Wataturu (Waberbaigi): Kabila pekee Tanzania na Afrika Mashariki lililoogopwa na Wamasai.

Wataturu (Waberbaigi): Kabila pekee Tanzania na Afrika Mashariki lililoogopwa na Wamasai.

Mgambilwa ni mntu

JF-Expert Member
Joined
May 30, 2017
Posts
2,869
Reaction score
3,187
Wamasai ni jamii ya Nilo-Hamitic walioingia Afrika Mashariki kutokea eneo la Sudan na Ethiopia. Ni mojawapo ya jamii maarufu za Ki-Nilotes zilizotapakaa katika Afrika Mashariki hasa Kenya na Uganda. Wamasai kama ilivyo kwa Wanilotes ni wafugaji kwa asili na wanaoishi kwa kutegemea nyama, damu na maziwa.

So, ili kujihakikishia malisho na maji, wamekuwa wakihamahama na hivyo kujikuta wakipigana na jamii wanazokutana nazo. Wamasai pamoja na Wataturu (Wadatooga) ndio makabila ya Nilotes yaliyojipenyeza Kusini kabisa hadi kwa Wabantu ambao traditionally ni wakulima na wanaoishi kwa amani.

Kujipenyeza kwa Wamasai na Wataturu katika jamii za wakulima wa kibantu kulisababisha wawe wanavamia jamii za Wabantu mara kwa mara na kupora mifugo yao. Kwa woga wa kuuawa na kuporwa mifugo muda wote, jamii za makabila jirani zilianza kuiga baadhi ya mila za kimasai ikiwemo mavazi ya kimasai. Wasukuma (Wanyantuzu), Wambulu, Wambgwe, Wagorowa, Waalagwa, Warangi, ni baadhi ya walioathirika na hofu dhidi ya Wamasai.

Hata hivyo, Wamasai nao walikuwa na mbabe wao, indeed ni ndugu zao Wataturu (Waberbaig/Wadatooga), walioishi katika eneo linalozunguka Mlima Hanang (Hanang & Mbulu). Wataalamu wanadai kuwa almost kila Wamasai walipopigana na Wataturu, walipigwa mweleka na hivyo kuwafanya Wataturu kuogopeka zaidi na Makabila yanayowazunguka ya Wambulu, Wasukuma, Wanyilamba, Waisanzu, Waiambi, Wanyaturu, Wasandawe, Wahadzabe (Watindiga), Wagorowa (Wafiome), Waalagwa na Warangi.

Sema tu kuwa, Wataturu walikuwa wachache na waki-cover eneo dogo kulinganisha na Wamasai. Kumbukeni Wamasai wanna eneo kubwa kuanzia Kenya na Wamasai walioko Kenya ndio wengi kuliko walioko Tanzania.

Probably kuwa kwao Nairobi, Serengeti, Masai Mara, Ngorongoro, Tsavo, Engaruka, Tarangire, Manyara, Ziwa Natron (Flamingo) kuliwafanya wajulikane sana kidunia kuliko Wataturu.

IMG_5208.jpg


Nawasilisha wazee.
 
Hii habari inamapungufu makubwa. Inawezekana kabisa Wabarbaig wakawa na tishio kwetu Wahadzabe na dio kwa Waisanzu (Wanyisanzu)!

Hawa wabantu ambai pia ni wafugaji na wakulima wamepigana vuta nyingi sana na wabarbaig hata mwishoni mwa miaka ya 1980 ambapo hadi Mwl. Nyerere alipeleka kikosi cha jeshi kudhubiti mauaji ya jamii hizi mbili!

Wabarbaig waliawa sana sana na hao Wanyisanzu na mifugo yao kuchukuliwa kiasi kwamba wakakimbia hata maeneo yao ya asili!

Kuna bonde moja nadhani maeneo ya Ibaga au Kuelekea Msingi wazee wansema wabarbaig waliuawa sana kiasi kwamba mpaka leo hii ukitembelea maeneo hayo utapata mafuvu wa watu!
 
Hii habari inamapungufu makubwa. Inawezekana kabisa Wabarbaig wakawa na tishio kwetu Wahadzabe na dio kwa Waisanzu (Wanyisanzu)!

Hawa wabantu ambai pia ni wafugaji na wakulima wamepigana vuta nyingi sana na wabarbaig hata mwishoni mwa miaka ya 1980 ambapo hadi Mwl. Nyerere alipeleka kikosi cha jeshi kudhubiti mauaji ya jamii hizi mbili!

Wabarbaig waliawa sana sana na hao Wanyisanzu na mifugo yao kuchukuliwa kiasi kwamba wakakimbia hata maeneo yao ya asili!

Kuna bonde moja nadhani maeneo ya Ibaga au Kuelekea Msingi wazee wansema wabarbaig waliuawa sana kiasi kwamba mpaka leo hii ukitembelea maeneo hayo utapata mafuvu wa watu!
Baada ya uhuru, nguvu yao ilipungua kwa kuwa, walikuwa wakihamidhwa hamishwa kutokana na kugomea mabadiliko. So Serikali ilikuwa ikiwa-favour wakulima at the expense of Datooga.
Usiniulize sana, sina details za kujitosheleza. But ukweli utabakia palepale kuwa, makabila ya kifugaji kwenye vita yamekuwa juu kulinganisha na wakulima kutokana na wepesi wao wa kujikusanya.
Na kwa jinsi Kabila la Waisanzu lilivyo dogo, hakuna namna wangeweza kushindana na Wataturu basi tu. Tangu utotoni tumesoma ushujaa wao wa kuua simba ama mnyama mkali.
 
Baada ya uhuru, nguvu yao ilipungua kwa kuwa, walikuwa wakihamidhwa hamishwa kutokana na kugomea mabadiliko. So Serikali ilikuwa ikiwa-favour wakulima at the expense of Datooga.
Usiniulize sana, sina details za kujitosheleza. But ukweli utabakia palepale kuwa, makabila ya kifugaji kwenye vita yamekuwa juu kulinganisha na wakulima kutokana na wepesi wao wa kujikusanya.
Na kwa jinsi Kabila la Waisanzu lilivyo dogo, hakuna namna wangeweza kushindana na Wataturu basi tu. Tangu utotoni tumesoma ushujaa wao wa kuua simba ama mnyama mkali.
Nakushauri ukafanye katafiti kadogo maeneo hayo na hao Waisanzu!
 
Ndio hilo kabila la Stopa The Rhyme Maker Yokoi "WATURUTUMBI"? Style 3 Mtu M1.
 
Nakushauri ukafanye katafiti kadogo maeneo hayo na hao Waisanzu!
Ni ngumu kufanya hivyo kwa sababu Wadatooga wameshasambaratishwa na Wabantu. Nimeweka link hapo jaribu kuipitia. Mi nina uhakika Wambulu, Wanyilamba (+Waisanzu) na Wanyaturu waliwafanyia mbaya kwa msaada wa Serikali Kama ambavyo pia Wabantu waliwaua kikatili Wamasai kipindi chakula chao kikuu - mifugo ilipokufa kwa sotoka (rinderpest) in 1880s - 1890s.
Hata hivyo, unaonekana Wewe ni wa huko Mkalama Singida, so unaweza ukatusaidia humu ABC za mahusiano yenu jinsi yalivyokuwa enzi za kabla ya ukoloni kwani Waisanzu, Wanyilamba na Wanyaturu mmechukua genes nyingi za Hamites (Wairaq) na Nilotes (Wadatooga). Aidha, kipimo cha uwezo wa Kabila ni ukubwa wa eneo but katika Makabila yote ya katikati ya Tanzania - Singida, Tabora, Dodoma, Manyara, Shinyanga, Mwanza, Simiyu, Arusha, Iringa na Morogoro, Waisanzu (pamoja na Waiambi) ndo wenye maeneo madogo sana. Maeneo yao yanazidiwa na Wadatooga.
 
Wanaongea kama waarabu au kama wasomali vile, Mara ya kwaza kwenda Manyara vijijini ña kuwajua vizuri nilishangaa sana
 
Wanaongea kama waarabu au kama wasomali vile, Mara ya kwaza kwenda Manyara vijijini ña kuwajua vizuri nilishangaa sana

..hao uliokutana nao ni kabila la WA-IRAQW.

..wakati mwingine hutambulishwa kama Wa-Mbulu.

..maeneo yao ya asili ni wilaya za MBULU na KARATU.

..ila nimeshangaa unavyosema ulishangaa kukutana na hao ndugu zetu ulipokwenda mkoa wa Manyara.

..watu maarufu toka kabila la Wa-Iraqw ni kama Filbert Bayi, Dr.Slaa, Philip Marmo, Prof.Martha Qorro,..
 
Back
Top Bottom