Tetesi: Watumishi hewa ndani ya jeshi la polisi!

Tetesi: Watumishi hewa ndani ya jeshi la polisi!

ZamdaIssa

JF-Expert Member
Joined
Nov 10, 2015
Posts
879
Reaction score
1,458
Hongera mheshimiwa na Mtukufu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kazi nzuri unayoifanya ya kutumbua majipu. Endelea na mwendo huohuo mpaka sisi wanyonge tupate walau kuonja keki ya Taifa hili japo kidogo!

Hongera pia Waziri Charles Kitwanga kwa kuchaguliwa kuwa waziri wa Wizara ya Mambo ya ndani ya nchi, Usalama wetu uko mikononi mwako ingawa na sisi wenyewe wananchi tunajilinda.

Hon.Pres. Magufuli, Agizo lako kuhusu kubaini watumishi hewa linatekelezwa ijapokua kwa spidi ya Taratibu kidogo, Labda kutokana na ugumu wa kukusanya Takwimu(Sijui)

Mhe Rais, Tunaomba Umulike Jeshi letu la Polisi, watumishi hewa wako wengi, kila siku askari Polisi wa vitengo mbalimbali wanafukuzwa kazi, wengine wanaacha kwa ridhaa zao, wapo wanaofariki. Lakini cha ajabu salary slip za askari hawa bado zinatolewa kila mwezi kutoka Hazina! ina maana kwamba mshahara unaendelea kuingizwa kwenye account zao!

Nimesikia Watumishi wa Wizara hii wameshahakikiwa!lakini mheshimiwa Rais tunaomba Wizara irudie tena uhakiki huo kwa umakini zaidi, Wastaafu wengi wa Polisi wanapokea Mishahara isiyo halali!

Nina Imani Polisi peke yake inaweza kuwa na watumishi hewa zaidi ya 2000, Magufuli mulika!
 
aiseee babayangu ww kama ni askari police uliyepata mafunzo miez 9 pale ccp moshi na kuapa kiapo cha police basi unakwenda kinyume na maadili ya kazi yako..kutoa siri za kazi yako wachiee wenyewe wafanye kazi yao....
 
polisi?? tutahakikiwa idara zingine tu sio hizo za usalama,unajua kwann? sana sana km hivo unaambiwa zimehakikiwa tyr lkn hutapata maelezo ya ziada,hujawahi kusikia zile kauli kwamba hili swala linahusu usalama wa taifa? hasahasa ufisadi unaogusa wasioguswa,ukielewa kwann wanasema hivo bila shaka utajua kwann hatutakaa tusikie watumishi hewa waliotumbuliwa pande hizo.hapa kazi tu
 
aiseee babayangu ww kama ni askari police uliyepata mafunzo miez 9 pale ccp moshi na kuapa kiapo cha police basi unakwenda kinyume na maadili ya kazi yako..kutoa siri za kazi yako wachiee wenyewe wafanye kazi yao....
Ningekuwa Polisi ningeshukuru,Bado nahangaika kutafuta Ajira.Polisi wenyewe ndio wanazungumza hayo huku mtaani tena bila hata kuulizwa
 
polisi?? tutahakikiwa idara zingine tu sio hizo za usalama,unajua kwann? sana sana km hivo unaambiwa zimehakikiwa tyr lkn hutapata maelezo ya ziada,hujawahi kusikia zile kauli kwamba hili swala linahusu usalama wa taifa? hasahasa ufisadi unaogusa wasioguswa,ukielewa kwann wanasema hivo bila shaka utajua kwann hatutakaa tusikie watumishi hewa waliotumbuliwa pande hizo.hapa kazi tu
Ni kweli mkuu,Kuna Idara na Wizara Untouchable nchi hii[emoji22] [emoji24]
 
uliyeleta thread hii kama ni askali basi uaskali wako mdogo sana.trained soldier ana channel za kuwasilisha habari.ndio maana zamani wanajeshi na polisi walikuwa wahehe na wakulya wee utakuwa mtu wa ...................
 
Ningekuwa Polisi ningeshukuru,Bado nahangaika kutafuta Ajira.Polisi wenyewe ndio wanazungumza hayo huku mtaani tena bila hata kuulizwa
SI JAMBO ZURI KUPIGA FITINA NA UNOKO HIYO NI ZAMBI KWA BABA MBINGUNI.
 
Watumbuliwe tuu...japo hao huwa ndio wanajua milki za wakubwa na kuwakingia vifua kwa kigezo cha usalama wa taifa.
 
uliyeleta thread hii kama ni askali basi uaskali wako mdogo sana.trained soldier ana channel za kuwasilisha habari.ndio maana zamani wanajeshi na polisi walikuwa wahehe na wakulya wee utakuwa mtu wa ...................
Siri zenye manufaa kwa taifa na sio kila siri inatunzwa coz wao wenyewe ndio wakamataji wa wahujumu iweje wao wawe wahujumu na waachwe eti kwa sbb ni jeshi na litaanza vurugu. Wafate maadili ndo hapo watastahili heshima na sio jeshi la kulinda uovu...WATUMBULIWE hao wanaokula na wafanyakazi hewa!!!
 
siri kwenye wizi? aliyeanzisha thread na wanaomuunga mkono ni mashujaa! pia wazalendo!
 
Kwenye mashirika ya uma, polisi nakwingineko ndo kuna watumishi hewa wengi kuliko TAMISEMI kwa sababu huko kwingine kazi ya mtu iko mikononi mwa Boss fulani atacho amua ndo hicho hamna kubadrisha kwa kweli Mtoa mada ubalikiwe. wananchi tunaomba majeshi yote ya hakikiwe na yatangazwe kama wafanyakazi walioko chini ya TAMISEMI wanavyo tangazwa. Jamani mbona hatusikii watumishi hewa kwenye majeshi yetu au wenyewe hawastahili hili zoezi? kila siku tu nasikia tu mkoa, mara wilaya... mbona mashirika hatusikii chochote hasa jeshi la polisi na UDsm, USA, MNH.. nakwingineko? au mumelenga walimu wa primary tu!
 
Kwenye mashirika ya uma, polisi nakwingineko ndo kuna watumishi hewa wengi kuliko TAMISEMI kwa sababu huko kwingine kazi ya mtu iko mikononi mwa Boss fulani atacho amua ndo hicho hamna kubadrisha kwa kweli Mtoa mada ubalikiwe. wananchi tunaomba majeshi yote ya hakikiwe na yatangazwe kama wafanyakazi walioko chini ya TAMISEMI wanavyo tangazwa. Jamani mbona hatusikii watumishi hewa kwenye majeshi yetu au wenyewe hawastahili hili zoezi? kila siku tu nasikia tu mkoa, mara wilaya... mbona mashirika hatusikii chochote hasa jeshi la polisi na UDsm, USA, MNH.. nakwingineko? au mumelenga walimu wa primary tu!
Ahsante mkuu,sisi vijana ndio wa kuliokoa Taifa hili.Magufuli peke yake hawezi bila ushirikiano kutoka kwetu sisi wananchi.
 
uliyeleta thread hii kama ni askali basi uaskali wako mdogo sana.trained soldier ana channel za kuwasilisha habari.ndio maana zamani wanajeshi na polisi walikuwa wahehe na wakulya wee utakuwa mtu wa ...................
Hao watu wanajua kuishi viapo vyao. Mhehe akiapa hata ufanyaje ataishia kukuambia "nene swelaga" hapo yuko tayari hata umuue
 
Back
Top Bottom