Watanzania tuchangamkie: UDSM centre, India Universities.

Watanzania tuchangamkie: UDSM centre, India Universities.

Sinkala

JF-Expert Member
Joined
Dec 22, 2008
Posts
1,773
Reaction score
688
Kuna kozi zinaendelea kutolewa kupitia LIVE VIDEOCONFERENCE katika centre ya Tanzania iliyopo UDSM. Project hii ipo katika nchi 53 za Africa na watu wanasoma huku wakimuona mwalimu LIVE katika big plasma screen + projector screen. Unaweza kuuliza swali kwa kunyoosha kidole na mwalimu anaweza kuuliza swali direct kwa kumchagua mwanafunzi anayemtaka. Hii ni tofauti na online learning, hii ni Tele-Education system ambapo wote (mwalimu na mwanafunzi) lazima muwepo darasani muda wa lecture. Kuna posibility pia ya kudownload video ya lecture iliyopita for your revision. Wanafunzi wa centre ya Tanzania wana uwezo pia wa kuwaona wenzao wa centre nyingine. Kuna centre zina wanafunzi hadi 200 (km Uganda) lakini watanzania tunachechemea. Project hii inatambuliwa na Serikali ya JMT kwani ni mkataba btn countries na sio Universities, na UDSM is just a centre, lakini Wizara ya Sayansi na Teknolojia ingeweza kuweka centre popote pale nchini kama ingetaka. Kwa maelezo zaidi soma hapo chini na ukimbie kuapply kabla pazia halijafungwa:

attachment.php
 
Kuna watu wametuma PM, mimi nami nimeiona tu hiyo announcement na kwenda pale kujionea, ni programme nzuri sana, ila nawashauri kwa maelezo zaidi muwaone wahusika pale UDSM
 
sasa wewe umeleta taarifa au unauliza? mbona inaonekana wewe mwenyewe huna uhakika na kile ulichokileta?
Kuna watu wametuma PM, mimi nami nimeiona tu hiyo announcement na kwenda pale kujionea, ni programme nzuri sana, ila nawashauri kwa maelezo zaidi muwaone wahusika pale UDSM
 
sasa wewe umeleta taarifa au unauliza? mbona inaonekana wewe mwenyewe huna uhakika na kile ulichokileta?
Nimeleta taarifa kwa sababu nimejionea jinsi programme inavyoeendeshwa, na nikafanikiwa kupata copy ya announcement pamoja na application form (hardcopy + softcopy). Kama kuna upungufu wa maelezo au hujaelewa niliyoeleza au yaliyopo kwenye tangazo, ndio hapo nimeshauri uwaone wahusika pale UD.
 
Back
Top Bottom