John Haramba
JF-Expert Member
- Feb 4, 2022
- 365
- 1,374
Watuhumiwa wa mauaji ya mtumishi wa kanisa katoliki Makambako Nickson Myamba (46) wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Njombe.
Hakimu Mkazi Mfawidhi Wilaya ya Njombe, Matilda Kayombo akitaja shauri namba 5 la mwaka 2022 linalowakabili Daniel Mwilango (42) na Nickson Nyamideko (23) kuwa ni la mauaji yaliyotokea Makambako mkoani Njombe.
Alisema marehemu alikuwa Katibu wa Halmashauri ya Walei Kanisa la Romani Katoliki Kigango cha Parokia ya Makambako mjini Njombe.
Alisema watuhumiwa hao wanadaiwa kuhusika na mauaji ya Nickson Myamba yaliyotokea Februari 7 mwaka huu huko mjini Makambako.
Wakili wa Serikali Magdalena Kisoka akisaidiwa na Paul Ngonyani walisema kosa wanalokabiliwa nalo ni Kinyume na kifungu namba 196 na 197 cha kanuni ya adhabu Sura ya 16 ya sheria ya makosa ya jinai kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2019.
Aidha, Hakimu Magdalena Kisoka amepanga tarehe ya kusikilizwa shauri hilo ambapo itakuwa tarehe 28 Februari 2022 kutokana na kutokamilika kwa upelelezi wa shauri hilo.
Hata hivyo watuhumiwa hao wamerejeshwa rumande kutokana na kesi inayowakabili kutokuwa na dhamana.
Watuhumiwa hao wawili Nickson Nyamwideko na Daniel Mwilango wanashikiliwa kwa tuhuma za kumpiga na chuma na kumkata kwa panga vipande vipande na kusababisha kifo cha Nickson Myamba kilichotokea mtaa wa Mangula Mjini Makambako mkoani Njombe.
Kuhusu mauaji hayo, soma:
Hakimu Mkazi Mfawidhi Wilaya ya Njombe, Matilda Kayombo akitaja shauri namba 5 la mwaka 2022 linalowakabili Daniel Mwilango (42) na Nickson Nyamideko (23) kuwa ni la mauaji yaliyotokea Makambako mkoani Njombe.
Alisema marehemu alikuwa Katibu wa Halmashauri ya Walei Kanisa la Romani Katoliki Kigango cha Parokia ya Makambako mjini Njombe.
Alisema watuhumiwa hao wanadaiwa kuhusika na mauaji ya Nickson Myamba yaliyotokea Februari 7 mwaka huu huko mjini Makambako.
Wakili wa Serikali Magdalena Kisoka akisaidiwa na Paul Ngonyani walisema kosa wanalokabiliwa nalo ni Kinyume na kifungu namba 196 na 197 cha kanuni ya adhabu Sura ya 16 ya sheria ya makosa ya jinai kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2019.
Aidha, Hakimu Magdalena Kisoka amepanga tarehe ya kusikilizwa shauri hilo ambapo itakuwa tarehe 28 Februari 2022 kutokana na kutokamilika kwa upelelezi wa shauri hilo.
Hata hivyo watuhumiwa hao wamerejeshwa rumande kutokana na kesi inayowakabili kutokuwa na dhamana.
Watuhumiwa hao wawili Nickson Nyamwideko na Daniel Mwilango wanashikiliwa kwa tuhuma za kumpiga na chuma na kumkata kwa panga vipande vipande na kusababisha kifo cha Nickson Myamba kilichotokea mtaa wa Mangula Mjini Makambako mkoani Njombe.
Kuhusu mauaji hayo, soma:
- Makambako: Katibu wa Baraza la Walei auawa ndani ya eneo la Kanisa Katoliki, kichwa chatenganishwa na kiwiliwili
- Njombe: Akamatwa akituhumiwa kumuua Katibu wa Baraza la Walei Kanisa la Roman Katoliki