Watu wote si wabaya, ila wabaya ni wale

Watu wote si wabaya, ila wabaya ni wale

Mshangazi dot com

JF-Expert Member
Joined
Nov 19, 2011
Posts
1,345
Reaction score
3,503
  1. Wanaotelekeza watoto wao na wanaokimbia majukumu ya kifamilia (ikiwemo kutunza wazazi wakizeeka).
  2. Wanaowaonea wivu wengine na kuweka nguvu kwenye kuwashusha kiuchumi na au kuwazibia fursa kwenye shughuli zao za kujiingizia kipato.
  3. Wanaochepuka kwenye mahusiano na kuleta magonjwa kwa wenza wao.
  4. Wanaoiba, wabinafsi na wala rushwa.
  5. Wanaoharibu maisha ya mabinti na vijana wadogo hasa wa shule kwa kuwadanganya na kuwaingiza kwenye mahusiano yasiofaa.
  6. Wanaotoa siri na madhaifu ya ndani ya wenza wao wa ndoa kwa marafiki au familia zao.
  7. Wanaopiga na kunyanyasa wenza wao kihisia, ukatili wa kimwili, kisaikolojia (ikiwemo kuwanyima unyumba) na kwa kutumia dini au mila.
  8. Wanaoficha ndoa zao au mahusiano yao ili kuwarubuni wengine.​
Ongezea na wewe sifa nyingine za watu wasiofaa 🚫🔥🙅🏽‍♀️
 
Back
Top Bottom