Watu wanaoomba misaada mitaani yadaiwa kuwa ni miradi ya watu. Je, kuna ukweli?

Watu wanaoomba misaada mitaani yadaiwa kuwa ni miradi ya watu. Je, kuna ukweli?

Suley2019

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2019
Posts
2,203
Reaction score
5,610
omba.jpg

Salaam ndugu zangu,

Katika pitapita zangu za hapa na pale nimekutana na watu adhaa wakanionya kuwasaidia watu naokutana nao njiani na kunisisitiza kuwa makini.

Wadau wanasema kwamba watu wengi wanaomba mijini hawafanyi hivyo kwa ajili yao bali kuna baadhi ya watu wenye vipato vikubwa ambao wanawatoa watu vijijini kisha kuwafanya ombaomba na jioni wanapeleka hesabu.

Inaelezwa kuwa watu hao pia wamewakusanya na kuwaajiri watu kwenye biashara za karanga na mayai kisha jioni wanaenda kupeleka hesabu.

Je, kuna ukweli katika hili?

Kama kweli je vyombo vya usalama vinakwama wapi kuhakikisha wanazuia watu kufanywa bidhaa?
 
Salaam ndugu zangu,

Katika pitapita zangu za hapa na pale nimekutana na watu adhaa wakanionya kuwasaidia watu naokutana nao njiani na kunisisitiza kuwa makini...
Kuna wadada/wamama wa umri wa kati mitaani nao Huwa wanaomba buku za unga au hela ya chakula Huwa siwaelewi kabisa malengo yao Hasa mida ya jioni sa moja moja hivi.

Halafu siyo walemavu wala nini
 
Salaam ndugu zangu,

Katika pitapita zangu za hapa na pale nimekutana na watu adhaa wakanionya kuwasaidia watu naokutana nao njiani na kunisisitiza kuwa makini...
Haujakosea upo sahihi kabisa mi nipo Moro Kuna madogo wamemaliza tu la 7 vijijini jamaa kawakusanya kawaleta mjini,asubuhi wanachemshiwa mayai kibao wanapenda kuzungusha wanaleta pesa jioni,na kuhusu omba omba ni ukweli pia Tena wengine ni omba omba WA kimataifa,

Kuna walemavu wanasafirishwa kutoka bongo ( Mwanza) na mikoa mingine kwenda Kenya kwa ajili ya kutumikishwa kwenye kuomba omba
 
Kuna mmoja yupo na wheelchair kila siku nampita kimya kimya.. jamaa mpk kanikariri akiniona hakingi mkono.

Shida ilianzia pale alipomkuta mwenzie anaomba msaada yeye akasogea kwa mbele yake ili amzibie yule wa kwanza (Huo mchezo niliusoma)

Huyo aliyezibiwa lizk nae hakuridhika (ni mlemavu wa macho) akaamua asogee mbele zaidi. Naona hakuridhika akaamua aite wenzie wafanye ubunifu (Wapige ngoma na spika kubwa)

Huyo wa wheelchair akaona sio poa.

Akaamua abebe Biblia aanze kuhubiri kuhusu kutoa misaada kwa watu wa hali yao.

Mie huo mchezo nausoma maana ndio njia yangu kila siku.

Nikasema hawa wote hawataiona hela yangu.
 
Kuna wadada/wamama wa umri wa kati mitaani nao Huwa wanaomba buku za unga au hela ya chakula Huwa siwaelewi kabisa malengo yao Hasa mida ya jioni sa moja moja hivi.

Halafu siyo walemavu wala nini
Hawa nimekutana nao mwanamke mzuri anakuomba 1000 akawanunulie chakula.alaf mida ya night saa1,2 asilimia kubwa wanajiuza kwa njia mpy tuliweka mtego kwa 3 njia zao wanazijua target sio 1000 bali muongee biashara
 
Kuna wadada/wamama wa umri wa kati mitaani nao Huwa wanaomba buku za unga au hela ya chakula Huwa siwaelewi kabisa malengo yao Hasa mida ya jioni sa moja moja hivi.

Halafu siyo walemavu wala nini
Hawa nimekutana nao mwanamke mzuri anakuomba 1000 akawanunulie chakula.alaf mida ya night saa1,2 asilimia kubwa wanajiuza kwa njia mpy tuliweka mtego kwa 3 njia zao wanazijua target sio 1000 bali muongee biashara
 
Unauliza majibu shee?Watu wanaenda chukua vilema vijijni na kuahidi kuja kuwapa maisha mazuri town.Ila wakifika picha linaanza kila Mmoja anapewa wheelchair na bakuli,na mtu wa kumsukuma,anapangiwa hesabu.Hii Dunia yakipuuzi sana
 
Unauliza majibu shee?Watu wanaenda chukua vilema vijijni na kuahidi kuja kuwapa maisha mazuri town.Ila wakifika picha linaanza kila Mmoja anapewa wheelchair na bakuli,na mtu wa kumsukuma,anapangiwa hesabu.Hii Dunia yakipuuzi sana
Daah noma sana. Shida kuwajua wenye shida kweli na wahuni ni changamoto
 
Kuna ubaya gani mtu mwenye mtaji wa kuuza karanga na mayai akaanzisha biashara hiyo kisha akaajiri watu wa kumtembezea bidhaa hizo mitaani? Ubaya upo kwenye kuwafanya watu wakaombeombe mitaani kisha wampelekee hesabu. Kuajiri ombaomba hilo haliko sawa
 
Hawa nimekutana nao mwanamke mzuri anakuomba 1000 akawanunulie chakula.alaf mida ya night saa1,2 asilimia kubwa wanajiuza kwa njia mpy tuliweka mtego kwa 3 njia zao wanazijua target sio 1000 bali muongee biashara
Du hatari Sana, maanake ule ni mtongozo.
 
Ingekuwa vyema kama ungetoa location kabisa mkuu.
Hawa nimekutana nao mwanamke mzuri anakuomba 1000 akawanunulie chakula.alaf mida ya night saa1,2 asilimia kubwa wanajiuza kwa njia mpy tuliweka mtego kwa 3 njia zao wanazijua target sio 1000 bali muongee biashara
 
Matapeli wamekua na mbinu nyingi za kuchukua hela za watu kiasi kwamba imepelekea hata kama MTU kama ni mhitaji kweli kweli unashindwa kusaidia . Siku moja nimekutana na mwanamke mmoja na mtoto mgongoni maeneo flani nchini ananiomba nauri ya kutoka mji mmoja hadi mwingine kwasababuî amepoteza fadha s ,Sasa cha kushangaza MTU yule yule katika madhingira to fauti anakuja na ombi like lie ndipo nilipogundua kuwa haya mambo ni kuwa makini unapo amua kusaidia.
 
Back
Top Bottom