DOKEZO Watumishi wa afya kitengo cha uzazi wa mpango katika kituo cha afya cha Utegi -Rorya acheni kuwaibia wateja wenu

DOKEZO Watumishi wa afya kitengo cha uzazi wa mpango katika kituo cha afya cha Utegi -Rorya acheni kuwaibia wateja wenu

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

nyanthorogo

JF-Expert Member
Joined
Jun 28, 2014
Posts
220
Reaction score
402
Leo mke wangu ameenda kubadilisha kipandikizi katika kituo hiki Cha Afya Utegi, huduma hiyo ni ya bure, Cha ajabu wauguzi wakasema hawana vifaa mpaka atoe hela. Vifaa hivyo ni ganzi na kiwembe.

Wakamwambia anunue kachupa ka ganzi kwa sh 8,000/= Huku wakisemezama kana kwamba wanamsaidia kwa sababu kichupa kingemgharimu sh 12,000/=. Baada ya kuwapatia fedha ,vifaa hivyo vikapatikana hapo hapo hospital, Huku wakisemezama kuwa wateja wakiona gari limeingia wanajazana kutafuta huduma, wakiambiwa huduma hiyo haipo watoe hela hawaelewi.

Naomba uongozi wa kituo hiki Cha Afya Cha Utegi wawachunguze watoa huduma hiyo. Huu ni wizi wa mchana kweupe
 
Watumishi wa Afya, tena ndanindani huko, kazi wanazochapa sio za Mchezo .

Tuendelee kuwapa Moyo na kuwatia nguvu !!.
 
Back
Top Bottom