John Haramba
JF-Expert Member
- Feb 4, 2022
- 365
- 1,374
Meya wa Jiji la Moscow Nchini Urusi, Sergei Sobyanin amesema kuwa takriban wafanyakazi 200,000 wa makampuni ya kigeni wanakabiliwa na hatari ya kupoteza ajira zao kutokana na vikwazo ilivyowekewa Urusi kufuatia uvamizi wake kwa Ukraine.
Sobyanin amesema wiki iliyopita, mamlaka iliidhinisha mpango wa dola milioni 41 kusaidia ajira katika Mji Mkuu wa Urusi na kwamba mpango huo unalenga wafanyakazi wa makampuni ya kigeni ambayo yamesimamisha shughuli zao kwa muda au kuamua kuondoka nchini Urusi.
Mamia ya makampuni hasa ya Magharibi yametangaza kusimamisha shughuli zao au kuondoka Urusi baada ya Rais Vladimir Putin kutuma wanajeshi wake Ukraine mnamo Februari 24, 2022.
Wataalamu wa uchumi wanaamini kwamba, vikwazo zaidi dhidi ya Urusi vinatarajiwa kuitumbukiza nchi hiyo katika mgogoro mkubwa wa kiuchumi.
Source: DW
Sobyanin amesema wiki iliyopita, mamlaka iliidhinisha mpango wa dola milioni 41 kusaidia ajira katika Mji Mkuu wa Urusi na kwamba mpango huo unalenga wafanyakazi wa makampuni ya kigeni ambayo yamesimamisha shughuli zao kwa muda au kuamua kuondoka nchini Urusi.
Mamia ya makampuni hasa ya Magharibi yametangaza kusimamisha shughuli zao au kuondoka Urusi baada ya Rais Vladimir Putin kutuma wanajeshi wake Ukraine mnamo Februari 24, 2022.
Wataalamu wa uchumi wanaamini kwamba, vikwazo zaidi dhidi ya Urusi vinatarajiwa kuitumbukiza nchi hiyo katika mgogoro mkubwa wa kiuchumi.
Source: DW