Watanzania tunataka katiba itakayopendekezwa na watu mil.60 sio hii iliyopendekezwa na watu 20

Tumia Akili japo Kidogo Watu Mil.60 wanapaswa watoe Maoni na Mapendekezo yao ndio maana yake
Lengo lenu ni kutaka mchakato wa Katiba Mpya uendelee kuchelewa ili muendelee kulamba asali siyo!!!
 
Tumia Akili japo Kidogo Watu Mil.60 wanapaswa watoe Maoni na Mapendekezo yao ndio maana yake
Nothing like that. Hakuna popote Duniani kila raia akafikiwa. Ushirikishwani unaweza kupitia vyama vya siasa, asasi za kiraia, Jumuiya mbalimbali n.k.
 
Tukichapana tutarudi nyuma miaka mingi sana hebu angalia Somalia.

Dialogue, Rasimu ya Warioba.
Nakubaliana na wewe. Lkn nadharia na mtazamo huo ndiyo ccm wanautumia kucheza na kuvuruga matakwa ya wananchi. Kwasababu wanajua watanzania hawapendi kuchapana.
 
Nakubaliana na wewe. Lkn nadharia na mtazamo huo ndiyo ccm wanautumia kucheza na kuvuruga matakwa ya wananchi. Kwasababu wanajua watanzania hawapendi kuchapana.
Sisi tujikite kwenye kutoa Darasa kwa Wananchi wa kawaida kuhusu umuhimu wa Katiba mpya,kwasababu ukienda Vijijini leo wengi hata hawaelewi tofauti ya Katiba na Kabati.
 
Ila Rais Samia bwana sijui anajionaje. Tume ya Warioba ilizunguka nchi zima watanzania karibu woote wakatoa maoni wasomi na wasio wasomi wakaweka mezani.Yeye akaacha yoote hayo akajitungia kakikundi ka watu 20 eti ndio kana maoni mazuri?

Hii dharau hata Mungu atakasirika.
 
Tumia Akili japo Kidogo Watu Mil.60 wanapaswa watoe Maoni na Mapendekezo yao ndio maana yake
Toa mfano wa nchi iliyowahi kusanya wananchi wake pamoja na kutoa maoni yao kile wanancho kiamini, wachache wanatuwakilisha tuliowengi na tusifikiri tunaweza kuwa na jipya lolote ambalo halipo na haliwezi kizungumzwa mahali pengine na mtu mwingine
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…