Watu 13 wafariki dunia kwa kuanguka kisimani wakiwa harusini

Watu 13 wafariki dunia kwa kuanguka kisimani wakiwa harusini

John Haramba

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2022
Posts
365
Reaction score
1,374
Watu 13 akiwemo mtoto mmoja wamefariki dunia baada ya kuangukia ndani ya kisima wakati wa sherehe ya harusi Kaskazini mwa India, juzi Februari 16, 2022.

Waliopoteza maisha asilimia kubwa ni wanawake na mtoto huyo ambapo walikuwa wamekaa juu ya kisima kilichokuwa kimezibwa kwa muda.

Taarifa ya Polisi wa Jimbo la Kushinagar ambapo ndipo tukio lilipotokea wamekiri kutokea kwa maafa hayo huku mmoja akijeruhiwa.

"Tukio hili limetokea wakati wa sherehe za ndoa, upelelezi unaendelea,” amesema Polisi wa Kushinagar, Sachindra Patel.

Waziri Mkuu wa India, Narendra Modi amelitaja tukio hilo kuwa ‘linaloumiza moyo’.

Waziri Modi ametangaza kutoa fidia ya dola 2,662 kwa kila familia iliyokumbwa na majanga hayo, pia dola 665 kwa kila familia ambayo imepata majeruhi katika tukio hilo.

Mamlaka ya Wilaya ya Kushnigar nayo imeongeza kwa kutoa dola 5,323 kwa kila familia iliyoathirika na tukio hilo.

India-thumbnail.jpg
 
Wa hindi wanashida kubwa ya ma eneo ya kufanyia sherehe kwasabb ya wingi wa watu wao na umasikini ulio kithiri, wakikosa chakula cha harusi huenda wa sile vizuri paka harusi nyingine bora Tanzania yetu
 
Wa hindi wanashida kubwa ya ma eneo ya kufanyia sherehe kwasabb ya wingi wa watu wao na umasikini ulio kithiri, wakikosa chakula cha harusi huenda wa sile vizuri paka harusi nyingine bora Tanzania yetu

Hao akina dewji na wahindi wenzie washukuru sana wako Tanzania. Ila wahindi bwana wengi wana dharau na ubinafc/ubaguzi,,,,Wawaige waarabu tunaishinao vizuri na wamechanganyikana na wabongo, hawana midharau.
 
Back
Top Bottom