Watendaji wa Kata, Vijiji na Mitaa marufuku kumweka ndani mtuhumiwa kwa Saa 24

Watendaji wa Kata, Vijiji na Mitaa marufuku kumweka ndani mtuhumiwa kwa Saa 24

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Watendaji wa kata, vijiji au mitaa wametakiwa kuacha tabia ya kuwakamata watuhumiwa na kuwaweka ndani saa 24 ikielezwa kuwa hawana mamlaka kisheria.

Kauli hiyo imetolewa na Mkufunzi wa Elimu ya Uraia na Utawala Bora kutoka Wizara ya Mambo ya Ndani, Iddah John wakati akitoa ufafanuzi wa swali lililoulizwa na Mtendaji wa Kata wa Misungwi, Vicent Wana ambaye aliomba kupata ufafanuzi wa sheria inayowapa mamlaka watendaji kuruhusiwa kumkamata na kumweka ndani mtuhumiwa ndani ya saa 24.

Kupata taarifa na matukio yanayojiri kuelekea uchaguzi mkuu kwa kila mkoa ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Akiunga mkono hoja hiyo Afisa Tawala Mwandamizi Ofisi ya Rais- TAMISEMI, Mashaka Makuka amewataka watendaji kuacha tabia hiyo huku akisisitiza kuwafikisha watuhumiwa kwenye vyombo husika vyenye mamlaka ya kukamata na kuweka ndani.

CHANZO: Jambo TV
 
Watendaji wa kata, vijiji au mitaa wametakiwa kuacha tabia ya kuwakamata watuhumiwa na kuwaweka ndani saa 24 ikielezwa kuwa hawana mamlaka kisheria.

Kauli hiyo imetolewa na Mkufunzi wa Elimu ya Uraia na Utawala Bora kutoka Wizara ya Mambo ya Ndani, Iddah John wakati akitoa ufafanuzi wa swali lililoulizwa na Mtendaji wa Kata wa Misungwi, Vicent Wana ambaye aliomba kupata ufafanuzi wa sheria inayowapa mamlaka watendaji kuruhusiwa kumkamata na kumweka ndani mtuhumiwa ndani ya saa 24.

Akiunga mkono hoja hiyo Afisa Tawala Mwandamizi Ofisi ya Rais- TAMISEMI, Mashaka Makuka amewataka watendaji kuacha tabia hiyo huku akisisitiza kuwafikisha watuhumiwa kwenye vyombo husika vyenye mamlaka ya kukamata na kuweka ndani.

Ni kukosa uadilifu na utumiaji wa Madaraka vibaya . Jambo jingine uwezo wao yd kutumia hayo madaraka
 
Kwa chama kipi? Ni hiki hiki chakavu au kingine? Chama kisichokuwa na utawala wa sheria kuanzia mashinani mpaka idara za kitaifa. Ndio chama hicho hicho kilichowatuma akina Bashite na Sabaya kuwatesa watu bila hatia na kuwaweka ndani huku jiwe akichekelea chooni. Watu wasiokuwa na hatia wamepoteza mali zao na viungo vyao huku Bashite na Sabaya wakipeta mtaani bila wasiwasi sababu chama chakavu kinawalinda.

Eti leo hii ndio chama hicho hicho kinawaambia watendaji wake hakuna kumuweka mtu ndani saa 24 wakati kimeshindwa kuwachukulia hatua akina Bashite na Sabaya kwa ukatili walioufanya kwa binadamu wenzao? Bata wahed!
 
Na mtendaji mpaka akukamatishe na migambo wake walioishiwa nguvu na akuweke ndani automatically lazima na wewe uwe ni raia dhaifu hapo kijijini ,kiuchumi ,kijamii ,kiintelenjensia na mwisho usiyetakiwa katika hiyo kata
 
Back
Top Bottom