KERO Watumishi tulioko masomoni tunaonewa, hatupandishwi madaraja

KERO Watumishi tulioko masomoni tunaonewa, hatupandishwi madaraja

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest
Mimi ni mwalimu nimeajiriwa mwaka 2014.

Pamoja na kuwa ni mujibu wa sheria mtumishi kupanda daraja Kila baada ya miaka mitatu, sisi hatukupanda hata baada ya miaka 7, tulidhulumiwa madaraja mawili na serikali ya Magufuli, tukapewa daraja moja na mama mwaka 2021, Mungu amlinde Kwa Nia njema.

Nimeomba kwenda masomoni mwaka 2022 baada ya kutumikia daraja Kwa mwaka na nusu nikarubusiwa na mwajiri Kwa sharti la kujisomesha na nikakubali kusain mkataba wa ruhusa nikakabidhiwa barua.

Mwaka huu mwezi wa 6 wenzangu tuliopanda nao mwaka 2021 wamepanda madaraja, lakini mimi na wenzangu tulio masomoni tumeambiwa hatuna sifa ya kupanda kwasababu kuu 2, kwanza hatujajaza taarifa za utendaji kwenye mfumo wa PEPMIS, pili hatuwezi kupanda daraja ambalo hatujalitumikia!! Seriously! Mwaka 2017, tulitakiwa kupanda daraja tulilolitumikia na hatukupanda, mwaka 2020, tulitakiwa kupanda daraja linguine tulilolitumikia na hatukupanda, lakini leo tunaambiwa hatutapanda daraja ambalo hatujalitumikia.

Tunadhulumiwa, wanajua hatuna wa kututetea. Tukitoka shuleni tutapaswa kukaa tena miaka 3 ili tupande daraja hivyo tutakua tumepitwa madaraja mawili na tulioajiriwa nao na walioajiriwa mbele yetu.

Naamini siyo Nia ya mama Samia kutunyima haki zetu bali ni ujuaji wa baadhi ya watu wa utumishi. Swala hili litaathiri sana utendaji kazi wetu na madhara yake ni marefu.
 
Mimi ni mwalimu nimeajiriwa mwaka 2014.

Pamoja na kuwa ni mujibu wa sheria mtumishi kupanda daraja Kila baada ya miaka mitatu, sisi hatukupanda hata baada ya miaka 7, tulidhulumiwa madaraja mawili na serikali ya Magufuli, tukapewa daraja moja na mama mwaka 2021, Mungu amlinde Kwa Nia njema.

Nimeomba kwenda masomoni mwaka 2022 baada ya kutumikia daraja Kwa mwaka na nusu nikarubusiwa na mwajiri Kwa sharti la kujisomesha na nikakubali kusain mkataba wa ruhusa nikakabidhiwa barua.

Mwaka huu mwezi wa 6 wenzangu tuliopanda nao mwaka 2021 wamepanda madaraja, lakini mimi na wenzangu tulio masomoni tumeambiwa hatuna sifa ya kupanda kwasababu kuu 2, kwanza hatujajaza taarifa za utendaji kwenye mfumo wa PEPMIS, pili hatuwezi kupanda daraja ambalo hatujalitumikia!! Seriously! Mwaka 2017, tulitakiwa kupanda daraja tulilolitumikia na hatukupanda, mwaka 2020, tulitakiwa kupanda daraja linguine tulilolitumikia na hatukupanda, lakini leo tunaambiwa hatutapanda daraja ambalo hatujalitumikia.

Tunadhulumiwa, wanajua hatuna wa kututetea. Tukitoka shuleni tutapaswa kukaa tena miaka 3 ili tupande daraja hivyo tutakua tumepitwa madaraja mawili na tulioajiriwa nao na walioajiriwa mbele yetu.

Naamini siyo Nia ya mama Samia kutunyima haki zetu bali ni ujuaji wa baadhi ya watu wa utumishi. Swala hili litaathiri sana utendaji kazi wetu na madhara yake ni marefu.
Msipandishwe nyie si wale mnaowachangia fomu ya miaka mitano mingine!
 
Sasa unapandaje hujatekeleza majukumu yako ya kikazi ya kukufanya upande daraja,maluza shule uje utekeleze majukumu upande.
 
Thread hii ianzishe baada ya mshahara wa July.

June hii masuala ya madaraja bado yanashughulikiwa na sio wa masomoni tu ambao hamjapanda daraja bali watumishi wengi Sana wenye sifa za kupanda daraja bado hawajapanda.
 
Upo mkoa Gani . Kama upo mwanza Nenda Busisi kuna Daraja la Magufuli na Mabatini.

Kama upo Dar kapande Mfugale au Kijazi.
Usisubiri kupandishwa.

Just a Joke.
 
Kurudi shule nao ni jau tu kama lengo ni kuja kupata kipato kizuri kutokana na shule.

Hivi standing order inasemaje kuhusu hili jambo la madaraja ukiwa masomoni?
 
Mm najamaa angu yuko masomoni toka 2019 ....mwaka 2021 alipanda na mwaka huu kapanda asee maisha haya
 
Back
Top Bottom