chakubimbi
Member
- Nov 25, 2010
- 21
- 1
Watoto wengi wa wanasiasa na baadhi ya wakubwa wa nchi wamekua wakipewa mikopo na bodi ya mikopo ya elimu ya juu wakati hawana sifa za kupata mikopo hiyo. Wengi wa watoto hao huwa wanapewa scholarship nje ya nchi kupitia wizara ya elimu na wengine huwafata wazazi wao ambao ni mabalozi nje.
Mfano wa nchi ambazo hao watoto wa wanasiasa na wakubwa wengine wa nchi wamejazana ni Algeria, China, Cuba, Poland Urusi n.k wakiwa hawana sifa kwani wengi wao ni kidato cha nne au kidato cha sita waliofeli vibaya mno. Wakifika katika hizo nchi hupewa mikopo 100% ambazo ni mamilioni ya pesa za kitanzania.
Wengi wao wanapewa mikopo kwa wazazi wao kuwashinikiza watendaji wa bodi wawape mikopo watoto wao, Hii sio haki hata kidogo kwani watoto wa wakulima wanateseka bila kupata mikopo lakini watoto wa hawa wanasiasa wanapeta tu.
TANZANIA NI NCHI YETU SOTE .
Mfano wa nchi ambazo hao watoto wa wanasiasa na wakubwa wengine wa nchi wamejazana ni Algeria, China, Cuba, Poland Urusi n.k wakiwa hawana sifa kwani wengi wao ni kidato cha nne au kidato cha sita waliofeli vibaya mno. Wakifika katika hizo nchi hupewa mikopo 100% ambazo ni mamilioni ya pesa za kitanzania.
Wengi wao wanapewa mikopo kwa wazazi wao kuwashinikiza watendaji wa bodi wawape mikopo watoto wao, Hii sio haki hata kidogo kwani watoto wa wakulima wanateseka bila kupata mikopo lakini watoto wa hawa wanasiasa wanapeta tu.
TANZANIA NI NCHI YETU SOTE .