Wateja Mjifunze kuheshimu wafanyabiashara, Wanajitoa kuliko Mnavyofikiria

Wateja Mjifunze kuheshimu wafanyabiashara, Wanajitoa kuliko Mnavyofikiria

CONTROLA

JF-Expert Member
Joined
Sep 15, 2019
Posts
7,001
Reaction score
23,449
Kuna hii kauli ya Mteja ni Mfalme ni moja ya kauli mbaya na ya dharau kwa wafanyabiashara, ni kauli ambayo siiipendi kuisikia hata kuona mtu anaitamka mbele ya macho yangu.

Pesa ni roho inayoambatana na matabia mengi sana nyuma yake,na moja ya tabia za mwenye pesa ni "dharau" hizi dharau zimejaa kwa wateja wengi sana wakiamini kwasababu wameshika Pesa basi bidhaa za wenzao ni taka taka.

leo acha niwambie nyie wateja Mkae mlijue hili kwa ufupi sana.

Hivi umeshawahi kwenda Hardware kutafuta cement ukaingia hardware ya 1 cement hamna (wanakwambia zimeisha) unaenda hardware ya pili (wanakwambia zimeisha pia) Anatokea mtu anakwambia Twende kwenye Hard ware Flani kule cement zipo,kweli unapelekwa unakuta cement ipo.

Hivi kabla hujatoa hiyo pesa yako ushawahi jiuliza maswali kwanini umezunguka hardware zingine zaidi ya 5 umekosa cement??? wakati na wao ni wauzaji wa cement tena wakubwa tu lakini hawana? unafikiri huyo mwenye cement yeye anazitengeneza hizo cement?

Watu wanajitoa hawataki wateja zao mteseke kwa kukosa bidhaaa,huko alipofata cement ukute aliuziwa kwa bei ya juuu lakini akaamua kulipa ili wateja mkija msikose, ukifata cement kuna foleni ya gari sio unaingia tu kiwandani unawekewa cement,magari yanapakia kwa foleni,hivi unajua gharama ya kupambana mpaka gari yako inakaa kwenye foleni kuanza kupakia cement? Tutoke huko..

Umeshawahi kwenda ilala au karume sokoni asubuhi saa 11 au 10 alfajiri ukaona wafanyabiashara wanavyogombania Viatu na Nguo? mimi ni mmoja wa wafanyabiashara ambae nauza viatu vya mtumba,unaweza kwenda karume sokoni kufata viatu vimemwagwa kilaa mtu anachagua kiatu,Bahat mbaya kwenye kuchagua nikashika kiatu cha mguu wa kushoto nimekiona kizuri, sasa inabdi nitafute kiatu cha mguu wa kulia ili pair ikamilike...

wakati natafuta kiatu cha mguu wa kulia kuna mwenzangu pembeni nae kashakidaka kiatu cha mguu wa kulia anatafuta cha mguu wa kushoto,tunakutana uso kwa uso mimi nina cha mguu wa kushoto,yeye ana chamguu wakulia, Namwambia Oyaaaa nipe mguu huo mimi ndio nimewahi kukiona,Jamaaa anakataaa na yeye anasema ndio kawahi,kinachofuata mnajua ni nini nyie wateja?

kama tumekutana wastarabu tunakubaliana mimi nampa hela kidogo ananipa mguu wa kulia,au yeye ananipa hela kidogo mimi nampa mguu wa kushoto,ila kama tumekutana wote tumevurugwa Hiyo siku lazima tushikane shkane vuta nikuvute mwenye nguvu anampokonya mwenzake kiatu... Tutoke huko

Umeshawahi kwenda kariakoo j3 ukaona wale madogo wanaonunua CD wakauze namna wanazigombania zile CD as if wanapewa bure,msukumano wake na mvutano wake ukiwaangalia unaweza hisi zile CD wanapewa bure hawatoi hela, Tutoke huko

Wauza magenge mitaani hivi umeshawahi kuwakuta wakiwa sokoni wanakusanya mzigo wa gengeni namna wanahangaika, ni mara ngapi unaenda gengeni kununua nyanya unakosa karoti? genge la kwanza karoti hamna,la pili karoti hamna, unaenda genge la 4 unakuta ana karoti Hivi unajua imekuaje wenzake hawana karoti halafu yeye anazo,unahisi ana shamba la karoti nyumban kwake nn? Wateja muwe mnajiuliza hayo maswali... Tutoke huko

Hivi mnajua kasheshe za kutoa mzigo pale bandarini? Mpaka kontena lako linafikiwa hivi mtiti wake mnahisi unakuaga automaticaly eeeh? watu wanapigana/wanagombana/wanashushiana heshima/wanalogana/wanauana, nk nk

Mifano ni mingi,unapoenda mahali kununua kitu acheni ujuaji mwingi, Ukitajiwa bei Lipia kama unaona kubwa omba kistarabu upunguziwe usipoeleweka ondoka kistarabu acha kujitia unajua sana bei za bidhaaa kama unamiliki kiwanda cha sukari...

Mteja anakuja dukani unamwambia karibu,Hakujibu kitu unamuacha ashangae unakaa zako chini maana umechoka na mihangaiko,Unamskia bila aibu "we kijana huoni naangalia vitu si usimame" sasa mimi nisimame ili iweje? umetaka nini ukaacha kutolewa? wateja madharau muache Pesa zenu hazina thamani ya nguvu na utu tunaojitoa na kuupoteza kupata hizo bidhaaa mnazoziona zimekaa kwenye mashelf...

Ukija ofisini kwangu Ufalme unaishia huko kwenu,ukiingia ofisini kwangu "we are all equal" Tuheshimiane, pesa yako ingekua na thamani sana ungeikaaanga uinywe na chai, ungeikoroga uinywe uji, lakini ili ujue hiyo pesa yako si kitu haiwezi fanya yote hayo ndio mana umeileta kwangu tubadilishane,sasa usijione kwamba unachonipa kina Thamani kuliko ninachokupa Mimi.

Hiyo sukari ninayokupimia,gas ninayokuuzia,kiatu ninachokuuzia,chakula ninachokuuzia kina Utu wangu ndani yake,nimetukanwa sana kwa ajili ya hiyo bidhaaa,nimepigana sana kwa ajili ya hiyo bidhaa,nimedhalilishwa so Wateja jaribuni kuheshimu tena heshima yenu itoke ndani ya moyo msi force maana wafanyabiashara wanajitoa kuliko hata haya niliyoyaelezea hapa.

Muuzaji na Mteja wote ni sawa

Muuzaji na Mteja wote ni wafalme

Dharau ziache kwako/kwenu ukienda ofisi za watu fata taratibu/kanuni/sheria zilizowekwa hudumiwa sepa zako.
 
Kuna hii kauli ya Mteja ni Mfalme ni moja ya kauli mbaya na ya dharau kwa wafanyabiashara,ni kauli ambayo siiipendi kuisikia hata kuona mtu anaitamka mbele ya macho yangu.

Punguza jazba ndugu,binadamu tumetofautiana.Hata mimi pia hiyo pesa ninayokupa mpaka naipata Utu wangu niliweka rehani pia.

Mteja ni mfalme,itabaki kuwa hivyo na haijalishi unataka au hutaki!

Unyenyekevu ni muhimu sana kwenye biashara yoyote ile,kama mtu hajakutukana anakuvunjia vipi heshima ili hali mkishindwana anajiondokea zake!

Punguza huo umwinyi.
 
Pole mleta mada.

Nadhani una tatizo la kuangalia vitu vidogo na kutilia manani. Wewe una malengo yako. Mapambano ya kupata hizo bidhaa yanafaa yawe pia mapambano ya kuuza. Hivi vi-stori vya katikati ili uonewe huruma hakuna tija.

Wewe pambana.

Lakini pia kumbuka kuwa wewe ni muuzaji wa kitu kimoja na mnunuzi wa hicho kitu na kinginecho.

Jiulize wewe ni mteja wa aina gani.
 
Ukitaka kulielewa vizuri hilo somo
Soma kitabu cha joeli nanauka kinaitwa saikilojia ya mteja. Utakuja kujua kwanini mteja anunue kwako.
 
Na utaishia kuiuzia familia yako tu kwa mentality hiyo,hufai kuwa mfanyabiashra,wafanyabiashara hawana tabia hiyo,na wenye tabia hiyo hawadumu katika biashara zao.
 
Kama unaona wateja wanadharau si uache hiyo kazi ujue kwenda kupigania viatu karume sio unamuangaikia mteja unatafuta bidhaa nzuri ili uje uuze kwa haraka na faida kubwa huyo mteja nae ujue hiyo pesa anatokupa ww ameipata kwa njia gan,wengine tunatoka kuoga kwenye matope plus zege ili tupate hela ya kukuletea ww.
N:B,maisha ni vita broo utakutana na misukosuko mingi ili uweze ku win
 
Dah asee kuna watu wana dharau sana kuna siku nimeingia dukani sasa naongea bei na muuzaji kaingia mother flani akaanza kuongea maneno tu ya hovyo mbaka anatukana ikabidi mimi nitulie yule dada muuzaji akaongea na yule mother alipotoka nkampa pole yule dada kwa kazi ngumu ya kuvumilia wateja wakorofi.
 
Kama unaona wateja wanadharau si uache hiyo kazi ujue kwenda kupigania viatu karume sio unamuangaikia mteja unatafuta bidhaa nzuri ili uje uuze kwa haraka na faida kubwa huyo mteja nae ujue hiyo pesa anatokupa ww ameipata kwa njia gan,wengine tunatoka kuoga kwenye matope plus zege ili tupate hela ya kukuletea ww.
N:B,maisha ni vita broo utakutana na misukosuko mingi ili uweze ku win
Hata kama wewe unakua umeipata kwa kazi ngumu nd utukane watu wanaouza bidhaa flani eti kisa tu wewe umepata hela iyo kwenye zege, hapana kabisa Mkuu inabidi tu uwe mstaarabu basi Ila kuna situation nyingn wauzaji nao wanazingua unaweza kuta muuzaji ana nyodo kinoma alaf ukifikilia the way ulivopata hela yako lazma utukane mtu asee
 
SAFI SANA, SAFI SANA

WATANZANIA WENGI WAPO HIVYO, kwa sababu tu yeye ni mteja na anataka kununua kwako basi anakufanya mtumwa na atakusumbua mpaka unaweza kuacha biashara

Wamelelewa na kuamini hivyo kwamba mteja ni mfalme > ni upumbavu mkubwa.

Mimi binafsi mteja kwangu 'ni ndugu na rafiki yangu wa karibu' ila siyo mfalme na nikionaga tu mteja mpumbavu hata kama ana hela na anahitaji bidhaa huwa nawablock tu.

Sina uwezo wa kuhudumia wafalme mimi.

Namna nzuri ya kufanya biashara ni kuajiri wengine wafanye badala yako ila ukifanya mwenyewe mmiliki unaweza kuahirisha

By the way mimi napanga kustaafu kazi au biashara za kuhudumia watu mapema iwezekanavyo, nataka kufanya shughuli zisizo lazimu kuonana au kuwasiliana na wateja tena wateja wengi kila siku kwani zinachosha na zinazeesha mapema
 
Umeandika vizuri sana mkuu uzi wako!
Mtu aliyetulia ndiye pekee atauelewa.
Ila kwa mtu jamii ya kiberenge hawezi kukuelewa!
 
SAFI SANA, SAFI SANA

WATANZANIA WENGI WAPO HIVYO, kwa sababu tu yeye ni mteja na anataka kununua kwako basi anakufanya mtumwa na atakusumbua mpaka unaweza kuacha biashara

Wamelelewa na kuamini hivyo kwamba mteja ni mfalme > ni upumbavu mkubwa.

Mimi binafsi mteja kwangu 'ni ndugu na rafiki yangu wa karibu' ila siyo mfalme na nikionaga tu mteja mpumbavu hata kama ana hela na anahitaji bidhaa huwa nawablock tu.

Sina uwezo wa kuhudumia wafalme mimi.

Namna nzuri ya kufanya biashara ni kuajiri wengine wafanye badala yako ila ukifanya mwenyewe mmiliki unaweza kuahirisha

By the way mimi napanga kustaafu kazi au biashara za kuhudumia watu mapema iwezekanavyo, nataka kufanya shughuli zisizo lazimu kuonana au kuwasiliana na wateja tena wateja wengi kila siku kwani zinachosha na zinazeesha mapema
Kuongea/kuonana na mteja sio WITO wako mkuu, usilazimishe ajiri watu wenye passion na hiyo sector!.
 
Kuongea/kuonana na mteja sio WITO wako mkuu, usilazimishe ajiri watu wenye passion na hiyo sector!.
Ni mtu mwenye akili ndiyo anaweza kunielewa nini nimeandika siyo wewe

Siku hizi hatuangalii tena mambo ya wito wala passion

Siyo lazima nikuuzie bidhaa hata kama wewe ni mteja, ninao uwezo wa kukublock ukanunue kwa wengine huko na siyo uniletee upumbavu wako kisa una vihela

Wapo wanaonielewa na nafanya nao kazi ila mapumbavu huwa nayablock tu and I have nothing to lose
 
Kuna Mshamba mmoja juzi nataka kununua kilo kadhaa za nyama akaanza kunletea pigo flani za kichoko!

Namwambia nataka nyama nzuri, kantolea stake nzuri ..,hii stake 12,000. Ya kawaida 8,000 nikwambia hebu pima hio ya kawaida kaniwekea nyama inamafupa karibia nusu kilo nzima ni mafupa tu😅 nikamwambia hio hapana! Nataka kilo 2 ntalipia stake 10,000 na unipe na kilo ingine hio ya kawaida sasa ila unipe nyama fresh!

Kaniwekea pande la stake akaongezea nyama ikafika 1.0 kgs nikamwambia hapo freshi kacheki mzani eti akaanza kupunguza ikafika 0.8 eti oh nilizidisha. Kushika ile nyama naskia ni ya baridi nikamwambia hii nyama mbona kama imelelala yani ndaza.

Kaanza ooh nyama haijalala bana we naona kama unazingua kama vipi baki na hela yako tu complain nyingi! Nikamwambia sio kesi nikasepa. Nikaenda nunua bucha ingine pembeni jamaa alini treat vizuri sana akanipimia nyama fresh kwa jinsi ambavyo nilihitaji!
 
Ni mtu mwenye akili ndiyo anaweza kunielewa nini nimeandika siyo wewe

Siku hizi hatuangalii tena mambo ya wito wala passion

Siyo lazima nikuuzie bidhaa hata kama wewe ni mteja, ninao uwezo wa kukublock ukanunue kwa wengine huko na siyo uniletee upumbavu wako kisa una vihela

Wapo wanaonielewa na nafanya nao kazi ila mapumbavu huwa nayablock tu and I have nothing to lose
Ni ngumu kutatua tatizo ambalo unaamini hauna...
 
Ni ngumu kutatua tatizo ambalo unaamini hauna...
Siku hizi kama upo bize na passion na wito unapoteza muda wako bure

Huyu mleta mada ana akili sana nimemkubali mno sababu ameongea ukweli mtupu

Kama unataka kununua bidhaa kwangu uwe na adabu ila kama unafikiri vihela vyako ndiyo mhimu kuliko bidhaa au huduma yangu potelea huko. Wapo waelewa hao ndiyo nitakuwa bize nao siyo kila mtu tu hata chizi wa hela

Money is important but it's not everything
 
Back
Top Bottom