KERO Watoto wa mitaani wanaoishi chini ya daraja la Ubungo(Kijazi interchange) wamekuwa tatizo sana

KERO Watoto wa mitaani wanaoishi chini ya daraja la Ubungo(Kijazi interchange) wamekuwa tatizo sana

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

NBica

Member
Joined
Sep 13, 2010
Posts
39
Reaction score
36
Je, serikali imeshindwa kabisa kuwaondoa na kuwadhibiti watoto hawa wa mitaani wanaolala chini ya daraja la Ubungo(Kijazi interchange) na ambao wamekuwa wakifanya kazi ya kusafisha vioo vya magari?

Sasa hivi wamejijengea tabia ya ajabu kabisa ya kutaka kusafisha kwa nguvu vioo vya magari, sasa ukiwazua, subiri taa zikiruhusu ndio utaelewa. Wamekuwa wakigonga vioo na kumwagia maji yao machafu ndani ya gari

Juzi kati walipishana na dereva wa daladala katika hatua hiyo hiyo ya kulazimisha vitu, Taa iliporuhusu walikuwa wameshajikusanya walivamia daladala na kuanza kuligonga huku wakimwaga maji yao yale ya kuoshea ndani ya daladala.

Nimeshuhudia tena katika gari binafsi, ameanza kusafisha kioo dereva akamzuia, Gari zinaruhusiwa tu, walianza kulipiga gari na kugonga vioo na walijikusanya sijui hata walipotokea.

Sasa hali hii imekuwa kero ukifika ubungo mataa muda wote unakaa kwa wasiwasi. Tabia hii ikikomaa itakuwa hatari zaidi wadhibitiwe mapema
 
Makonda alianzisha kampeni ya kudhibiti wazazi wanaokimbia majukumu yao kwenye familia ili kudhibiti watoto wa mtaani, naona ile kampeni imeyeyuka, watoto wa mtaani wanatoka kwenye familia zinazokosa matunzo au uangalizi mbovu pengine kutoweka kwa wazazi kutokana na vifo au kifungo jela.

Ikiwa serikali ni ya wananchi wote hata watoto pia ni wananchi na ndy kitovu cha nchi, wakikosa uangalizi basi taifa liko mbioni kupotea.

Ninachotamani kusema ni kwamba vipi ikiwa ndani ya kila kata au kitongoji kuwe na mfumo wa kuhakikisha watoto yatima na wale wasio na malezi mazuri kwa wazazi wao wakusanywe na kuwekwa sehemu salama kwa ajili ya uangalizi malezi na hata kusomeshwa kwa gharama za serikali.
 
Back
Top Bottom