Watu 18 wauawa katika shambulio la wanamgambo wa Niger

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191

Raia 18 nchini Niger wameuawa katika shambulio la wanamgambo magharibi mwa nchi hiyo, serikali inasema.

Majambazi waliokuwa na pikipiki walivamia lori lililokuwa likisafirisha watu kati ya vijiji viwili vya mkoa wa Tillaberi.

Magharibi mwa Niger - kama vile nchi jirani za Mali na Burkina Faso - kwa miaka mingi imekuwa ikikabiliwa na mashambulio ya wanamgambo, licha ya juhudi za vikosi vya kimataifa vilivyotumwa katika eneo la Sahel kupambana na wanamgambo wa kijihadi.

Majirani wote wawili wa Niger sasa wana serikali za kijeshi baada ya wakuu wa jeshi kuwatimua tawala za kiraia, wakisema wameshindwa kukabiliana na uasi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…