Watu wanaweza wasielewe thamani ya matendo yako leo, lakini watatambua umuhimu wako ukishaondoka!

Dogoli kinyamkela

JF-Expert Member
Joined
Nov 21, 2024
Posts
618
Reaction score
1,440
Nyani na tumbili walipojua kwamba mkulima aliyewafukuza kutoka kwenye shamba la mahindi amekufa, walisherehekea kwa furaha.

Lakini mwaka uliofuata hakukuwa na mahindi tena. Hapo ndipo walipogundua kwa uchungu kwamba mkulima waliyemdhania kuwa adui yao ndiye mkulima aliyelima mahindi.

Watu wanaweza wasielewe thamani ya matendo yako leo, lakini watatambua umuhimu wako ukishaondoka!
 
Kweli mkuu!
 
Kuna Jamaa waliungana na mama Yao,kila siku kumshambulia Baba Yao!Alipofariki Mzee wa watu kwa stress,wakaanza kuuza magari kwa bei ya kutupa na duka kufilisika,Ndipo mzozo ulipoanza mama na watoto, watoto wanadai mama ulitupotosha ona Sasa jembe halipo tuna Hali mbaya!
 
Yaan acha tu mkuu
 
Leo tunakumbuka michango mingi ya wanasayansi kama Tesla na wengine ambao teknolojia zao zimekuwa msaada kubwa.Kama tungetambua thamani zao mwanzoni tungekuwa mbali sana.
 
Inatokea sana kwenye jamii, vile jamii hua inamuonea huruma mwanamke hata avurunde vipi. Umuhim wa baba huonekanq baadae
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…