapenda shotikati.
njoeni huku kijijini tulime.
ukitaka mali utapata shambani sio kijijini.
Sasa mkuu wote tukija kijijini maflyover ya Magufuli atayatumia nani huku dasilamu?
 
Hizo sio hasira ni jazba,yani unamkuta mtu kanuna tu bila sababu,akianza kuwazia kabeba walet mfukoni tokea asubuhi mpaka jioni haina kitu ndio mpaka ndita zinatokea usoni.
 
Hizo sio hasira ni jazba,yani unamkuta mtu kanuna tu bila sababu,akianza kuwazia kabeba walet mfukoni tokea asubuhi mpaka jioni haina kitu ndio mpaka ndita zinatokea usoni...
Hahahaha oyaaa ukweli unajua kuwa unauma hasa kwa sisi wataftaji ila mm sikati tamaa
 
Back
Top Bottom