LGE2024 Watendaji wa kwenye Serikali Za Mitaa, epukaneni na mtego huu

LGE2024 Watendaji wa kwenye Serikali Za Mitaa, epukaneni na mtego huu

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Mushkov

JF-Expert Member
Joined
Feb 16, 2024
Posts
357
Reaction score
686
Tunapoelekea kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa, kumekuwa na ripoti za kuenguliwa kwa wagombea, hususan wa upinzani, na wanaotekeleza hayo ni ninyi watendaji wa mitaa. Naomba kuwaasa ndugu zangu, epukaneni na mtego huu.

Kumbukeni kuwa wale wanaowaagiza mfanye hivyo wana ulinzi masaa 24. Wanalindwa kikamilifu, hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi na hata baada ya uchaguzi.

Ninawaona kama mmetolewa kafara kwa manufaa ya watu wengine.

Igeni mfano wa watendaji kadhaa huku kwetu ambao wamekataa katakata kufanya hujuma hizo na wamesema wako tayari kufukuzwa kazi kwa ajili ya msimamo huo. Huku kwetu, hakuna mtu hata mmoja aliyeenguliwa.

Nawatakia majukumu mema.
 
Haki huinua taifa bali dhambi ni aibu ya watu wowote. Endeleeni na dhuluma maana kuna siku ya mavuno.
 
Hawa wapuuzi wanaojiita wasimamizi wa uchaguzi washitakiwe wao kama wao kwa kutaka kuchafua uchaguzi.

Hii ndiyo dawa yao.
 
Haki huinua taifa bali dhambi ni aibu ya watu wowote. Endeleeni na dhuluma maana kuna siku ya mavuno.
Hizi kauli za kusubiri Haki ya Mungu CCM huwa wanazipenda saana.

Kumbuka hata kipindi cha Sauli - Mungu alimwambia Sauli nyenyuka ukawapiganie watu wangu..

Mbona hakumwambia kaa tu usubiri hukumu siku ya mwisho.
 
Hizi kauli za kusubiri Haki ya Mungu CCM huwa wanazipenda saana.

Kumbuka hata kipindi cha Sauli - Mungu alimwambia Sauli nyenyuka ukawapiganie watu wangu..

Mbona hakusema kaa tu usubiri hukumu siku ya mwisho.
Hapo nimekuelewa. Upo sasa kabisa. Yaani, unamkuta jamaa anakuibia mke wako badala ya kumshikisha adabu, unasubiri huruma ya Mungu.
Mungu mwenyewe huwa hamsaidii mtu ambaye anapata tatizo, badala ya kupambana na lile tatizo mpaka uwezo wake unapoishia yeye anakaa kimya kusubiri huruma ya Mungu.
 
Hii dhambi ya kunyonga uchaguzi wa serikali za mitaa ilimpeleka kuzimu Yule Mzee 2021.....Hii dhambi imeanza kupiga hodi huko Cuba
Bila ya shaka yoyote na kama Mungu aishivyo huyo anayeshinikiza ujambazi huu atakinywea kikombe kile kile alichonywea yule dhalim aliyeko kuzimusasa hivi.
 
Hauna Cha kuwafanya hao watendaji, vinginevyo utafungwa na kufilisiwa.

Mngedili na wakurugenzi tu muachane na vidagaa
 
Hauna Cha kuwafanya hao watendaji, vinginevyo utafungwa na kufilisiwa.

Mngedili na wakurugenzi tu muachane na vidagaa
Wakishughulikiwa hawa wataogopa kutekeleza maagizo ya kipumbavu,itokee wafanyiwe kitu mbaya kama 400 kwa nchi nzima hakuna ambaye atakuja kupokea amri haramu tena, kuna wengi tu wamekataa kutii amri haramu hii kwani ni uvunjaji wa sheria.
 
Wakishughulikiwa hawa wataogopa kutekeleza maagizo ya kipumbavu,itokee wafanyiwe kitu mbaya kama 400 kwa nchi nzima hakuna ambaye atakuja kupokea amri haramu tena, kuna wengi tu wamekataa kutii amri haramu hii kwani ni uvunjaji wa sheria.
Hakuna mtendaji WA kuzinda kutii amri ya mkurugenzi iwe halali au haramu iliyohalalishwa.


Narudia, hakuna mtu anaweza kumgomea boss wake kwenye amri haramu iliyohalalishwa akabaki salama.


OGOPA sana maelekezo kutoka juu.
 
Wakishughulikiwa hawa wataogopa kutekeleza maagizo ya kipumbavu,itokee wafanyiwe kitu mbaya kama 400 kwa nchi nzima hakuna ambaye atakuja kupokea amri haramu tena, kuna wengi tu wamekataa kutii amri haramu hii kwani ni uvunjaji wa sheria.
Upo sahihi kabisa. Je, wangeambiwa wamnyonge mtoto au mzazi wao wangekubali?
Bila shaka wasingekubali. Wangeona ni afadhali kufukuzwa kazi kuliko kutenda jinai hiyo.
 
Back
Top Bottom