KERO Watoza ushuru wa maegesho ya magari Manispaa ya Morogoro wanatoza ushuru kinyume na utaratibu

KERO Watoza ushuru wa maegesho ya magari Manispaa ya Morogoro wanatoza ushuru kinyume na utaratibu

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

TAWA

JF-Expert Member
Joined
Jun 23, 2013
Posts
3,674
Reaction score
1,572
Naripoti kutoka Morogoro manispaa:

Kumekuwa na changamoto kwa wakazi wa manispaa ya Morogoro kutozwa ushuru wa maegesho ya magari na watu wa halmashauri ya Manispaa ya Morogoro kinyume na utaratibu.

Ukiegesha gari bila kujali katika maegesho rasmi ya Manispaa au popote pale anakuja mtu wa Manispaa na mashine na kuipiga picha gari na kukuandikia deni bila kukupa control number ya kulipia au kukueleza chochote kuhusiana na malipo hayo. Utakuja kuuona malipo siku ukija kusimamishwa na kukaguliwa madeni ndipo utaona kuwa Una madeni mengi ya ushuru wa maegesho.

Kilicho kibaya zaidi, watu hawa wanachaji maegesho mpaka kwenye nyumba za watu au sehemu za kutolea huduma binafsi kama vile kwenye migahawa, bar au hospital japo watoa huduma hizo wameweka maegesho kwa ajili ya wateja wao.

Soma Pia: Ushuru wa maegesho umegeuka kuwa wizi usiotumia mabavu wa serikali dhidi wananchi wake

Nadhani huu ni utapeli unaopaswa kupigwa vita kwani kuwa na gari siyo laana katika taifa hili.

Ushauri wangu kwa Mkurugenzi, atengeneze maegesho rasmi ya magari mfano Ile stendi ya zamani pale mjini Kati, soko kuu la Kingalu stendi ya Msamvu na maeneo yanayofanana na hayo. Hapo ni halali kwake kuchaji ushuru wa maegesho na siyo kwenye majumba ya watu.
 
Kama hoja yako ni kuboreshwa kwa parking ni vyema ungeenda straight na kupendekeza hivyo.hakuna haja ya kudanganya eti Mtu ni tapeli.
 
Kama hoja yako ni kuboreshwa kwa parking ni vyema ungeenda straight na kupendekeza hivyo.hakuna haja ya kudanganya eti Mtu ni tapeli.
Nadhani hujanielewa na hutaki kuelewa. Morogoro kwa sasa ukipaki gari yako hata nje ya nyumba yako itadaiwa ushuru wa maegesho. Sasa huo siyo utapeli!?
 
Nadhani hujanielewa na hutaki kuelewa. Morogoro kwa sasa ukipaki gari yako hata nje ya nyumba yako itadaiwa ushuru wa maegesho. Sasa huo siyo utapeli!?
Nje ya nyumba ya mtu kama kuna barabara inakuwa ni mali ya umma. Ukipaki gari ndani ya kiwanja chako hulipii, ila kwenye eneo la umma pembeni ya barabara ni sawa halmashauri ikiweka utaratibu wa malipo.
Hata Kariakoo watu wanalipia parking pembeni ya barabara zilizo nje ya nyumba na maduka yao.
 
Nje ya nyumba ya mtu kama kuna barabara inakuwa ni mali ya umma. Ukipaki gari ndani ya kiwanja chako hulipii, ila kwenye eneo la umma pembeni ya barabara ni sawa halmashauri ikiweka utaratibu wa malipo.
Hata Kariakoo watu wanalipia parking pembeni ya barabara zilizo nje ya nyumba na maduka yao.
Tunachobishania hapa, wewe unaongea nadharia na kutetea usichokijua Mimi nakwambia uhalisia na kitu ambacho kinafanyika. Hapo ndiyo kwenye shida
 
Maisha ya mtanzania, umeamua kujenga kakibanda kako kwenye kiwanja cha urithi hujakaa sawa unakutana na lialama X kibali. Unawasha kacorolla kako kwenda kufuatilia ili uwahi kurudi kibaruani unapaki kutoa elfu tano ya mafuta uliyosongesha ukirudi unakuta cheni ya wakusanya ushuru wa parking, unataka kupiga simu uombe msaada inaingiliwa na simu ya mwenye nyumba inaita ukatoe vitu kapata mpangaji mpya.
 
Back
Top Bottom