Watu 200,000 hatarini kupoteza ajira Urusi kutokana na vikwazo

Watu 200,000 hatarini kupoteza ajira Urusi kutokana na vikwazo

John Haramba

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2022
Posts
365
Reaction score
1,374
Meya wa Jiji la Moscow Nchini Urusi, Sergei Sobyanin amesema kuwa takriban wafanyakazi 200,000 wa makampuni ya kigeni wanakabiliwa na hatari ya kupoteza ajira zao kutokana na vikwazo ilivyowekewa Urusi kufuatia uvamizi wake kwa Ukraine.

Sobyanin amesema wiki iliyopita, mamlaka iliidhinisha mpango wa dola milioni 41 kusaidia ajira katika Mji Mkuu wa Urusi na kwamba mpango huo unalenga wafanyakazi wa makampuni ya kigeni ambayo yamesimamisha shughuli zao kwa muda au kuamua kuondoka nchini Urusi.

Mamia ya makampuni hasa ya Magharibi yametangaza kusimamisha shughuli zao au kuondoka Urusi baada ya Rais Vladimir Putin kutuma wanajeshi wake Ukraine mnamo Februari 24, 2022.

Wataalamu wa uchumi wanaamini kwamba, vikwazo zaidi dhidi ya Urusi vinatarajiwa kuitumbukiza nchi hiyo katika mgogoro mkubwa wa kiuchumi.

Source: DW
 
Sijaelewa vyema, hao laki mbili wako mbioni kupoteza ajira Urusi au Moscow? Maana hapo aloongea ni meya wa moscow.

Ila bora Russia, siku US au EU ikifunga kampuni zake China nahisi itakuwa ni balaa na kilio kikuu china.
 
Sijaelewa vyema, hao laki mbili wako mbioni kupoteza ajira Urusi au Moscow? Maana hapo aloongea ni meya wa moscow.

Ila bora Russia, siku US au EU ikifunga kampuni zake China nahisi itakuwa ni balaa na kilio kikuu china.
Trump alijaribu kuhamasisha makampun kuhama China akashindwa
 
Trump alijaribu kuhamasisha makampun kuhama China akashindwa
Sio kwamba alishindwa, aliona vyema kubaki. Unataka kusema hakuna sehemu wanaweza wakapata cheap labour zaidi ya china? US aliamua kuwekeza china ili kwamba aje amshike vizuri kiuchumi. Tazama Balanc of Trade kati ya US na China kisha nambie nani anayemhitaji mwenzie kiuchumi.
 
Sijaelewa vyema, hao laki mbili wako mbioni kupoteza ajira Urusi au Moscow? Maana hapo aloongea ni meya wa moscow.

Ila bora Russia, siku US au EU ikifunga kampuni zake China nahisi itakuwa ni balaa na kilio kikuu china.
Mkuu Moscow ni mji mkuu wa Russia ukiambiwa makampuni yashafungwa Moscow ndio anazungumzia Russia huyo, kazi ndo zishabuma apo kila mtu arudi kwao atafute kibarua nchi nyengine urusi hakukaliki sasaiv wanapanga foleni kununua mkate
Urusi wanaongozwa ni kichwa cha mwendazimu mpaka watakapojielewa na kumtoa madarakani kwa nguvu zote putini wa mchongo
 
Hao 200,000 si ndo wahitimu wa tanzania tu wasio nakazi wa miaka mitano. Kwa inchi kama urusi yenye watu milion 150 hao ni wachache sana. Waondoke tu

Sent from my TECNO K7 using JamiiForums mobile app
 
Mkuu Moscow ni mji mkuu wa Russia ukiambiwa makampuni yashafungwa Moscow ndio anazungumzia Russia huyo, kazi ndo zishabuma apo kila mtu arudi kwao atafute kibarua nchi nyengine urusi hakukaliki sasaiv wanapanga foleni kununua mkate
Urusi wanaongozwa ni kichwa cha mwendazimu mpaka watakapojielewa na kumtoa madarakani kwa nguvu zote putini wa mchongo
Siyo kweli kama ni propaganda umefeli Urusi ni kati ya wazalishaji wakubwa wa ngano duniani iweje wapange foleni kwa ajili ya mikate? Yaani kama tz kipindi kile yalipokosa soko la mahindi nje ya nchi ndo unataka kusema watz tulipanga foleni kununua unga? Au mpunga ukikosa soko ndo watz wapange foleni kutafuta mchele? Hii inaonesha wengi hawajui chochote kuhusu Urusi.
Kwamba nchi izalishe chakula ikose soko halafu ndani ya hiyo nchi wananchi wateseke kutafuta chakula kilichotapakaa kila mahala ni akili za wapi hizi? Yaani Mtwara wazalishe korosho kwa wingi wakose soko halafu wana mtwara hao hao wapange foleni ndefu kununua korosho? Kumbe urusi anasemwa na MAMBUMBU yasiojua hata jiografi ya darasa la sita na ndo maana PUTIN KAWASHIKA VIJAMBIO
 
Sio kwamba alishindwa, aliona vyema kubaki. Unataka kusema hakuna sehemu wanaweza wakapata cheap labour zaidi ya china? US aliamua kuwekeza china ili kwamba aje amshike vizuri kiuchumi. Tazama Balanc of Trade kati ya US na China kisha nambie nani anayemhitaji mwenzie kiuchumi.
Jibu ni alishindwa na tatizo halikuwa cheap labour pekee bali pi na miundo mbinu China inasoko kubwa la bidhaa kuliko America na Europe kwa pamoja.

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
Siyo kweli kama ni propaganda umefeli Urusi ni kati ya wazalishaji wakubwa wa ngano duniani iweje wapange foleni kwa ajili ya mikate? Yaani kama tz kipindi kile yalipokosa soko la mahindi nje ya nchi ndo unataka kusema watz tulipanga foleni kununua unga? Au mpunga ukikosa soko ndo watz wapange foleni kutafuta mchele? Hii inaonesha wengi hawajui chochote kuhusu Urusi.
Kwamba nchi izalishe chakula ikose soko halafu ndani ya hiyo nchi wananchi wateseke kutafuta chakula kilichotapakaa kila mahala ni akili za wapi hizi? Yaani Mtwara wazalishe korosho kwa wingi wakose soko halafu wana mtwara hao hao wapange foleni ndefu kununua korosho? Kumbe urusi anasemwa na MAMBUMBU yasiojua hata jiografi ya darasa la sita na ndo maana PUTIN KAWASHIKA VIJAMBIO
Narudia hata kama urusi wanazalisha ngano, tunasema vikwazo vimesababisha demands kuwa kubwa kwa warusi hata kama wanazalisha wao., kabla ya vikwazo katika nchi yoyote ulimwenguni wananchi huwa wanakuwa na option mbali mbali za mahitaji lakini kama umebanwa inabidi tu upange foleni kuwania kile ulichonacho.,
 
Back
Top Bottom