Watanzania wasomi na wasio wasomi lakini ni wajasiriamali acheni kukodi fremu ili kufungua biashara

Mama Edina

JF-Expert Member
Joined
Dec 18, 2022
Posts
850
Reaction score
2,019
Jamani eeh, kukodi fremu ufungue duka unapoteza hela zako. Somo hili kichwa cha habari hii kinahusika.

Hii tabia imekithiri sana hapa nchini. Utakuta mjasiriamali analipa pesa nyiiiingi kulipia chumba cha duka akitarajia kupata pesa nyingi, ni kosa kubwa sana.

Njia zifuatazo zinaweza tumika badala ya kumfadisha landlord's.

1. Tangaza biashara yako pelekea wateja wewe mwenyewe (huu mfumo door to door upo lkn kidogo sana)
2. Tumia social media kuuza bidhaa.
 
Sijajua shida nini, sijui huwa wana mwapu wa kufanya biashara.

Ila wenye fremu kwetu ni raha tu, akishindwa huyu anakuja yule, na kama fremu zipo sehemu nzuri unapiga pesa vizuri tu.

Ni biashara ambayo unaweza funga msuli na ukacheza bao, mwisho wa mwezi unaokota tu.
 
Mawazo yako ni mazuri ila tunarudi palepale tusipangiane matumizi na hela yangu
 
1. Tangaza biashara yako pelekea wateja wewe mwenyewe[huu mfumo door to door upo lkn kidogo sana
2. Tumia social media kuuza bidhaa.
Mfumo huu wateja hawakuamini wanataka uwaonyeshe ofisi yako ilipo, shida ndio inaanzia hapo ukiwa machinga au mchuuzi watu wanakosa uaminifu na wewe especially ikiwa unafanyia online, wanataka waone ofisi yako ilipo duka lako lipo wapi? Ofisi yako ipo wapi? Je! Wewe ni tapeli huna ofisi?

Wapo wanaofanya biashara za online Ila wanatumia ofisi za watu wengine kufanikisha biashara zao pale mteja anaposema anahitaji kufika ofisini, maana sio kila mteja atataka umfuate nyumbani mwingine atataka aje dukani kwako achague bidhaa tofauti tofauti ulizonazo anunue aende,
 
Uwekezaji mzuri Sana huo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…