Watu wanaipenda dunia kuliko ahera

Watu wanaipenda dunia kuliko ahera

Joined
Jul 6, 2024
Posts
97
Reaction score
72
Haamini Kama Kuna Siku ya Kiama

Ukijiona wewe ni kiongozi, na unaona watu unaowaongoza wanalalamikia uvunjifu wa Katiba, kanuni, miongozo, na taratibu ambazo kwa viapo vyako na ahadi yako kwa CCM uliahidi kuvilinda, kuvihifadhi, na kuvitetea, basi fahamu kuwa unafanya kosa kubwa.

Mheshimiwa Rais anasisitiza haki, lakini wewe husikii, umeweka pamba masikioni. Viongozi wa dini wanahubiri haki, lakini wewe husikii. Viongozi wa kitaifa wanahubiri haki, lakini wewe husikii. Umekuwa mkaidi.

Ujue wewe, hata ukitamka neno Mwenyezi Mungu, unajitamkusha tu kutuzuga. Wewe ni tapeli. Upo unasubiri kumaliza tu maisha ya kidunia ili uende zako kuishi motoni. Ndiyo maana hujali vilio vya mafukara, na ndiyo maana ukiona mtu anaandika ukweli, roho yako chafu inakereka.

Bado muda unao. Badilika. Acha kujisahaulisha kwa utamu wa fedha za kuwadhulumu mafukara wanaostahili. Kumbuka daima kuwa moto wa Jahanam kuni zake ni watu na mawe. Na inavyoonekana, usipobadilika na kuacha kufuru, utakuwa mmoja ya kuni za Jahanam.

Kidumu Chama Cha Mapinduzi.

Mathias Mugerwa Kahinga
 
Wengine hawaanini kama kuna hiyo akhera
 
Dunia uwanja wa fujo, sio sehemu ya kuoneana huruma, ukihisi unaonewa chukua hatua, usijifiche kwenye 'unyonge' utanyongwa kweli
 
KIONGOZI ALIYEMEZWA NA DUNIA KWA UTAMU WA KYWAHADAA NA KUWADHULMU MAFUKARA
HAAMINI KAMA KUNA SIKU YA KIAMA

Ukijiona

Wewe ni Kiongozi

Unaona Watu unao waongoza
Wanalalamikia
Uvunjifu wa Katiba , Kanuni miongozo na Taratibu
Ambayo Wewe Kiongozi kwa Viapo vyako na Ahadi yako kwa CCM uliahidi
Kuvilinda
Kuvihifadhi
Na kuvitetea
Mheshimiwa Rais anasisitiza Haki
Wewe husikii umeweka pamba masikioni
Viongozi wa Dini wanahubiti haki
Wewe husikii
Viongozi wa Kitaifa wanahubiti haki Wewe husikii
Umekuwa nunda
Ujuwe Wewe
Hata ukitamka neno Mwenyezi Mungu
Ujuwe unajitamkusha tu kutuzuga
Wewe ni Tapeli
Upo unasubiri kumaliza tu Maisha ya kidunia ili uende zako kuishi motoni.
Ndiyo Maana hujali vilio vya mafukara
Ndiyo maana ukiona mtu anaandika Ukweli liroho lako lichafu linakereka .
Bado muda unao
Badilika
Acha kujisahaulisha kwa utamu wa fedha za kuwadhulmu Mafukara wanaostahili.
Khmbuka Daima yakuwa
Moto wa Jahanam
Kuni zake ni watu na Mawe
Na inavyoonekana
Usipobadilika na kuacha kufuru utakuwa Mmoja ya kuni za Jahanam


Kidumu Chama Cha Mapinduzi


Mathias Mugerwa Kahinga
Wanahisi ahera inaweza kuwa kiini macho
 
Sasa kwan wewe hujasikia wahenga wakisema "heri kenda shika kuliko kumi nenda uje?".
Uache cha mkononi kwa unachopogia hesabu kukipata na hujakipa bado?

Dunian tunapajua, akhera hatupajui na waliokwemda hawajawah kutupa feedbacknkukoje, sasa tutapapenda vipi mahala ambapo tunapasikia tu na hatujawah kufika
 
Jamii ambayo Mwizi anatukuzwa na kuheshimiwa na Viongozi wa Dini wanapokea Sadaka zake.

Jamii hiyo hiyo ndio imezaa Viongozi Wezi.
 
Back
Top Bottom