Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,108
- 10,191
Watu 15 wamefariki na wengine 24 wamelazwa hospitali wakiendelea kupata matibabu kutokana na virusi vya ugonjwa wa Corona Zanzibar.
Hayo yamebainishwa na Waziri wa Afya wa Zanzibar Mhe Nassor Ahmed Mazrui wakati akitoa takwimu za ugonjwa wa Corona kuanzia Juni 25 hadi Agosti 10.
Waziri Mazrui amesema jumla ya watu 29,326 wamepimwa virusi vya Corona na 390 wamekutwa na virusi hivyo huku wageni wakiwa ndio wengi 278.
Akizungumzia chanjo ya Corona Mhe Mazrui amesema Zanzibar ina chanjo za aina mbili Sinovac ya china na Sputnik light 5 na chanjo hizo zimeanza kwa makundi.
Hayo yamebainishwa na Waziri wa Afya wa Zanzibar Mhe Nassor Ahmed Mazrui wakati akitoa takwimu za ugonjwa wa Corona kuanzia Juni 25 hadi Agosti 10.
Waziri Mazrui amesema jumla ya watu 29,326 wamepimwa virusi vya Corona na 390 wamekutwa na virusi hivyo huku wageni wakiwa ndio wengi 278.
Akizungumzia chanjo ya Corona Mhe Mazrui amesema Zanzibar ina chanjo za aina mbili Sinovac ya china na Sputnik light 5 na chanjo hizo zimeanza kwa makundi.