Watanzania tubadilishe mitazamo ya kutaka kufanya sherehe kubwa za gharama

Watanzania tubadilishe mitazamo ya kutaka kufanya sherehe kubwa za gharama

Bitcoinbase

JF-Expert Member
Joined
Jul 17, 2016
Posts
319
Reaction score
285
Kumezuka tabia ya kuendekeza starehe na sherehe kubwa za harusi kwa kutegemea michango ya watu, tatizo linakuja unapotaka kila mtu akuchangie ilimradi unamfahamu au Mtumishi katika taasisi moja, inakera sana michango inakuwa nongwa, msg mara simu mara nini nini? Mara umeadiwa kwenye group bila ridhaa. Kiukweli binafsi sipendagi hii tabia.

Halafu usipochangia unakasirikiwa kabisa kana kwamba lazima. Hebu nipate experience wezangu wenye mtazamo kama wangu wakutopenda kuchangia na wala huwa hawaombi michango?
 
Ni umaskini wa akili.Unataka kufanya sherehe,tafuta hela, alika watu wachache fanya sherehe kufuatana na resources ulizo nazo.

Mkuu naona kuna correlation ya tabia hizi na kupungua kwa IQ.Naona kwamba jinsi uzuzu unavyozidi kuongezeka,ndivyo tabia za hovyo hovvyo zinavyozidi kuongezeka.Tabia zingine ni kama kitchen party,kufanya misiba kama sherehe,sare za misiba,kuchukua video za misiba nk.nk.
 
Halafu usipochangia unakasirikiwa kabisa kana kwamba lazima. Hebu nipate experience wezangu wenye mtazamo kama wangu wakutopenda kuchangia na wala huwa hawaombi michango?
Yalinikuta, mwanamtaa mwenzangu alikuja nyumbani akatumbukiza kadi ya mchango chini ya mlango, mlango ulipofunguliwa kadi ikasukumwa kwenda unakofungukia mlango ambako kuna kabati hivyo kadi ikaingia uvunguni mwa kabati la vyombo, sikujua chochote.

Harusi ilipita nami sikushiriki, majuzi amenipita barabarani mvua inanyesha nikashangaa, nikamsimulia rafiki yangu kuwa muumini mwenzako amenipita kama hanijui hata kunipa msaada wa lift hakuna, akanijibu kuwa "yawezekana kwakuwa hukumchangia arusi ya mdogo wake kwani kuna siku alikuzungumzia",

Nikasema ningechangaje kama sikupewa mwaliko? ndipo nikaambiwa alifika nyumbani sipo akaslot in kadi chini, nilipofuatilia nikaona kadi ilizama chini ya kabati imeshaota ukungu wa unyevu😎
🤣
 
Kimsingi shehere kubwa au za gharama kubwa huwa zinafanywa na matajiri ili kuonyesha how rich they are na pia kutowaangusha matajiri wenzake watakaokuna kwenye sherehe.

Sasa ww tunakujua ni mtendaji kata katavi huko unataka kutudanganya nn kwenye sherehe yako? Mbaya zaidi bora hizo fujo ulete kwa hela zako za mkopo, unalazimisha watu wakuchangie.
 
Kimsingi shehere kubwa au za gharama kubwa huwa zinafanywa na matajiri ili kuonyesha how rich they are na pia kutowaangusha matajiri wenzake watakaokuna kwenye sherehe... Sasa ww tunakujua ni mtendaji kata katavi huko unataka kutudanganya nn kwenye sherehe yako? Mbaya zaidi bora hizo fujo ulete kwa hela zako za mkopo, unalazimisha watu wakuchangie... Fck off
Nimechekaaaa kwani watendaji kata uku Mpanda tumekukosea nini lakini
 
Mbaya kabisa wengine unakuta wana watoto tena mapacha wanatanga uchangie harusi

Tena kwa kulazimishana utafikiri utaalikwa siku moja kwenda kutindua [emoji38][emoji38]
 
Kumezuka tabia ya kuendekeza starehe na sherehe kubwa za harusi kwa kutegemea michango ya watu, tatizo linakuja unapotaka kila mtu akuchangie ilimradi unamfahamu au Mtumishi katika taasisi moja, inakera sana michango inakuwa nongwa, msg mara simu mara nini nini? Mara umeadiwa kwenye group bila ridhaa. Kiukweli binafsi sipendagi hii tabia.

Halafu usipochangia unakasirikiwa kabisa kana kwamba lazima. Hebu nipate experience wezangu wenye mtazamo kama wangu wakutopenda kuchangia na wala huwa hawaombi michango?
Mbona simple
Si unamkatalia tu / sina / Niko vibaya.
Wakiku- add kwenye group
Una-left.. veeeery very simple.. brother.
 
Jikune kadri uwezapo sio kutaka mambo makubwa ili hali ww mwenyewe unajua uwezo wako
 
Kumezuka tabia ya kuendekeza starehe na sherehe kubwa za harusi kwa kutegemea michango ya watu, tatizo linakuja unapotaka kila mtu akuchangie ilimradi unamfahamu au Mtumishi katika taasisi moja, inakera sana michango inakuwa nongwa, msg mara simu mara nini nini? Mara umeadiwa kwenye group bila ridhaa. Kiukweli binafsi sipendagi hii tabia.

Halafu usipochangia unakasirikiwa kabisa kana kwamba lazima. Hebu nipate experience wezangu wenye mtazamo kama wangu wakutopenda kuchangia na wala huwa hawaombi michango?
[emoji38][emoji38][emoji38][emoji38]
 
Asilimia 70% ya watu wanaotoa michango ya harusi huwa hawatoi kutoka moyoni.
Mtu anachangia ili kuondoa aibu tu kwa jamaa ama rafiki.
Siku hizi ishakuwa utamaduni kuchangishana. Baadhi ya watu wamefika mbali wanataka hadi michango ya birthday,kipaimara,komunyo, graduation n.k.
 
Kumezuka tabia ya kuendekeza starehe na sherehe kubwa za harusi kwa kutegemea michango ya watu, tatizo linakuja unapotaka kila mtu akuchangie ilimradi unamfahamu au Mtumishi katika taasisi moja, inakera sana michango inakuwa nongwa, msg mara simu mara nini nini? Mara umeadiwa kwenye group bila ridhaa. Kiukweli binafsi sipendagi hii tabia.

Halafu usipochangia unakasirikiwa kabisa kana kwamba lazima. Hebu nipate experience wezangu wenye mtazamo kama wangu wakutopenda kuchangia na wala huwa hawaombi michango?
samahani kwa kuvamia uzi , maana 'mimi si mwenzako mwenye mtazamo wa kutopenda kuchangia, na huwa ninatoa michango.
Ila nimeguswa niseme kitu.
Tabia ya kuchangishana haijazuka kama wewe usemavyo, imekuwapo toka enzi kabla wewe hujazaliwa. Toka enzi za ujima watu walikuwa wakichangishana hata mazao, mafano mchele, maharage, mahindi nk. kwa kwa ajili ya kufanikisha sherehe. Ikafika mahali mazao au vitu vikawa adimu kuliko pesa, hapo watu wakaanza kuchangishana pesa.
Wote waliochangia walifanya kwa furaha na kwa moyo wa kupenda. Hata ikitokea mtu hajaombwa mchango na ndugu, jamaa au rafiki alijisikia vibaya kwa kujihisi kwamba ameonwa vipi, wakati mwingine hata kukasirika kwamba amedharauliwa. Kutokana na hili , mleta mada usifikiri kwamba kila akuombaye mchango ana shida na pesa yako, wengine wanatimiza wajibu tu ili usije ukalaumu.
Imefika mahali pesa nayo imekuwa adimu. Sasa kumezuka SASA kumezuka tabia ya watu kutopenda kuchangia sherehe za wenzao hata kuwashushia heshima hao wanaamba michango.
Napenda kuwaambia mleta mada na washiriksa wake kwamba tatizo walionalo si la hao wawaombao michango, bali ni la jamii, maana jamii imejengeka hivo. Inahitaji ujasiri wa aina yake kuipinga jamii inapotaka uombe michango kwa watu, ushawishi huwa ni mkubwa sana kwamba sherehe ni yako lakini haujifanyii mwenyewe, wafanyiwa na wanajamii, ingawa mwisho wa siku unatwikwa zigo la kuomba michango huku ukisaidiwa kwa mbaaali, ili kina bitcoinbase wakuone kimeo.
Mawazo ya mleta mada ni mazuri nayeye pamoja wachangiaji wanaomsapoti wanaonesha kuwa jamii imeanza kubadilika taratibu, angalau sasa kuna watu wenye ujasiri wa kuiambia jamii kwamba ndoa na maisha ya ndoa ni bora kuliko sherehe ya ndoa .
Nakushukuru mleta mada, natamani jamii ibadilike, wasitarajie sana sherehe toka kwa vijana wanaooa maana wakati mwingine hata wamewakwamisha vijana kufanya maamuzi hayo kwa kufikiria gharama za sherehe za harusi. Bali wawe radhi kulingana na uwezo wa kijana ama familia yake, kuamua kwamba kutakuwa na sherehe au la , au sherehe kubwa au ndogo.
 
SIKU YA HARUSI YANGU TUNAENDA KANISANI, TUNAFUNGA NDOA TUNARUDI ZETU HOME KUENDELEA NA MAISHA YA KAWAIDA... KULA MTAKULA KWENU AU KWA MAMA NTILIE 😎😂
Wewe una mawazo mazuri sana,lakini mazuzu yaliyo kuzunguuka yatakubali?
 
Back
Top Bottom