Watanzania wenzangu, chonde chonde tutunze treni ya umeme ili idumu

Watanzania wenzangu, chonde chonde tutunze treni ya umeme ili idumu

koryo1952

JF-Expert Member
Joined
Mar 7, 2023
Posts
948
Reaction score
1,627
Treni ya umeme imeanza safari yake ya kwanza kwenda Morogoro ikitokea Dar. Hili ni jambo la kushukuru na kuipongeza sana Serikali. Tumeona mara nyingi kitu kipya kikianza kwa mbwembwe na kwa huduma nzuri lakini baadaye huduma yake ikidorora kwa kasi kubwa.

Treni ya umeme isifikie huko. Mifano hai ni Usafiri wa mwendo kasi ya hapa Dar. Mwanzoni huduma ilikuwa nzuri sana lakini fika pale leo, vituo vimechakaa, mabus yamechakaa, vyoo havitamaniki. Kwanini?. Mfano wa pili ni Uwanja wa Mkapa. Mwanzoni uwanja ulikuwa super kwa maana ya viti, muonekano, miundo mbinu kama vyoo,n.k.

Leo hii nenda pale. Watazamaji wanavunja viti kwa makusudi, vyoo vya pale havitamaniki. Watu wanajisaidia mpaka kwenye sinki za kunawia mikono. Inatisha. Sasa treni ya umeme imeanza kwa huduma nzuri. Chonde chode Watanzania tutunze treni hii ili idumu kwa muda mrefu.

Pia soma:Mazuri ya treni ya umeme
 
Ya maana zaidi ni kutunza miundombinu ya reli ya sgr na kuepuka hujuma kwa kung'oa mataruma 🐒
 
Treni ya umeme imeanza safari yake ya kwanza kwenda Morogoro ikitokea Dar. Hili ni jambo la kushukuru na kuipongeza sana Serikali. Tumeona mara nyingi kitu kipya kikianza kwa mbwembwe na kwa huduma nzuri lakini baadaye huduma yake ikidorora kwa kasi kubwa. Treni ya umeme isifikie huko. Mifano hai ni Usafiri wa mwendo kasi ya hapa Dar. Mwanzoni huduma ilikuwa nzuri sana lakini fika pale leo, vituo vimechakaa, mabus yamechakaa, vyoo havitamaniki. Kwanini?. Mfano wa pili ni Uwanja wa Mkapa. Mwanzoni uwanja ulikuwa super kwa maana ya viti, muonekano, miundo mbinu kama vyoo,n.k. Leo hii nenda pale. Watazamaji wanavunja viti kwa makusudi, vyoo vya pale havitamaniki. Watu wanajisaidia mpaka kwenye sinki za kunawia mikono. Inatisha. Sasa treni ya umeme imeanza kwa huduma nzuri. Chonde chode Watanzania tutunze treni hii ili idumu kwa muda mrefu.
Inakusaidia nini? kama madini, misitu, bahari havijakusaidia, sembuse mavyuma haya machakavu
 
Haiwezi kudumu. Ni 3 to 5 Years inakua imekufa.

Ili iendelee kuishi waikodishe iendeshwe na sekta binafsi.

Kumbuka atcl ilivyoanza ile 2017 hadi 2022 ilikua bomba sana, leo miaka 6 ama 6 ni flight cancellation tu na delays za kutosha.
 
Treni ya umeme imeanza safari yake ya kwanza kwenda Morogoro ikitokea Dar. Hili ni jambo la kushukuru na kuipongeza sana Serikali. Tumeona mara nyingi kitu kipya kikianza kwa mbwembwe na kwa huduma nzuri lakini baadaye huduma yake ikidorora kwa kasi kubwa. Treni ya umeme isifikie huko. Mifano hai ni Usafiri wa mwendo kasi ya hapa Dar. Mwanzoni huduma ilikuwa nzuri sana lakini fika pale leo, vituo vimechakaa, mabus yamechakaa, vyoo havitamaniki. Kwanini?. Mfano wa pili ni Uwanja wa Mkapa. Mwanzoni uwanja ulikuwa super kwa maana ya viti, muonekano, miundo mbinu kama vyoo,n.k. Leo hii nenda pale. Watazamaji wanavunja viti kwa makusudi, vyoo vya pale havitamaniki. Watu wanajisaidia mpaka kwenye sinki za kunawia mikono. Inatisha. Sasa treni ya umeme imeanza kwa huduma nzuri. Chonde chode Watanzania tutunze treni hii ili idumu kwa muda mrefu.
WAAMBIE CCM SIO SISI KWANI MWENDOKASI IMEKUFA NA NANI?
 
Ukitaka treni ya umeme itunzwe ondoeni kwanza umaskini. Vinginevyo tarajia watu kushuka na taa, viti na kila chuma kinachobebeka humo.

Hebu fikiria watu wanaiba ndala msikitini.
 
Haiwezi kudumu. Ni 3 to 5 Years inakua imekufa.

Ili iendelee kuishi waikodishe iendeshwe na sekta binafsi.

Kumbuka atcl ilivyoanza ile 2017 hadi 2022 ilikua bomba sana, leo miaka 6 ama 6 ni flight cancellation tu na delays za kutosha.
Binafsi naona kama kweli wanataka idumu, basi nauli yake iwe juu sana. Wapande wastaarabu (walioshiba) tu. Lkn wakiweka bei ambayo hata huyu pangu pakavu anaimudu. Kwisha habari yake.
 
Viongozi wenyewe hawana huruma na mali za taifa wanalo liongoza!
 
Treni ya umeme imeanza safari yake ya kwanza kwenda Morogoro ikitokea Dar. Hili ni jambo la kushukuru na kuipongeza sana Serikali. Tumeona mara nyingi kitu kipya kikianza kwa mbwembwe na kwa huduma nzuri lakini baadaye huduma yake ikidorora kwa kasi kubwa.

Treni ya umeme isifikie huko. Mifano hai ni Usafiri wa mwendo kasi ya hapa Dar. Mwanzoni huduma ilikuwa nzuri sana lakini fika pale leo, vituo vimechakaa, mabus yamechakaa, vyoo havitamaniki. Kwanini?. Mfano wa pili ni Uwanja wa Mkapa. Mwanzoni uwanja ulikuwa super kwa maana ya viti, muonekano, miundo mbinu kama vyoo,n.k.

Leo hii nenda pale. Watazamaji wanavunja viti kwa makusudi, vyoo vya pale havitamaniki. Watu wanajisaidia mpaka kwenye sinki za kunawia mikono. Inatisha. Sasa treni ya umeme imeanza kwa huduma nzuri. Chonde chode Watanzania tutunze treni hii ili idumu kwa muda mrefu.

Pia soma:Mazuri ya treni ya umeme
Nakuelewa usemayo lakini kwa ujinga wa Watanzania hatutaweza kuiendesha na kuibakisha kwenye standard tunayoanza nayo.

Mtu atengeneze treni million q1, si hesabu hiyo itakuwa "inflated" kwa million 21 na isitengenezzwe.

Kinachouwa ni wizi wa kijinga umejaa kila pembe.
 
Treni ya umeme imeanza safari yake ya kwanza kwenda Morogoro ikitokea Dar. Hili ni jambo la kushukuru na kuipongeza sana Serikali. Tumeona mara nyingi kitu kipya kikianza kwa mbwembwe na kwa huduma nzuri lakini baadaye huduma yake ikidorora kwa kasi kubwa.

Treni ya umeme isifikie huko. Mifano hai ni Usafiri wa mwendo kasi ya hapa Dar. Mwanzoni huduma ilikuwa nzuri sana lakini fika pale leo, vituo vimechakaa, mabus yamechakaa, vyoo havitamaniki. Kwanini?. Mfano wa pili ni Uwanja wa Mkapa. Mwanzoni uwanja ulikuwa super kwa maana ya viti, muonekano, miundo mbinu kama vyoo,n.k.

Leo hii nenda pale. Watazamaji wanavunja viti kwa makusudi, vyoo vya pale havitamaniki. Watu wanajisaidia mpaka kwenye sinki za kunawia mikono. Inatisha. Sasa treni ya umeme imeanza kwa huduma nzuri. Chonde chode Watanzania tutunze treni hii ili idumu kwa muda mrefu.

Pia soma:Mazuri ya treni ya umeme
Kwanza utunzaji sio utamaduni wa Watanzania

Nawapa mwaka mmja tuu kuwa kama mwendokasi
 
Nauli zipandishwe ili kudhibiti waharibifu
 
Back
Top Bottom