Wateule wa Rais Awamu ya Sita kitanzi shingoni

Wateule wa Rais Awamu ya Sita kitanzi shingoni

mwengeso

JF-Expert Member
Joined
Nov 27, 2014
Posts
9,227
Reaction score
6,670
Kila kukicha hotuba za Rais SSH kwenye mikutano na dhifa mbalimbali zinaakisi kauli yake Mimi ndiye Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kauli hiyo inatuma ujumbe mzito kwa wateule wake kwamba wasithubutu kumdharau kwa kwa sababu ya jinsi yake. Hoja yangu hii inathibitishwa na maagizo anayoyatoa wakati wa kuapishwa kwa wateule wake.

Kwa mfano, leo hotuba yake baada ya kuapishwa kwa Makatibu Tawala, ambao kimsingi ndio watendaji wakuu wa Serikali Kuu mikoani, ni ya maagizo na maonyo makali. Amewambia, bila kupepesa macho, baada ya kuwasimamisha mmoja mmoja na Wakuu wa Mikoa, kuwa atawapima kwa matokeo ya usimamizi wao katika masuala yote kijamii, kisiasa na kiuchumi.

Wateule wake, naamini wamemwelewa, wasisubiri vitanzi walivyofungwa shingoni vitumike kama vilivyokusudiwa. Tuwatakie kila la kheri.
 
Tanzania Mungu anaipenda nchi yake na watu wake pia. Make kutokea mbinguni aliona kwa mfumo wa uchaguzi ulivyo, jiwe hawawezi kumuondoa, make anauwezo wa kupenyeza kura feki akaongoza atakavyo.

Watanzania wangesema kwakuwa hawaridhishwi na tume ya uchaguzi wangesema labda waandamane, jiwe angewavunja miguu kama alivyokuwa akiahidi.

BAADA YA MUNGU KUONA ANALIOKOAJE TAIFA LAKE PENDWA NDO KAFANYA YALIYOFANYWA NA SASA TUKO AWAMU YA SITA NA KAZI IENDELEE!!!
THANK YOU JESUS!!
 
Mkuu Nyange tatizo ni letu WaTz ambao huwa tunafanya kazi kwa mazoea. Rais wa Awamu ya Tano kwa kutambua hilo alikuwa mkali kwa kutumbua wateule wake pasipo kupoteza muda wa kusubiri uchunguzi wa tuhuma.

Ikumbukwe kwamba wachunguzi ni binadamu ambao udhaifu wao huweza kuharibu uchunguzi kwa maslahi binafsi kama walivyo watuhumiwa. Tusubiri matokeo ya chunguzi ambazo zingine hadu sasa siku, wiki na miezi inakatika.
 
Binafsi nitafurahi endapo tu ripoti ya CAG ya mwakani itaonyesha hati safi kwahalmashauri zote.
hakuna wizi wala ubadhirifu wa fedha za umma.
 
Tanzania Mungu anaipenda nchi yake na watu wake pia. Make kutokea mbinguni aliona kwa mfumo wa uchaguzi ulivyo, jiwe hawawezi kumuondoa, make anauwezo wa kupenyeza kura feki akaongoza atakavyo.

Watanzania wangesema kwakuwa hawaridhishwi na tume ya uchaguzi wangesema labda waandamane, jiwe angewavunja miguu kama alivyokuwa akiahidi.

BAADA YA MUNGU KUONA ANALIOKOAJE TAIFA LAKE PENDWA NDO KAFANYA YALIYOFANYWA NA SASA TUKO AWAMU YA SITA NA KAZI IENDELEE!!!
THANK YOU JESUS!!
Umenena vyema.
 
Kila kukicha hotuba za Rais SSH kwenye mikutano na dhifa mbalimbali zinaakisi kauli yake Mimi ndiye Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kauli hiyo inatuma ujumbe mzito kwa wateule wake kwamba wasithubutu kumdharau kwa kwa sababu ya jinsi yake. Hoja yangu hii inathibitishwa na maagizo anayoyatoa wakati wa kuapishwa kwa wateule wake.

Kwa mfano, leo hotuba yake baada ya kuapishwa kwa Makatibu Tawala, ambao kimsingi ndio watendaji wakuu wa Serikali Kuu mikoani, ni ya maagizo na maonyo makali. Amewambia, bila kupepesa macho, baada ya kuwasimamisha mmoja mmoja na Wakuu wa Mikoa, kuwa atawapima kwa matokeo ya usimamizi wao katika masuala yote kijamii, kisiasa na kiuchumi.

Wateule wake, naamini wamemwelewa, wasisubiri vitanzi walivyofungwa shingoni vitumike kama vilivyokusudiwa. Tuwatakie kila la kheri.
Ila mimi binafsi hiyo kauli ya "Mimi ndiye Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania" sipendi aitumie mara kwa mara. Inaonesha kama haamini kama watu wanajua kuwa ni Rais! Akomae tu!!!
 
Back
Top Bottom