Watu 37 wauawa katika maporomoko ya udongo magharibi mwa Kenya

joto la jiwe

JF-Expert Member
Joined
Sep 4, 2017
Posts
26,117
Reaction score
46,617

Mafisa nchini Kenya wamethibitisha kuwa idadi ya watu waliofariki kutokana n atukio la maporomoko ya udongo katika eneo la Pokot magharibi imefikia 37 .

Hii ni baada ya nyumba zao kusombwa na mafuriko iliyotokana na mvua kubwa inayonyesha katika eneo hilo.

Maporomoko hayo yalioathiri zaidi vijiji vya Nyarkulian na Parua, yameripotiwa kusababishwa na mvua kubwa inayoripotiwa kuendelea kunyesha katika eneo hilo.

Vijiji hivyo vinasemekana kutenganishwa kabisa na mafuriko ambayo yameharibu daraja.

Maafisa pia wamesema kuwa miili ya watu 12, ikiwemo ya watoto saba zilipatikana asubuhi ya Jumamosi.

Joel Bulal, mmoja wa wasimamizi wa serikali katika eneo hilo ameliambia gazeti la Daily Nation kuwa shughuli za uokozi zinaenedelea huku na kuwatafuta wale ambao hawajulikani waliko

Kamishena wa jimbo hilo Apollo Okelo amesema watu wengine wengi huenda wamekwama chini ya matope na kuongeza kuwa shughuli ya kuwaokoa zinaathiriwana hali mbaya ya hewa.

"Tunajaribu kutafuta mahali ambapo daraja limesombwa na maji ya mafuriko,"alinukuliwa na mtando wa habari wa Standard nchiniKenya.

Picha zinazosambazwakatika mitandao ya kijamii zinaonesha miti iliyosombw ana maji na mingine kung'olewa, huku matope yakisambaa barabrani

Katika Twitter yake, Shirika la Msalaba mwekundu limethibitisha ripoti zinazoashiria tukio la maporomoko "makubwa" ya matope.

Kumeshuhudiwa mvua nyingi katika eneo la Afrika Mashariki na upembe wa Afrika kwa wiki kadhaa sasa.

Kijiji kizima kimesombwa na maji nchi Sudan Kusini huku visa ajaliya maporomoko ya ardhi ikiripotiwa Tanzania, Ethiopia na Somalia.

Wanasayansi wanasema hali mbaya ya hewa inatarajiwa kukumba baadhi ya nchi katika kanda hiyo kwasababu viwango vya joto katika bahari Hindi vinatarajiwa kupanda kupita kiasi cha kawaida, hali ambayo huenda ikasababisha mvua kubwa .
 
Mafisa nchini Kenya wamethibitisha kuwa idadi ya watu waliofariki kutokana n atukio la maporomoko ya udongo katika eneo la Pokot magharibi imefikia 36 .

Hii ni baada ya nyumba zao kusombwa na mafuriko iliyotokana na mvua kubwa inayonyesha katika eneo hilo.

Maporomoko hayo yalioathiri zaidi vijiji vya Nyarkulian na Parua, yameripotiwa kusababishwa na mvua kubwa inayoripotiwa kuendelea kunyesha katika eneo hilo.

Vijiji hivyo vinasemekana kutenganishwa kabisa na mafuriko ambayo yameharibu daraja.

Maafisa pia wamesema kuwa miili ya watu 12, ikiwemo ya watoto saba zilipatikana asubuhi ya Jumamosi.

Joel Bulal, mmoja wa wasimamizi wa serikali katika eneo hilo ameliambia gazeti la Daily Nation kuwa shughuli za uokozi zinaenedelea huku na kuwatafuta wale ambao hawajulikani waliko

Kamishena wa jimbo hilo Apollo Okelo amesema watu wengine wengi huenda wamekwama chini ya matope na kuongeza kuwa shughuli ya kuwaokoa zinaathiriwana hali mbaya ya hewa.

"Tunajaribu kutafuta mahali ambapo daraja limesombwa na maji ya mafuriko,"alinukuliwa na mtando wa habari wa Standard nchiniKenya.

Picha zinazosambazwakatika mitandao ya kijamii zinaonesha miti iliyosombw ana maji na mingine kung'olewa, huku matope yakisambaa barabrani

Katika Twitter yake, Shirika la Msalaba mwekundu limethibitisha ripoti zinazoashiria tukio la maporomoko "makubwa" ya matope.

Kumeshuhudiwa mvua nyingi katika eneo la Afrika Mashariki na upembe wa Afrika kwa wiki kadhaa sasa.

Kijiji kizima kimesombwa na maji nchi Sudan Kusini huku visa ajaliya maporomoko ya ardhi ikiripotiwa Tanzania, Ethiopia na Somalia.

Wanasayansi wanasema hali mbaya ya hewa inatarajiwa kukumba baadhi ya nchi katika kanda hiyo kwasababu viwango vya joto katika bahari Hindi vinatarajiwa kupanda kupita kiasi cha kawaida, hali ambayo huenda ikasababisha mvua kubwa .



Chanzo: BBC Swahili
 
Hata Sengerema Mkoani Mwanza , Kuna mafuriko yametokea, na Kuna vifo
 
Poleni Pia kule Sengerema Mkoani Mwanza.People should move to higher grounds for safety
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…