Watoto wa Mjini Dar


Ndama ana tamaa sana, alimzima mshikaji wangu discman long time, enzi hiyo brotherkaka yake mshkaji wangu karudi kutoka Greece / Italy (watu walikuwa hawajazibukia States bado) basi akamtupia discman acheze CD.Enzi hiyo discman is a novelty, basi Ndama akaomba asikilize, akatoweka nayo, kuanzia hapo story kibao, mpaka mshkaji akamtia kituoni polisi makuti pale.

Schadenfreude is never my style but frankly I am surprised it took this long for Ndama, his azz shoulda been in jail a long time ago, mazishi mkubwa.

Ndama Shaaban ana tamaa sana na wala sishangai kusikia hizi habari.
 

Watu wengi nadhani sio Ndama peke yake walikuwa wasanii wasanii kipindi cha nyuma kidogo wakati bado ndio wanaanza anza maisha,mimi na mjua Ndama personal na hata huyo Kizai zai nimesha fanyanao biashara.Labda kubadilika kumekuja baada ya kupata vijisent baadae akaja kuwa bonge la msaada kwa wale walio kwenye msoto kwa kuwarushia kamba si unajua kimjini mjini.
Lakini inastajabisha watu wanaweza kufanya mambo gani wakijaribu kuweka status isipotee,hii cha mtoto hao jamaa wanuozo mwingi zaidi
 
Lakini imeboa pale watu wanapoanza kurusha kashfa za rejareja tena wengine ni watu niliodhani ni wa kuheshimika kabisa hapa JF..ndo maana nikasema..

Mkuu Mtindio,

Chill bro, hapa tunapunguza stress tu za EPA bros, sometimes tunahitaji hii yaani entertainment, chill out mkuu!
 
Hivi "big deal" ya kuzaliwa mjini as opposed to kuzaliwa mikoani/ vijijini ni ipi? Are those born in the city (Dar) better than those born in other places?
 
Wakulu naona mnataja mitaa yote ya Dar..kuna yeyote mwenyeji wa mitaa ya gerezani??? Yaani naongelea block loote tokea mtaa wa msimbazi hadi mitaa ya co-cabs?? nani hajatengenezewa gari yake Gerezani?? Ile ni DETROIT ya dar...kifaa gani cha gari ukikose pale??
Wakati huo ukienda shule kuna malolabugi bwana...lazima wakujue wewe ni mtoto wa mzee fulani otherwise wanaweza kukuchukulia madaftari hasa kipindi cha mwanzoni mwa muhula....
Kali kuliko yote unapigwa makonzi ukimshangaa msela akila msuba...
 
PUNDIT,naomba msaada hapa kumbukumbu zangu kidogo zinakataa kuclick,ule msikiti wa mindu/united nations angalau upo kwenye hood yangu,sikumbuki vizuri kama zama hizo ulikuwepo,cause it seems like i remember seeing it go up,thanks in advance kwa jibu
 

GEREZANI,tulikuwa twaenda cheza tombola,alaafu wazee wetu wakiibiwa vioo vya magari,tunakwenda kuvikuta gerezani,hapo mdingi hata aje na bunduki,atake,asitake kioo chake mwenyewe anauziwa
 
GEREZANI,tulikuwa twaenda cheza tombola,alaafu wazee wetu wakiibiwa vioo vya magari,tunakwenda kuvikuta gerezani,hapo mdingi hata aje na bunduki,atake,asitake kioo chake mwenyewe anauziwa

Sana tu mi mzee alishawahi kuuziwa site mirror ya kwake mwenyewe, si unajua ile unaziandika namba ya gari....Aaaah walimuuzia!!
 
mwazange,lakini asili ya hili jina la gerezani lilitoka wapi?kulikuwa na gereza nini? mazee unaikumbuka railway crossing ya pale TAZARA hapa palikuwa machinjioni mtu kibao zimekumbwa na train hapa. kwenye sagula sagula ulikuwa unajichanganya?au wewe mwenzetu matawi ya juu
 

Aah wapi mkuu mimi sikuwa wale wa mitaa ya juu, mimi nilikuwa wa kawaida tu, nimekwenda sana kwenye mabehewa ya kutoka bara kukusanya mbolea kwa ajili ya skonga...
Nilishawahi kuuliza kuhusu asilia ya jina hilo lakini sikupatiwa jibu la kueleweka...Mkuu umehudhuria shule mitaa ya hapo nini....nianze kukumbuka mie.
Crossing ipi hiyo unayoizungumzia? Ya kule kwa Pugu Road au ya shaurimoyo mkuu...?
 

Nilijaribu kutafuta source ya hili jina lakini nakuta hata enzi za Wajerumani back in 1905 hili eneo lilikuwa linaitwa Gerezani.

Katika kitabu cha historia ya Dar-es-salaam cha James R. Brennan na Andrew Burton "Dar es Salaam Histories from an Emerging African Metropolis" wamesema

 
Kuna mtu kamuongelea NDAMA sasa na mimi nimekumbuka watu wengine

Hivi kuna mtu anaweza kuniambia kama TALL keshajenga nyumba maana dalali yule alikuwa akiishi kwenye gesti Haus za migo migo


Hivi ile hoteli ya wakuja ya KIBODYA bado ipo maana ile watu woote from country side esp wanaotoka KIGOMA LAADHI ndio destination yao wakija Dar


Hivi kuna mtu anajua DARWESH swahiba yake ndama aliishia wapi?


Jamani hivi MUDI MAS aka MUDI MWARABU aka TAJIRI MTOTO bado anaendelea kuuza chupi pale mtaa wa kisutu ?


Jamani MAO FLEX naye alipotelea wapi? (mara ya mwisho nilisikia alirudi kwenye fani yake ya zamani ya kusafisha ma kapeti kule mississippi) sijui ndio anazushiwa au sijui vipi

na zaidi ya hayo nani anajua ukweli kuhusu kifo cha yule mtoto wa Temeke HAMZA? maana tunaambiwa alijipiga risasi wengine wanadai alijui ukweli ni upi


Jamani kama kuna mtu anazo taarifa za MWAKITWANGE mpeni salaaam mwambieni asijifiche sana mjini


Of course tutamsahau vipi Brother Khery wa SALAMANDER? Maana pale magazines zote za dunia nzima unazipata na hata Ben na Mkewe walikuwa wanafunga on Sundays pale wananunua FT WEEK-END




Na zaidi ya yote hayo nauliza hivi? Hivi UGWENO GUEST HOUSE na EXANADU GUEST HOUSE bado zipo au?


la micho mwicho mwisho zaidi

Hivi nani kati yenu bado anaenda kupiga simu za Internatinal za kimitikasi pale MUHIMBILI?

nawasilisha
 

Mkulu GT wewe kweli wakitambo.
Hao jamaa uanwauliza kweli ni watoto wa mji kweli kweli.

Nitakujibu wachache ambao ninewaona Khery Magazines alikuwapo kama miaka miwili ya nyuma(sina uhakika sana na muda) nilimwona alafu kama huna habari SALAMANDER pamevunjwa mwezi huu wa 11.alafu hapo nyuma kulikua na watu wanakuwepo kuwepo pale kwenye ile meza ukimuulizia jamaa wanakuambia katoka.siku hizi yale magazines unauziwa kwenye Trafic lights kwahiyo sio sana kwenda samora.

Mwandewazimu MUDI MAS nilikutana nae China mwaka jana kaweka nywele zake rangi alikua na Manganja ,pamoja na KIboko.
Jamaa anaongea kama katiwa Funguo,"anadai yeye utajiri kwao kaukuta,kuliko vitoto vinavyo jua safari siku hizi )
 
nani,anakumbuka wahujumu uchumi wanaingiliwa makwao wanasearchiwa na kutupwa gerezani?kuliko kukutwa na ushahidi ndani,vitu wanatupa barabarani.sisi dogo tunazurura kutafuta vitu vilivyotupwa.pale maeneo ya boy scouts,upanga sisi tuliokota kama raba mtoni 30 sema vyote vya kushoto huyu muhujumu alikuwa na roho mbaya,sijui vya mguu wa kulia alivitupa wapi? some people!!!!!!!!!
 
na zaidi ya hayo nani anajua ukweli kuhusu kifo cha yule mtoto wa Temeke HAMZA? maana tunaambiwa alijipiga risasi wengine wanadai alijui ukweli ni upi

GT,

Hamza huyu yupi? Yule aliyekuwa anakaa kurasini hapa bendera tatu kwenye nyumba za BP? Mshua wake alikuwa BP na step-mom British Airways? Brotherman player type? alitesa sana Majira mpaka wazee wakaona anakufuru? Au mwingine?
 
GT,

Hamza huyu yupi? Yule aliyekuwa anakaa kurasini hapa bendera tatu kwenye nyumba za BP? Mshua wake alikuwa BP na step-mom British Airways? Brotherman player type? alitesa sana Majira mpaka wazee wakaona anakufuru? Au mwingine?

Ebwana yule HAMZA mshua wake alikuwa kigogo fulani zamani lakini aliishi sana UK alikuwa ni BONGE la mtu. Infact naye ndio katika watoto wa TEMEKE aka MKOA WA PWANI maana sie watu wa Kinondoni Temeke tunakita MKOA WA PWANI...kume kaa kushoto kushoto sana lakini ndio WILAYA (enzi hizo) uliotoa mabaharia wengi

Huyu Hamza alikuwa na Ofisi pale nyuma ya Bilicanas...sasa hivi zimevunjwa na ofisi yake ilikuwa kabla hujafika ofisi ya MAKUNDI


By the way hivi kuna mtu anajua what Mr MAKUNDI is up to? mara ya mwisho niliambiwa kama Contractor sijui kweli au la


anyway back to HAMZA alikuwa swahiba mkubwa sana wa DARWESHI sijui naye yuko wapi

by the way kuna mtu anajua ALIPO yule mtoto wa Mgomeni Mr SLIM au mwenyewe alikuwa anajiita CHEKIBOBU MAARIFA..alikuwa ana PONY TAIL...mara ya mwisho nilimwona OSLO lakini sijui sasa hivi yuko wapi lakini wazee wa MELI mtakuwa mnamjua huyu. Huyu naye ni mtoto wa KARIAKOO kuleee chini jina sijui ni mtaa gani lakini nyumba yao ilikuwa si mbali sana na kwa akina AMANI MASHA aliyekuwa anachezea (Simba) enzi hizo

By the way huyu Slim alipanda pipa 1978 tena meli yao iliitokea UGIRIKI kwenda kuchukua Ndizi Venezuela na kuna watu walikutana na SLIM meli ilipotia nanga San Francisco na watakuaon=mbia enzi hizo tTHE COMMODORES walikuwa ni akina nani
 


Ebwana unajua upande wa pili pale SALAMANDER kulikuwa kunauzwa JUISI na jamaa mmoja anaitwa LUGANO.... na oppositepale (mtaa wa Mkwepu) kulikuwa na Travel Agency ya wazungu wote wanaokwenda shamba...al maarufu kama NGAZI TANO


Ebwana Kheri alikuwepo na nadhani Maggid Mjengwa alipiga picha naye akaweka kwenye blog...ngoja niitafute kisha ntakuwekea hapa

Basi pale MWAKITWANGE yeyey alikuwa nasoma magazeti bila kulipa kitu. Na enzi hizo MSOFE alikuwa anaitwa Msofe na sio PAPAA MUSOFE...noma tupu

Ebwana hivi kuna mtu anajua CARL LEWIS alipoelea wapi huko NEW YORK?

na kabla sijaanza nani tati yenu kala kwenye CANTEEN ya Ujenzi kule opposite na Motel Agip?

Au kama misosi kule New Africa Hotel...si unajua tena kama ulikuwa unajuana na Meneja basi ahhhh mchana wee unaingiza timu na unapata msosi sawa na investor ...


Jamani akina YU-YU mnajua waliishia wapi?


kwa sasa naishia hapa maana naona nitakuwa ninawa overwhelm


cha ajabu kimya cha MWANAKJIJI kwenye hii thread kinatuthibitishia kuwa hata Dar atakuwa hakuishi

lakini poa tu vile vile
 
GAME THEORY,nimekubali,kila baharia,kila mtoto wa mjini unamjua wewe!!!! sasa hiyo shule ulisoma saa ngapi? je hao mabaharia wakirudi fresh,walikuwa wanakususia vitu vikubwa mwenzetu,lazima ulikuwa pina.nashukuru sana humu JF tuna watoto wa mjini,heshima zako mkuu,mimi napandisha white flag
 

Namsuribi ES kwa hamu na mabaharia wenzie najua takuwa anawajua hawa

kuna kusoma basi? sie tukisoma shule hao akina Rev Kishoka watafanya nini?

sie wengine shule ilitushinda...ndio maana tunazuga tuu humu kwenye ma internet

Ebwana is so true jamaa walikuwa wakirirudi i was always fascinated na magari na pamba zao

kama zihi




kama hiyo haitoshi..nakumbuka MIGURUWE KAMA HII NDIO ILIKUWA YENYEWE...NAKUMBUKA 1988 baharia malima aliporudi toka BURUDA basi alikuwa na guruwe kama hili








halafu lilikuwa limepigwa ma sticker kibao ya Regae na Bob Marrley basi mjioomba huo mziki ndani ya Gari ulikuwa ni second to nona....maana mle ilikuwa ni BOBA MARLEY tena album zilikuwa ni mbili tuu zina pigwa kama si hii



basi ilikuwa ni hii




Sasa hapo mwanangu likipigwa lile NATURAL MYSTIC basi aaahhhh wee acha tuuu na enzi hizo bara bara zilikuwa mbovu ile kichizi.....

na nakumbuka COASTER aliporudi mwaka uliofuata basi kwenye chati alikuwpo huyu bibie





kwa hiyo mwanangu maneno yalikuwa ni BUFFALO STANCE

halafu tunakuja humu unakutaka na watoto wadogo waliosoma tution kwa MWALIMU NDOSI na wenyewe wanaanza kukukoromea. Lakini ndio hivyo tena mamabo ya kukaa kijiweni na wajinga wajinga

anyway naona box langu limegoma na mimi nataka nicheki game ya MAn City ntarudi baadae kidogo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…