Watu wanadanganya kuwa ajira ya serikali ina Job security kubwa, kumbe wanazunguka tu lengo hasa ni kusema ajira ya serikali ina madili mengi salama

Watu wanadanganya kuwa ajira ya serikali ina Job security kubwa, kumbe wanazunguka tu lengo hasa ni kusema ajira ya serikali ina madili mengi salama

Mwamuzi wa Tanzania

JF-Expert Member
Joined
Apr 7, 2020
Posts
15,486
Reaction score
45,256
Watu wanavyosema ajira za serikali zina job security maana yake ni kwamba unaweza kupiga dili na ukajulikana lakini usichukuliwe hatua yoyote.

Hata warning letter hupewi.

Maana kuanzia Mkurugenzi, meneja, mpaka mfagizi na mlinzi wanajuana madili yao.

Sasa wa chini au wa kati akiharibu kwanza bosi anawaza nikimkomalia sana huyu lazima ataibua na mengine akaniharibia.

Pili anawaza ile kibinadamu mbona Mimi mwenyewe nakula kwa urefu wa kamba yangu ngoja huyu nimpotezee tu.

Sekta binafsi mara nyingi mkurugenzi ndiye mmiliki wa kampuni au ndiye mtu ambaye kampuni inamlipa vizuri na kumfanya kampuni aione mali yake. Wa chini au wa kati ukiharibu hawezi kukutupia taulo . Lazima ufukuzwe.
 
Watu wanavyosema ajira za serikali zina job security maana yake ni kwamba unaweza kupiga dili na ukajulikana lakini usichukuliwe hatua yoyote.

Hata warning letter hupewi.

Maana kuanzia Mkurugenzi, meneja, mpaka mfagizi na mlinzi wanajuana madili yao.

Sasa wa chini au wa kati akiharibu kwanza bosi anawaza nikimkomalia sana huyu lazima ataibua na mengine akaniharibia.

Pili anawaza ile kibinadamu mbona Mimi mwenyewe nakula kwa urefu wa kamba yangu ngoja huyu nimpotezee tu.

Sekta binafsi mara nyingi mkurugenzi ndiye mmiliki wa kampuni au ndiye mtu ambaye kampuni inamlipa vizuri na kumfanya kampuni aione mali yake. Wa chini au wa kati ukiharibu hawezi kukutupia taulo . Lazima ufukuzwe.
Hata uchome mtu kisu haufukuzwi
 
Kwa hiyo waziri mkuu kusema twende
VETA kashawaka fungu lake huko
 
Back
Top Bottom