bmbalamwezi
JF-Expert Member
- Mar 12, 2015
- 788
- 195
Katika pitapita yangu katika mitandao ya kijamii na sehemu za wasomi kama vyuo vikuu, UDOM, UDSM, SAUT, DUCE, Tumaini na TEKU nimegundua wengi wanaikubali Katiba Inayopendekezwa. Baadhi yao wamesema tulikuwa tunafuata mkumbo kwa yale tunayoyasikia kwa watu. Mwanachuo mmoja toka UDOM kasema kuwa Katiba Inayopendekezwa alidhani imeitambua mahakama ya Kadhi lakni baada ya kuisoma na kuielewa ameikubali. Akasema kumbe watu tunadanganywa. Na wengine wengi kwenye mitandao ya kijamii wameikubali katiba hii. Hata kwenye televisheni na redio pia magezi inaonekana kuwa watu wengi wameikubali. Hii itadhihirika katika Kura ya Maoni ambayo inasubiriwa kwa hamu. Kwenu wanaJF.:clock: