Wateja 24 waliotorosha makontena kufilisiwa

Ashura9

JF-Expert Member
Joined
Oct 21, 2012
Posts
740
Reaction score
485
Wateja 24 waliotorosha makontena kufilisiwa





Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya YONO, Bw, Stanley Yono Kevela

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni hiyo Yono Kevela amesema hayo jana na kuongeza kuwa wamepewa amri na TRA, ya kisheria ya kukamata mali za wadaiwa na kuwafilisi ili kulipa kodi wanazodaiwa.

Bw. Kevela amesema baada ya kupata kazi hiyo wameona ni busara kutangaza na kuwapa siku 14 kulipa kodi wanazodaiwa na kwamba baada ya muda huo kumalizika hatua za kukamata mali za wadaiwa zitaanza.

Majina ya wadaiwa hao yametolewa jana kwa vyombo mbalimbali vya habari na kampuni hiyo ya udalali baada ya TRA, kuwakabidhi kazi ya kuwafilisi kutokana na kushindwa kutekeleza wajibu wao baada ya kupewa muda wa kufanya hivyo.

Kevela amesema ili kurahisisha kazi Kampuni ya Said Salim Bakharesa(SSB), ambayo ndiyo mmiliki wa bandari kavu pamoja na kampuni ya Regional Cargo Service wanapaswa kutoa ushirikiano kuhakikisha wadaiwa hao wanalipa kodi walizokwepa.
Chanzo: EATV
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…