Phillipo Bukililo
JF-Expert Member
- Dec 29, 2015
- 18,487
- 13,611
Mwaka 1980 ni miaka 39 iliyopita. Ni kitambo. Tanzania ya wakati ule ilikuwa bado ni nchi ndogo sana. Kiuchumi na hata katika suala la idadi ya watu.
Mwaka ule mtu ukikatiza mbele ya meza ya magazeti unakuta yanayouzwa hayazidi matatu. Uhuru na Mzalendo, daily news na sunday news, siku za jumamosi litatoka gazeti la mfanyakazi.
Ni mwaka ambao wimbo wetu wa taifa uliimbwa kabla ya mechi tatu za hatua ya makundi ya kombe la mataifa huru kule Nigeria. Ni mwaka ambao ulikuwa ndio wa mwisho kwa Taifa Stars kuonekana katika michuano mikubwa.
Vijana kina Samatta, Msuva na wengine wametutoa kimasomaso na wimbo wetu utasikika tena kule Misri katikati ya mwaka huu. Vijana wetu wataonekana kwenye runinga wakiuimba wimbo huku mikono yao ikiwa katika eneo la moyo.
Heshima imerudi tena, na heshima hii iwe ni somo muhimu kwetu. Tuache kujiona hatuwezi, tuache kuwa na roho ya kuiombea mabaya nchi ambayo wazazi wako wote wawili wamezaliwa na kukulea wewe kwa upendo wa hali ya juu.
Kufanikiwa kwenda Misri inaweza kuonekana ni bahati kama mtu hajishughulishi katika kuwaza kwa kina.
Samatta yupo Belgium pengine msimu ujao anaweza kununuliwa Uingereza. Msuva yupo Morocco
pengine msimu ujao anaweza kununuliwa Hispania. Ambokile yupo Afrika ya Kusini pengine misimu miwili ijayo anaweza kuuzwa Ulaya.
Wachezaji wetu wameanza kujiamini na kutoka nje ya Tanzania kwa kasi kubwa, tuwaunge mkono kwa kila namna. Wanajazwa wivu kila wanapomuona Samatta akifunga magoli Belgium.
Ikiwa vijana wadogo wanajiamini na kwenda nje kutafuta fursa, inashangaza sana kumuona mtu ambaye anaitakia mabaya Tanzania. Inakera pia kumsoma mtu mwenye kuombea mabaya Taifa Stars isionekane kimataifa.
Watanzania tuachane na hizi hulka za kujiona hatuwezi, kujiona sisi tumeumbiwa kukosa.
Mwaka ule mtu ukikatiza mbele ya meza ya magazeti unakuta yanayouzwa hayazidi matatu. Uhuru na Mzalendo, daily news na sunday news, siku za jumamosi litatoka gazeti la mfanyakazi.
Ni mwaka ambao wimbo wetu wa taifa uliimbwa kabla ya mechi tatu za hatua ya makundi ya kombe la mataifa huru kule Nigeria. Ni mwaka ambao ulikuwa ndio wa mwisho kwa Taifa Stars kuonekana katika michuano mikubwa.
Vijana kina Samatta, Msuva na wengine wametutoa kimasomaso na wimbo wetu utasikika tena kule Misri katikati ya mwaka huu. Vijana wetu wataonekana kwenye runinga wakiuimba wimbo huku mikono yao ikiwa katika eneo la moyo.
Heshima imerudi tena, na heshima hii iwe ni somo muhimu kwetu. Tuache kujiona hatuwezi, tuache kuwa na roho ya kuiombea mabaya nchi ambayo wazazi wako wote wawili wamezaliwa na kukulea wewe kwa upendo wa hali ya juu.
Kufanikiwa kwenda Misri inaweza kuonekana ni bahati kama mtu hajishughulishi katika kuwaza kwa kina.
Samatta yupo Belgium pengine msimu ujao anaweza kununuliwa Uingereza. Msuva yupo Morocco
pengine msimu ujao anaweza kununuliwa Hispania. Ambokile yupo Afrika ya Kusini pengine misimu miwili ijayo anaweza kuuzwa Ulaya.
Wachezaji wetu wameanza kujiamini na kutoka nje ya Tanzania kwa kasi kubwa, tuwaunge mkono kwa kila namna. Wanajazwa wivu kila wanapomuona Samatta akifunga magoli Belgium.
Ikiwa vijana wadogo wanajiamini na kwenda nje kutafuta fursa, inashangaza sana kumuona mtu ambaye anaitakia mabaya Tanzania. Inakera pia kumsoma mtu mwenye kuombea mabaya Taifa Stars isionekane kimataifa.
Watanzania tuachane na hizi hulka za kujiona hatuwezi, kujiona sisi tumeumbiwa kukosa.