Watoto wa vigogo waongoza kuchakachua ripoti vyuo vikuu

Watoto wa vigogo waongoza kuchakachua ripoti vyuo vikuu

kilimasera

JF-Expert Member
Joined
Dec 2, 2009
Posts
3,068
Reaction score
277
SUALA la uchakachuaji mitihani limeingia katika sura mpya baada ya kuibuka kampuni zinazoendesha biashara ya kuwaandikia ripoti za utafiti, wanafunzi wanaohitimu elimu ya juu katika vyuo vikuu.

Uchunguzi wa Mwananchi Jumapili umebaini kuwa kampuni hizo hutengeneza kazi hizo, ambazo baadaye huziandika ili zionekane zimefanywa na mwanafunzi husika baada ya kukamilisha malipo.

Wanafunzi hao ni wale wanaomaliza elimu ya juu katika vyuo vikuu mbalimbali nchini katika ngazi ya shahada, shahada ya uzamili na shahada ya uzamivu (PhD).

Wanafunzi wengi kabla ya kukamilisha mafunzo katika ngazi husika kwa kawaida hutakiwa kufanya utafiti na baadaye kuandika ripoti kuhusu taaluma aliyosomea, lakini kwa kuona ugumu wa kazi hiyo, wenye uwezo hutumia kampuni hizo ili kufanyiwa kazi hiyo tena kwa ustadi wa hali ya juu.

Uchunguzi unaonyesha kuwa wanafunzi wenye tabia hiyo wengi wao ni watoto wa vigogo ambao hutumia ipasavyo uwezo wa kifedha wa wazazi au baadhi ya wale wanaosoma huku wakiwa kazini.

Wanafunzi hao inaelezwa hutoa kati ya Sh2 milioni hadi saba ili kupata taarifa za tafiti wanazozihitaji zikiwa tayari zimetengenezwa katika mfumo wa kitabu.

Baadhi ya wahadhiri wa vyuo vikuu mbalimbali nchini wamekiri kuwapo kwa vitendo hivyo wakieleza kuwa walivibaini baada ya kuwauliza maswali wanafunzi kuhusu tafiti walizoziwasilisha, lakini wakashindwa kujitetea.

"Mmoja aliandika tafiti nzuri. Nikawa na wasiwasi.
 
Hili ni tatizo kubwa na sio tu kwa watoto wa vigogo hata wengine wanatumia miili yao kama rushwa kuandikiwa riport tabu inakuja pale wanapoambiwa wafanye presentation.unakuta hata mtu hajui eneo alilifanyia hiyop research.
 
hahaaaaaa kweli nchi sasa inaandaa vilaza kwanini watu wasijitume tu hv kwa mtindo huu tutaendelea kweli
Hili ni tatizo kubwa na sio tu kwa watoto wa vigogo hata wengine wanatumia miili yao kama rushwa kuandikiwa riport tabu inakuja pale wanapoambiwa wafanye presentation.unakuta hata mtu hajui eneo alilifanyia hiyop research.
 
Hili ni tatizo kubwa na sio tu kwa watoto wa vigogo hata wengine wanatumia miili yao kama rushwa kuandikiwa riport tabu inakuja pale wanapoambiwa wafanye presentation.unakuta hata mtu hajui eneo alilifanyia hiyop research.

nakubaliana na wewe tena maswali katika presentation mengi yanataka ku prove kama hiyo research umeifanya wewe mwenyewe au vinginevyo (HASA RESEARCH ZA UNDERGRADUATE), ila wanavyochemka aibu... ukitaka kuwagundua mapema fanya uchunguzi karibu na siku ya presentatation utakuta mtu anakomaa kuisoma repoti utafikiri ni desa!!! kumbe hajui kilichomo kwenye hiyo repoti

SHAME ON THEM...
 
Tuanze kwa kuwataja kwanza watoto wa vigogo alafu tuenddlee kuchangia.....................hivi wale wa bot waliishia wapi?
 
Kama hali ndo hii basi tumekwisha! unategemea mtu kama huyu anaweza kuwa critical kwa jambo linalohusu maendeleo ya nchi yake? sidhani kwani huyu atakuwa mstari wa mbele kujilimbikizia mali na kuiacha Tanzania ikiwayawaya. kweli tumekwisha, ukombozi haupo hata kidogo!
 
Nadhani Si lazima wawe watoto wa vigogo tu wote wanaofanya hivyo ni sawa tu-VIHIYO++++++
 
...for a great thinker THIS IS AN OPPORTUNITY! if we have too many fools at mid-levels, then the smart few will ultimately PROSPER. Just a matter of staying awake. Usijali sana ukimwona kobe juu ya mti, jipange.
 
Hili ni tatizo kubwa na sio tu kwa watoto wa vigogo hata wengine wanatumia miili yao kama rushwa kuandikiwa riport tabu inakuja pale wanapoambiwa wafanye presentation.unakuta hata mtu hajui eneo alilifanyia hiyop research.

Nasikia IFM wanaongoza
 
yalimalizwa kimyakimya ila mpaka sasa bado wanabebana pale nadhani hali hii itakwisha labda mpaka chama cha upinzani kichukue madaraka!wewe huoni tu hali ilivyo sasa hv kila sehemu CCM wanachakachua kisa watoto wao ndio warithi nafasi hizo!wakati utafika tu hata kama itachukua muda mbona kenya waliweza na maka sasa haoo wanapiga bao!
Tuanze kwa kuwataja kwanza watoto wa vigogo alafu tuenddlee kuchangia.....................hivi wale wa bot waliishia wapi?
 
kama mtu kuanzia anaanza 1st yr amezoea kumeza unategemea mwisho afanye nini ili apete gamba? ARDHI kidogo wanjitahidi maana wao kuanzia semister ya kwanza hadi ya mwisho wana project hii inawasaidia wakati wa dissertation
 
Back
Top Bottom