KERO Watumishi Hatulipwi likizo Morogoro kwanini?

KERO Watumishi Hatulipwi likizo Morogoro kwanini?

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest
Kumekuwa na tatizo la wakurugenzi na wakuu wa idara Mkoa wa Morogoro hasa Manispaa ya Morogoro kuwazungusha Watumishi hela zao za nauli wakati wa kwenda likizo.

Hili ni tatizo limekuwa likijirudia na limekuwa mazoea (Kero) ya muda mrefu. Wadau na Watumishi tumekuwa tukizungushwa mara kwa mara , Kero zinakuwa nyingi ikifika kipindi Cha kutakiwa kulipwaa nauli Huwa wakuu wa idara hasa elimu na afya kutoa sababu zisizoeleweka. Ikama inafahamika kwa Kila mwaka Watumishi gani wanakwenda likizo na inahitajika walipwe nauli zao kwa kuzingatia vigezo/ nauli za LATRA lakini inakuwa sivyo.

Wakuu wa idara hutoa nauli nusu na mara nyingine hawatoi kabisa kwa Watumishi hawa. Waziri mhusika ashughulikie hili imekuwa Kero kubwa. Watu wengi hudhani wanalalamikia hili . Mfano likizo ya mwaka huu 2024 Watumishi likizo zao zilianza tarehe 6/12/2024 lakini mpaka Sasa bado hawajalipwa.

Hii ni Kero, tunataka kukomaa kwa tabia hii mbaya, kwamba pesa za nauli zinapangiwa matumizi mengine na swala la nauli halizingatiwi. Walipe nauli hizo haraka ni haki ya Msingi kwa mfanyakzi kulipwaa nauli na kupata likizo Ili kuongeza ufanisi wakati wa Kazi.
 
Samia mitano Tena. ...RAIS KALALA WALA HANA SHIDA NA RAIA...JPM ALIKUWA na madhaifu lakin alikuwa Bora zaidi
 
Hebu fanya kazi, tuifukue PEPMISS yako ulivyojaza uongo mtupu
 
Back
Top Bottom