figganigga
JF-Expert Member
- Oct 17, 2010
- 25,724
- 55,906
Watu wasiofahamika wamekata nguzo za umeme katika eneo la Kola B mjini Morogoro kwa lengo la kuiba kopa na mafuta ya Transfoma katika line kuu ya umeme na kulisababishia shirika la umeme Tanesco hasara ya zaidi ya shilingi milioni 200.
ITV imeshushudia wafanyakzi wa shirika la umeme Tanesco wakifanya jitihada za kubadilisha nguzo zilizokatwa ambapo afisa habari na uhusinao washirika hilo Esta Msacky amesema matukio ya kuhujumu miunombinu ya umeme yanaongezeka mkoni Morogoro na kusababisha hasara na usumbufu kwa wananchi kukosa huduma ya umeme
Nao wakazi wa mkoa wa Morogoro wa kizungumzia tukio hilo wametupia lawama na kulitaka shirika hilo kuangalia upya watumishi wake wanaoshirikiana na vishoka katika kuharibu miundominu badala ya kualumu wananchi pekee.
==========================
UPDATES
Watu wawili wanashikiliwa na jeshi la polisi mkoa wa Morogoro baada ya kupatikana na lita 30 za mafuta ya transfoma baada yakukata nguzo za umeme kuvunja transfoma na kuiba mafuta na kusababisha wakazi wa eneo la kola mjini Morogoro kukosa huduma ya umeme kwa muda mrefu.
Kamanda wa polisi mkoa wa Morogoro Leonard Paul amethibitisha kukamatwa kwa watu hao ambapo amesema watuhumiwa walikamatwa katika eneo la kola kwa kamnyonge manispaa ya Morogoro wakihujumu miundombinu ya umeme ikiwemo kuiba mafuta ya trasfoma na kukata nguzo za umeme ambapo jeshi la polisi linaendelea kuwahoji watu hao na mara baada ya upelelezi kukamilika watafikishwa mahakamani.
Naye afisa uhusiano wa shilika na umeme Tanesco mkoa wa Morogoro Ester Msaki amsema mafuta hayo yana thamini ya zaidi ya shilingi laki tatu ambapo amewataka wananchi kuendelea kuwa na ushirikiano kwa kuwafichua wanaohujumu miundombinu ya umeme kwani shirika linaendelea kupata hasara na kusababisha baadhi ya wananchi kukosa huduma ya umeme.
Kwa upande wao wakazi wa manispaa ya Morogoro wameiomba serikali kuongeza ulinzi na kuwachukilia hatua kali watakaobainika wakihujumu miundombinu ya umeme na kusababisha wananchi kuishi gizani kwakukosa huduma ya umeme.
Chanzo: ITV
PIA SOMA
- Uelewa wangu juu ya kundi la watu wasiojulikana
~ Matukio ya Watu kupotea na wengine kudaiwa kutekwa, nini kinaendelea kuhusu usalama wa raia
- Kiongozi wa Madaktari (Dr. Ulimboka) atekwa, aokotwa akiwa katika hali mbaya sana
ITV imeshushudia wafanyakzi wa shirika la umeme Tanesco wakifanya jitihada za kubadilisha nguzo zilizokatwa ambapo afisa habari na uhusinao washirika hilo Esta Msacky amesema matukio ya kuhujumu miunombinu ya umeme yanaongezeka mkoni Morogoro na kusababisha hasara na usumbufu kwa wananchi kukosa huduma ya umeme
Nao wakazi wa mkoa wa Morogoro wa kizungumzia tukio hilo wametupia lawama na kulitaka shirika hilo kuangalia upya watumishi wake wanaoshirikiana na vishoka katika kuharibu miundominu badala ya kualumu wananchi pekee.
==========================
UPDATES
Kamanda wa polisi mkoa wa Morogoro Leonard Paul amethibitisha kukamatwa kwa watu hao ambapo amesema watuhumiwa walikamatwa katika eneo la kola kwa kamnyonge manispaa ya Morogoro wakihujumu miundombinu ya umeme ikiwemo kuiba mafuta ya trasfoma na kukata nguzo za umeme ambapo jeshi la polisi linaendelea kuwahoji watu hao na mara baada ya upelelezi kukamilika watafikishwa mahakamani.
Naye afisa uhusiano wa shilika na umeme Tanesco mkoa wa Morogoro Ester Msaki amsema mafuta hayo yana thamini ya zaidi ya shilingi laki tatu ambapo amewataka wananchi kuendelea kuwa na ushirikiano kwa kuwafichua wanaohujumu miundombinu ya umeme kwani shirika linaendelea kupata hasara na kusababisha baadhi ya wananchi kukosa huduma ya umeme.
Kwa upande wao wakazi wa manispaa ya Morogoro wameiomba serikali kuongeza ulinzi na kuwachukilia hatua kali watakaobainika wakihujumu miundombinu ya umeme na kusababisha wananchi kuishi gizani kwakukosa huduma ya umeme.
Chanzo: ITV
PIA SOMA
- Uelewa wangu juu ya kundi la watu wasiojulikana
~ Matukio ya Watu kupotea na wengine kudaiwa kutekwa, nini kinaendelea kuhusu usalama wa raia
- Kiongozi wa Madaktari (Dr. Ulimboka) atekwa, aokotwa akiwa katika hali mbaya sana