Lady Whistledown
JF-Expert Member
- Aug 2, 2021
- 1,147
- 2,008
Madai Mapya ya Unyanyasaji wa 'Dancers' yaibuliwa dhidi ya Mwanamuziki Lizzo, (Melissa Viviane Jefferson) baada ya Watu 3 kufungua madai kama hayo Wiki iliyopita
Mawakili wanaowakilisha Wacheza Dansi Watatu wa zamani wa Lizzo wamesema wanachunguza malalamiko mapya yaliyotolewa na watu 6 zaidi ambao walifanya kazi na Mwimbaji huyo
Watu hao wanatajwa kuwa walishiriki katika kuandaa 'Reality Show' ya Lizzo katika Studio za Amazon iitwayo "Lizzo's Watch Out for the Big Grrrls."
Mwanasheria wa Masuala ya Ajira, Ron Zambrano, amesema madai hayo yanahusu "mazingira yenye kashfa ya kingono" na kutofuatwa kwa malipo ya Wafanyakazi
Agosti 1, 2023 Wacheza Dansi Watatu waliofanya ziara ya Muziki na Lizzo, (Arianna Davis, Noelle Rodriguez na Crystal Williams) walifungua kesi wakidai walinyanyaswa Kingono, Kidini, Kwa misingi ya Rangi, na kufungwa kwa Sababu za Uongo na Mwanamuziki huyo
Akizungumzia tuhuma hizo, Lizzo amedai Madai yaliyotolewa dhidi yake siyo ya kweli na kuwa yeye sio muovu kama Vyombo vya Habari vinavyomwonesha
Chanzo: BBC
Mawakili wanaowakilisha Wacheza Dansi Watatu wa zamani wa Lizzo wamesema wanachunguza malalamiko mapya yaliyotolewa na watu 6 zaidi ambao walifanya kazi na Mwimbaji huyo
Watu hao wanatajwa kuwa walishiriki katika kuandaa 'Reality Show' ya Lizzo katika Studio za Amazon iitwayo "Lizzo's Watch Out for the Big Grrrls."
Mwanasheria wa Masuala ya Ajira, Ron Zambrano, amesema madai hayo yanahusu "mazingira yenye kashfa ya kingono" na kutofuatwa kwa malipo ya Wafanyakazi
Agosti 1, 2023 Wacheza Dansi Watatu waliofanya ziara ya Muziki na Lizzo, (Arianna Davis, Noelle Rodriguez na Crystal Williams) walifungua kesi wakidai walinyanyaswa Kingono, Kidini, Kwa misingi ya Rangi, na kufungwa kwa Sababu za Uongo na Mwanamuziki huyo
Akizungumzia tuhuma hizo, Lizzo amedai Madai yaliyotolewa dhidi yake siyo ya kweli na kuwa yeye sio muovu kama Vyombo vya Habari vinavyomwonesha
Chanzo: BBC