Wana JF kuna jambo ambalo linamtatiza jamaa yangu ambalo amekuwa akifikiri kwa muda mrefu bila ya kupata ufumbuzi, yeye amejaliwa kuwa na mke na watoto watano, lakini kati ya hao watoto watatu ni "true copy" ya sura, tabia, rangi na hata kutembea yao, lakini wale wawili hawafanani na wenzao hawako kwa mkewe wala kwake katika kufanana anaomba ushauri wenu inawezekana amefanyiwa uchakachuaji au ni hali halisi?