Watoto wa kishua hamuwezi kuielewa hii picha

Nimeng’oa kucha kisa mpira, nilishawai kumpasua jamaa uso kisa mpira. Niliponea kufukuzwa shule baada ya hapo mzee akanipiga marufuku kucheza mpira, sekondari nikawa shabiki tu.
 
Huo mpira usiombe ukaloana unakua ka jiwe
 
Nimeng’oa kucha kisa mpira, nilishawai kumpasua jamaa uso kisa mpira. Niliponea kufukuzwa shule baada ya hapo mzee akanipiga marufuku kucheza mpira, sekondari nikawa shabiki tu.
wazee wengi sana walikua hawataki wanao tucheze mpira....lkn leo wanapiga kelele " oooh kichuya noma nomaaa"" sasa sijui wanadhani kazaliwa anajua!!??
 
Duuu
 
Nimeng’oa kucha kisa mpira, nilishawai kumpasua jamaa uso kisa mpira. Niliponea kufukuzwa shule baada ya hapo mzee akanipiga marufuku kucheza mpira, sekondari nikawa shabiki tu.
Mkuu mi nakumbuka nilifungwa pop aka muogo mpira tu huo vidole viliteguka nikajificha kimya nimerudi jioni jua limezama sijaoga wacha nipigwe na chelewa miguuni na Bro namwambia nimeumia hasikii asubuhi wacha Mama anione mguu umevimba alikimbia hospital kanibeba na mbeleko hadi magari aliona yanamchelewesha dah nikikumbukaga Rip mum[emoji22] nimedeka sana enzi zangu.
 
huu mpira ulikua hauna wakukaa nje labda kama ni mtu mmoja yan mkiwa wawili tu kila mtu anachagua kwa kufunga ngoma inaendelea hata muwe 30 ilikua poa tu tulikua tunaita 'nyanka'
 
Mi nilikuwa nikija na mpira wenyewe tukiita "sembo" lazima nicheze mwanzo mwisho, nikitolewa tu natambaa na mpira wangu mechi inaisha!
Sie tulikuwa tunaita Sambi na ukipiga doso (yaani kwa dole gumba) mwenye mpira anakutoa maana unasababisha mpira kufumuka
 
huu mpira ulikua hauna wakukaa nje labda kama ni mtu mmoja yan mkiwa wawili tu kila mtu anachagua kwa kufunga ngoma inaendelea hata muwe 30 ilikua poa tu tulikua tunaita 'nyanka'
Na ulikuwa hauna refa lakini bado wachezaji waliheshimiana na kukubaliana kwamba hiyo ni faulo...pia mpira ulikuwa hauna mwisho yaani utachezwa dakika kadhaa, mpira unaisha mpaka mwenye mpira aamue au wacezaji mmoja mmoja wanaitwa wakaoge ama wakafanye shughuli za kuwasaidia wazazi
 
tulikua tunaita tobodunda
kitambo sana i miss those days
kuna majamaa yalikua yanakaa karib na mti yenyee hayachez kaz yao ni kukuzuia usishike mti mpk ule kichapo kwanza

noma sana
Nimecheka sana aisee afu huaga majamaa yanakudunda kweli hadi unatapika udaga!
 
ooh mkuu basi nyie mmekuja juzi...kizazi chetu sisi ilikua ni kondomu tu....yani ilikua noma sana hyo
Kondomu inapulizwa kama puto afu juu mnaweka masponji ya godoro mnafuma kwa nyuzi badae mnashonea vitambaa tofauti tofauti kama gozi vile
 
noma sana enzi izo nakumbuka tulikua tunachezea sana mpira wa karatasi (nyanka) kuna dogo mmoja wa kishua akaja na mpira wa gozi mzee ...tukatamania kichiz sema dogo anabania ...bei ulikua unauzwa 1300 tukasema kama vipi tujichange tulichanga kama wiki mbili ivi ikatosha hel ya kununulia gozi na bahat nzuri skuio ilikua ni jumapili kwenye gulio huwa wanapunguza bei ...

basi mzee tukanunua mpira ule tukamkabidhi daudi msenjelwa kwakua tulienda jioni zaid (mana jion zaidi ndo bei inapungua zaidi)
ikabidi mpira tumuachie daudi tutacheza kesho tukirudi shule

jumatatu shule kamakawa darasani muda auendi tunawaza kurudi tukachezee (tukapute) gozi

mda wa kurudi umefika ile kufika kwa kina daudi tunaona anatia huruma tu kumbe shule hajaenda ameshinda anachezea gozi tu mpaka akalipasua kwenye msumali wa paa la nyumba

tulimmaindi kichizi yan mpira umeharibika hatujaugusa hata kidogo hadi leo nikimkumbusha huwa tunaishia kucheka tu
 
[emoji23][emoji23][emoji23]daudi noma
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…