Shark
JF-Expert Member
- Jan 25, 2010
- 29,775
- 29,746
Kwema wakuu,
Niende moja kwa moja kwenye mada. Miezi ya hivi karibuni kuliibuka mtindo uliopachikwa jina la "Kuunga Mkono Juhudi" ambapo Viongozi mbalimbali waliokua upinzani walijiondoa na kujiunga na Chama tawala cha CCM.
Wengi wa hawa waunga mkono juhudi walitokea Chama cha CHADEMA, na mmojawapo ya sababu walizozitoa kwa wale wabunge ni kua wanalazimishwa kuchangia chama kutoka kwenye posho na stahiki zao za ubunge.
Viongozi wa CHADEMA walijitetea kua michango hiyo iko kikatiba, na matumizi yake yako kwenye taratibu za chama ambazo zinafahamika, na kua Waunga mkono juhudi hao wameamua kudanganya umma.
Sasa basi, sasa tuko kwenye kinyang'anyiro kingine, cha kuwapata Wabunge wa awamu ingine. Nina uhakika kabisa chama hiki kikapata wawakilishi wa awamu hii ingine inayokuja.
Ni vyema wawakilishi watarajiwa nyinyi mkaisoma Katiba ya chama inasemaje, pia msome na mjifunze taratibu za matumizi zikoje. Mtaonekana Wajinga sana kama sasa mnaomba kupitishwa na chama ambacho hamjui hata Katiba yake ikoje.
Mjue tu kua uungaji wenu Juhudi mkiwa mmechaguliwa mtaitia nchi hasara ya zaidi ya Billion 1 kwa kila Mbunge atakaeunga mkono Juhudi, fedha ambazo zingeweza kutumika kufanya mambo mengine ya Maendeleo.
Yangu ni hayo tu kwa ufupi kwa Weekend hii.
Niende moja kwa moja kwenye mada. Miezi ya hivi karibuni kuliibuka mtindo uliopachikwa jina la "Kuunga Mkono Juhudi" ambapo Viongozi mbalimbali waliokua upinzani walijiondoa na kujiunga na Chama tawala cha CCM.
Wengi wa hawa waunga mkono juhudi walitokea Chama cha CHADEMA, na mmojawapo ya sababu walizozitoa kwa wale wabunge ni kua wanalazimishwa kuchangia chama kutoka kwenye posho na stahiki zao za ubunge.
Viongozi wa CHADEMA walijitetea kua michango hiyo iko kikatiba, na matumizi yake yako kwenye taratibu za chama ambazo zinafahamika, na kua Waunga mkono juhudi hao wameamua kudanganya umma.
Sasa basi, sasa tuko kwenye kinyang'anyiro kingine, cha kuwapata Wabunge wa awamu ingine. Nina uhakika kabisa chama hiki kikapata wawakilishi wa awamu hii ingine inayokuja.
Ni vyema wawakilishi watarajiwa nyinyi mkaisoma Katiba ya chama inasemaje, pia msome na mjifunze taratibu za matumizi zikoje. Mtaonekana Wajinga sana kama sasa mnaomba kupitishwa na chama ambacho hamjui hata Katiba yake ikoje.
Mjue tu kua uungaji wenu Juhudi mkiwa mmechaguliwa mtaitia nchi hasara ya zaidi ya Billion 1 kwa kila Mbunge atakaeunga mkono Juhudi, fedha ambazo zingeweza kutumika kufanya mambo mengine ya Maendeleo.
Yangu ni hayo tu kwa ufupi kwa Weekend hii.