Watetezi wa Mo acheni fikra za Kinyonge, Mo ni mfanyabiashara sio mfanya hisani

Watetezi wa Mo acheni fikra za Kinyonge, Mo ni mfanyabiashara sio mfanya hisani

Wildlifer

JF-Expert Member
Joined
May 12, 2021
Posts
1,884
Reaction score
5,235
Mwaka 2008, nakumbuka nilisafiri kwenda huko Mpanda. Sasa basi tulilopanda, lilichelewa sana kuondoka. Abiria tulianza lalamika. Kondakta wa basi akatujibu 'kwanza hampaswi kulalamika, inabidi mumshukuru sana huyu Ali, maana amewasaidia sana kwa kuweka basi kwenye njia hii'. Kauli ile ilinikera sana, sababu huyo tajiri, habebi abiria bure, tunalipa nauli. Yeye anapata faida. Maana yake ameona sisi wasafiri na njia ile ni fursa. Hivyo, ni win win situation! Hatupi huduma. Nimemkumbuka kondakta huyu, baada ya kufuatilia Issue ya Manara.

Mjadala unaondelea dhidi ya Manara Vs Mo, watetezi wa Mo wanamjengea taswira kuwa ni mtu aliyejitolea kwa simba, ni mtu aliyetoa hela yake, na ameikoa Simba. Ni kama vile ameifanyia Hisani. Mimi siko upande wa Manara wala Mo, Sababu sijui mkweli nani. Ila hoja yangu, ni kuwataka mashabiki wa simba watetezi wa Mo, kuacha fikra za watu 'waliolewa dhiki ya maisha'. Ukilewa dhiki ya maisha, chochote kinachokuja maishani mwako, utaona hisani.

Simba ni klabu kongwe barani afrika. Ni klabu yenye mamilioni ya mashabiki. Hata mtoto anayezaliwa leo, lazima atakuwa na upande mmoja wa simba au yanga. Simba na Yanga, ni utambulisho wa Utanzania. Hivyo timu hizi ni bidhaa ambayo hata Sheikh Mansour anaweza itolea macho. Mtaji mkubwa wa Simba ni mashabiki, wafuasi, wanazi na wakereketwa. Hii ni hela. Ndio maana Mo, hakwenda Coastal Union au Pamba ya Mwanza, au kukomaa na African Lyon yake, au Singida United ya kwao Singida, anajua Simba (& Yanga) inacho ambacho Timu zote za Tanzania hazina; inacho ambacho matajiri wote wa Mpira wanakitaka. FAN BASE. Hivyo, Simba ni bidhaa ambayo haihitaji kubembeleza au kutukuza mtu! Ni Almasi Nyeusi. Hata Mo asingekuwepo, wawekezaji kwa Simba hawakosekani.

Kitu alicho nacho Mo (na alikuwa nacho Manji) wanajua kucheza na akili za mashabiki. Wanajua shida ya mashabiki wa Simba na Yanga. Wanajua ni wakereketwa wa Timu hizi. Wanajua matatizo ya miaka mingi ya timu hizi ni fedha. Wanajua ni watu wa kulewa mafanikio madogo madogo. Wanajua mkiishia Robo fainali ya CAF mnaridhika. Wanajua mkiifunga Yanga, mmeridhika kuliko Kuchukua Kombe. Wanajua mkiifunga Al Ahly ni kama mmetwaa Kombe la Shirikisho. Wanajua tuna fikra kama ya watu wenye lindi la umaskini. Hata anayekupa msaada wa pipi, huyo ni kama Masiah.

Tuache Ushamba, Simba na Yanga ni bidhaa za thamani sana. Na Mo anaihitaji Simba kuliko Simba inavyomuhitaji Mo.


Sent from my Infinix X688B using JamiiForums mobile app
 
Tunampenda Mo iwe jua iwe mvua, akiamua anaweza kuleta mchezaji yeyote wa Africa pale nsimbazi.
Yaani kwa lugha nyingine tunamuita sponsor hatari sana

#nguvumoja
 
Tunampenda Mo iwe jua iwe mvua, akiamua anaweza kuleta mchezaji yeyote wa Africa pale nsimbazi.
Yaani kwa lugha nyingine tunamuita sponsor hatari sana

#nguvumoja
Ni haki yako Kumpenda.
 
  • Thanks
Reactions: mmh
Mwaka 2008, nakumbuka nilisafiri kwenda huko Mpanda. Sasa basi tulilopanda, lilichelewa sana kuondoka. Abiria tulianza lalamika. Kondakta wa basi akatujibu 'kwanza hampaswi kulalamika, inabidi mumshukuru sana huyu Ali, maana amewasaidia sana kwa kuweka basi kwenye njia hii'. Kauli ile ilinikera sana, sababu huyo tajiri, habebi abiria bure, tunalipa nauli. Yeye anapata faida. Maana yake ameona sisi wasafiri na njia ile ni fursa. Hivyo, ni win win situation! Hatupi huduma. Nimemkumbuka kondakta huyu, baada ya kufuatilia Issue ya Manara.

Mjadala unaondelea dhidi ya Manara Vs Mo, watetezi wa Mo wanamjengea taswira kuwa ni mtu aliyejitolea kwa simba, ni mtu aliyetoa hela yake, na ameikoa Simba. Ni kama vile ameifanyia Hisani. Mimi siko upande wa Manara wala Mo, Sababu sijui mkweli nani. Ila hoja yangu, ni kuwataka mashabiki wa simba watetezi wa Mo, kuacha fikra za watu 'waliolewa dhiki ya maisha'. Ukilewa dhiki ya maisha, chochote kinachokuja maishani mwako, utaona hisani.

Simba ni klabu kongwe barani afrika. Ni klabu yenye mamilioni ya mashabiki. Hata mtoto anayezaliwa leo, lazima atakuwa na upande mmoja wa simba au yanga. Simba na Yanga, ni utambulisho wa Utanzania. Hivyo timu hizi ni bidhaa ambayo hata Sheikh Mansour anaweza itolea macho. Mtaji mkubwa wa Simba ni mashabiki, wafuasi, wanazi na wakereketwa. Hii ni hela. Ndio maana Mo, hakwenda Coastal Union au Pamba ya Mwanza, au kukomaa na African Lyon yake, au Singida United ya kwao Singida, anajua Simba (& Yanga) inacho ambacho Timu zote za Tanzania hazina; inacho ambacho matajiri wote wa Mpira wanakitaka. FAN BASE. Hivyo, Simba ni bidhaa ambayo haihitaji kubembeleza au kutukuza mtu! Ni Almasi Nyeusi. Hata Mo asingekuwepo, wawekezaji kwa Simba hawakosekani.

Kitu alicho nacho Mo (na alikuwa nacho Manji) wanajua kucheza na akili za mashabiki. Wanajua shida ya mashabiki wa Simba na Yanga. Wanajua ni wakereketwa wa Timu hizi. Wanajua matatizo ya miaka mingi ya timu hizi ni fedha. Wanajua ni watu wa kulewa mafanikio madogo madogo. Wanajua mkiishia Robo fainali ya CAF mnaridhika. Wanajua mkiifunga Yanga, mmeridhika kuliko Kuchukua Kombe. Wanajua mkiifunga Al Ahly ni kama mmetwaa Kombe la Shirikisho. Wanajua tuna fikra kama ya watu wenye lindi la umaskini. Hata anayekupa msaada wa pipi, huyo ni kama Masiah.

Tuache Ushamba, Simba na Yanga ni bidhaa za thamani sana. Na Mo anaihitaji Simba kuliko Simba inavyomuhitaji Mo.


Sent from my Infinix X688B using JamiiForums mobile app
Mo kawekeza simba ili mwisho wa siku timu ianze kuzalisha faida, kitu ambacho kwa miaka takribani 80 kilishindikana kbsa...sasa hapo tatizo la mo lipo wapi?

Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
 
Mo kawekeza simba ili mwisho wa siku timu ianze kuzalisha faida, kitu ambacho kwa miaka takribani 80 kilishindikana kbsa...sasa hapo tatizo la mo lipo wapi?

Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
Sina tatizo na Mo kuwekeza. Ni kitu kizuri sana kwa Maendeleo ya nchi yetu. Hoja yangu, ni kupinga dhana kuwa Mo ameisaidia Simba. Wakati amewekeza akitegemea faida.
 
Kama wewe mwanamke usiolewe na Tajiri lazima uwe na uvumilivu.
 
Tunampenda Mo iwe jua iwe mvua, akiamua anaweza kuleta mchezaji yeyote wa Africa pale nsimbazi.
Yaani kwa lugha nyingine tunamuita sponsor hatari sana

#nguvumoja
Anamiliki asilimia ngapi???.
 
Huu uswahili uswahili tunaoufanya hapa bongo ndio umetufanya mpk Leo vilabu vyetu vikongwe simba na yanga vimekosa ht uwanja km timu zingine tunazoona mafanikio km mazembe n.k tumeendeleza uswahili uswahili na majungu tupu
 
Sasa kama unajuwa kuwa MO ni Mfanya biashara kwanini munalialia kuwa MO anatengeneza hela pale Simba?
Hivi Uto mumeanza lini kubwa wasemaji wa Simba na Manara?
 
kawoli ni shabiki wa Mwamedi. Ukimkosoa tu Mwamedi, ytaporomoshewa matusi weeee. Uzuri ni mmoja tu, hakuna tusi jipya chini ya jua
 
Tunampenda Mo iwe jua iwe mvua, akiamua anaweza kuleta mchezaji yeyote wa Africa pale nsimbazi.
Yaani kwa lugha nyingine tunamuita sponsor hatari sana

#nguvumoja
na wasiwasi na elimu na utashi wako hivi una cheti cha form 4 kwanz kabla cjaenda mbali?
 
Sina tatizo na Mo kuwekeza. Ni kitu kizuri sana kwa Maendeleo ya nchi yetu. Hoja yangu, ni kupinga dhana kuwa Mo ameisaidia Simba. Wakati amewekeza akitegemea faida.
Miye ni mfuasi wa mo liwe jua au mvua sababu ni zifuatazo,
mositangu kuanzishwa kwa hii haijawahi kumiliki uwanja wa mazoezi kipindi cha uwekezaji wa mo imewezekana
Pili simba ameweza kushika nafasi ya 12 kwa ubora afrika zaidi ya yote kuiwezesha nchi kupata nafasi nne za uwakilishi kabla ya mo sikuyaona
Tatu, simba ameweza kuchukua vpl mara 4 mfululizo baada ya kulikosa mara 3 mfululizo
Nb: Hao wawekezaji unaosema watakuja kuwekeza simba walikuwa wapi kabla ya mo?
Au wamesubiri mo ameweka misingi mizuri ya uwekezaji na kupandisha thamani ya simba na ligi kwa ujumla ndiyo wanaona mo hafai?

Niombe nikuulize, Miye mshabiki wa simba/chelsea niliye huku rukwa vijijini inanihusu nini kama mo/ abromovic akiimiliki simba/chelsea kuna faida yoyote nitapata zaidi ya furaha ya ushindi na kombe?
 
Mwaka 2008, nakumbuka nilisafiri kwenda huko Mpanda. Sasa basi tulilopanda, lilichelewa sana kuondoka. Abiria tulianza lalamika. Kondakta wa basi akatujibu 'kwanza hampaswi kulalamika, inabidi mumshukuru sana huyu Ali, maana amewasaidia sana kwa kuweka basi kwenye njia hii'. Kauli ile ilinikera sana, sababu huyo tajiri, habebi abiria bure, tunalipa nauli. Yeye anapata faida. Maana yake ameona sisi wasafiri na njia ile ni fursa. Hivyo, ni win win situation! Hatupi huduma. Nimemkumbuka kondakta huyu, baada ya kufuatilia Issue ya Manara.

Mjadala unaondelea dhidi ya Manara Vs Mo, watetezi wa Mo wanamjengea taswira kuwa ni mtu aliyejitolea kwa simba, ni mtu aliyetoa hela yake, na ameikoa Simba. Ni kama vile ameifanyia Hisani. Mimi siko upande wa Manara wala Mo, Sababu sijui mkweli nani. Ila hoja yangu, ni kuwataka mashabiki wa simba watetezi wa Mo, kuacha fikra za watu 'waliolewa dhiki ya maisha'. Ukilewa dhiki ya maisha, chochote kinachokuja maishani mwako, utaona hisani.

Simba ni klabu kongwe barani afrika. Ni klabu yenye mamilioni ya mashabiki. Hata mtoto anayezaliwa leo, lazima atakuwa na upande mmoja wa simba au yanga. Simba na Yanga, ni utambulisho wa Utanzania. Hivyo timu hizi ni bidhaa ambayo hata Sheikh Mansour anaweza itolea macho. Mtaji mkubwa wa Simba ni mashabiki, wafuasi, wanazi na wakereketwa. Hii ni hela. Ndio maana Mo, hakwenda Coastal Union au Pamba ya Mwanza, au kukomaa na African Lyon yake, au Singida United ya kwao Singida, anajua Simba (& Yanga) inacho ambacho Timu zote za Tanzania hazina; inacho ambacho matajiri wote wa Mpira wanakitaka. FAN BASE. Hivyo, Simba ni bidhaa ambayo haihitaji kubembeleza au kutukuza mtu! Ni Almasi Nyeusi. Hata Mo asingekuwepo, wawekezaji kwa Simba hawakosekani.

Kitu alicho nacho Mo (na alikuwa nacho Manji) wanajua kucheza na akili za mashabiki. Wanajua shida ya mashabiki wa Simba na Yanga. Wanajua ni wakereketwa wa Timu hizi. Wanajua matatizo ya miaka mingi ya timu hizi ni fedha. Wanajua ni watu wa kulewa mafanikio madogo madogo. Wanajua mkiishia Robo fainali ya CAF mnaridhika. Wanajua mkiifunga Yanga, mmeridhika kuliko Kuchukua Kombe. Wanajua mkiifunga Al Ahly ni kama mmetwaa Kombe la Shirikisho. Wanajua tuna fikra kama ya watu wenye lindi la umaskini. Hata anayekupa msaada wa pipi, huyo ni kama Masiah.

Tuache Ushamba, Simba na Yanga ni bidhaa za thamani sana. Na Mo anaihitaji Simba kuliko Simba inavyomuhitaji Mo.


Sent from my Infinix X688B using JamiiForums mobile app
Utopolo mnatakiwa mjue kua GSM ni mfanyabiashara sio mtoa hisani
 
Miye ni mfuasi wa mo liwe jua au mvua sababu ni zifuatazo,
mositangu kuanzishwa kwa hii haijawahi kumiliki uwanja wa mazoezi kipindi cha uwekezaji wa mo imewezekana
Pili simba ameweza kushika nafasi ya 12 kwa ubora afrika zaidi ya yote kuiwezesha nchi kupata nafasi nne za uwakilishi kabla ya mo sikuyaona
Tatu, simba ameweza kuchukua vpl mara 4 mfululizo baada ya kulikosa mara 3 mfululizo
Nb: Hao wawekezaji unaosema watakuja kuwekeza simba walikuwa wapi kabla ya mo?
Au wamesubiri mo ameweka misingi mizuri ya uwekezaji na kupandisha thamani ya simba na ligi kwa ujumla ndiyo wanaona mo hafai?

Niombe nikuulize, Miye mshabiki wa simba/chelsea niliye huku rukwa vijijini inanihusu nini kama mo/ abromovic akiimiliki simba/chelsea kuna faida yoyote nitapata zaidi ya furaha ya ushindi na kombe?
Huo uwanja wa mazoezi aliununua huyo Moo? Na hizo nyasi bandia si zilitokana na hela za Okwi, kiasi cha kusababisha akina Evans Aveva, Geofrey Nyange na Hans Pope kuingia matatani baada ya kuzifuja hizo milioni 300!

Yeye kusaidia tu ujenzi, ndiyo uwanja amejimilikisha! Eti Mo Arena!! 😏
 
Back
Top Bottom