Watu wahoji kwa nini CHADEMA imeanza kupunguza kasi ya kudai Katiba Mpya

Cha ajabu baada ya Mbowe kutoka jela amekuwa hana tena msisitizo wa kuzungumzia katiba mpya, hata anapopata nafasi ya kuongea ni kama anakwepakwepa kuzungumzia katiba mpya.
Mada yako inalenga uchokonozi tu.
Aliyoyaeleza Mbowe baada ya kukutana na Samia hukuyaelewa?

Kwa hiyo kwa maoni yako unataka CHADEMA wafanye kana kwamba hapakuwepo kabisa na mazungumzo kati ya Mwenyekiti wao na Rais na kukawa na mambo waliyokubaliana?
Hawakupeana muda, kuona jinsi hali itakavyoendelea baada ha mkutano huo?

Wape muda CHADEMA, wachambue mambo yao vizuri. Wamepitia katika hali ngumu sana, na wakati wote huo baadhi ya watu wakiwacheka na kuwaona kama wapuuzi.
Sasa inapojitokeza nafasi nzuri ya kuonyesha ukomavu wao, baadhi ya watu hawa wanataka chama hicho kirukeruke kama hawana akili? Na hawa watu ndio watakaokuwa mbele kusema, si mnawaona CHADEMA wasivyoweza kujiheshimu?

Wape muda wayapime waliyoahidiwa, na wakiona ni maneno matamu yanayolenga kupoteza muda, hapo wasipozinduka, lawama iwaandame.
 
"hadi kufikia watu kudhani kuwa Mbowe alikamatwa na kuwekwa ndani sababu ya Kudai katiba mpya!" Huu ni utopolo kwani hujui kuwa Mbowe alikamatwa kwa sababu ya kudai Katiba mpya??
Kwa hiyo akida katiba mpya atakamatwa tena au siyo?-Labda hataki kukamatwa tena ndo maana ishu ya katiba mpya kaanza kuipotezea
 
Wananchi wa Arusha tumapiga kazi tu hayo madai ya katiba mpya sijui wananchi gani wanadai ,maana kila mtu na mbishe za kutosha
 
Mwenyekiti anacheza kwa step, alitaka kuzingua naye akazinguliwa ndiyo maana kapoa....[emoji3]
 
hawasikilizwi wanapiga kelele katiba katiba hakuna wa kuwajali
 
Tutapata KATIBA mpya 2026. Ila hapo katikati ya 2022 Hadi 2026 haipo RANGI ambayo hutaiona!!!!!!!
 
Kwakuwa ipo jikoni imeshatiwa Nazi Bado kuepuliwa na kuanza kuila TU🤔
 
Wapuuzi wakubwa nyie John Pambalu kila siku anazunguka nchi nzima
 
watanzania wengi hawajitambui bora watoswe tu wananchi ndo ilipaswa waanze kudai katiba sio chadema
 
Ndugu yangu, Erythrocyte (aka RBC). Nimesikiliza kwa makini clip. Mzungumzaji anaongea kitu ambacho nilihisi kabla ya kusikiliza hii clip. Nashangaa kweli CHADEMA mara hii wamekwishaisahau CCM? Mbowe kweli ameaminishwa kuwa katiba mpya itakuja hivi hivi tu?
Karibu kwenye kongamano la Katiba mpya Mbeya
 

Hao wananchi wako pembeni wanasubiri tu CDM wakawasaidie kuidai katiba mpya! Wao wanataka katiba mpya lakini hawathubutu kuidai, bali wameona ni wajibu wa CDM. Basi CDM wamechoka, kwakuwa na wao wanaitaka na CDM hawajawazuia kuidai, basi wajitokeze waidai.
 
Katiba siyo agenda ya kipaumbele kwa wananchi walio wengi. Katiba ni agenda ya wanasiasa wachache. Ingekuwa ya wananchi wengi ingekuwa ishapatikana
Toka lini maiti zinadai katiba?
Tozo kibao,pembejeo zimepanda,mafuta yamepanda,wapukujapungua sh100 na cent,wananchi hao wananchi wapo kimya! HUO NI UMAITI
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…