Kama ilivyo ada huwa nawaletea habari ambazo pengine mnazo ila hamtaki kuzisema na pengine hamna kabisa.
Mimi binafsi nahitaji kuona Wagombea wa chama changu Chadema wakishinda kwa kishindo, ila kwa yanayoendelea huko majimboni inakatisha sana tamaa.
Najua kuna changamoyo nyingi sana ikiwemo za kipesa kuwezesha wagombea wetu kufanya kampeni.
Lakini kwa hawa waliotoka bungeni kwenye bunge lililopita kuna tatizo kwao huko walikogombea kwa kuwa nina amini kabisa pesa walibaki nayo ya kutosha kufanya kampeni za jimbo.
Kumekuwa na sifa nyingi na mapambio kwa mgombea wetu wa Muheza mh. Yosepher Komba, ila cha kushangaza kwenye kampeni zake watu hamtokei (hii ni dharau na unafki wa hali ya juu).
Ukisoma post humu na comments kuhusu huyu mgombea alafu ukienda kwenye uhalisia, unaweza kuchoka kabisa.
Makamanda wenzangu tujirekebishe na pia tufanye namna juu chini kuweza kuwashawishi watu wa muheza kuhudhuria kampeni za mgombea wetu, la sivyo anaweza pata kura 2.
Chini hapa ni picha za mkutano wa kampeni wa mgombea wetu mh Yosepher Komba huko muheza. Watu wanaohudhuria kampeni yake hawafiki 20?
Nimeweka na video chini ili kuondoa maswali ya kijinga ya kuukataa ukweli uliopo.
Ulivyoukata Kwa wabunge, na Kwa wananchi hivyohivyo, watu hawendi si Kwa sabb wanapenda, kula, wanatafuta Kula, hivyo wakazane tu, watapigiwa Kura zao kutumia picha zao kwenye makaratasi ya NEC siku ya Uchaguzi, hata wasipowaona kabisa Wakati wa kamprni.
Ulivyoukata Kwa wabunge, na Kwa wananchi hivyohivyo, watu hawendi si Kwa sabb wanapenda, kula, wanatafuta Kula, hivyo wakazane tu, watapigiwa Kura zao kutumia picha zao kwenye makaratasi ya NEC siku ya Uchaguzi, hata wasipowaona kabisa Wakati wa kamprni
Nguvu majimboni ni ndogo sana ... Sasa tunawaza TL akishinda atawezaje kuunda serikali imara kama hata wabunge kumi kupata its too hard.
Nachelea kusema uwepo wake ni kuchangamsha kampeni?
Siyo kosa lako, Jiwe mwenyewe akiona umati wanaomsapoti lIssu anasema mikutano ya miaka ya nyuma? Hapo uanonyesha Bendera ya CHADEMA hujaonyesha mkutano mzee
Siyo kosa lako, Jiwe mwenyewe akiona umati wanaomsapoti lIssu anasema mikutano ya miaka ya nyuma? Hapo uanonyesha Bendera ya CHADEMA hujaonyesha mkutano mzee
Nakuita mjinga, kwa sababu kusoma hujui. Nimekuwekea video hapo ila kwa sababu ya uelewa wako hata hujui video ipoje na inafunguliwaje.
Nakuwekea tena hapa chini