Watumishi wa Serikali DSM ni lini wataacha kuwa "wahuni"?

Naipendatz

JF-Expert Member
Joined
Jul 27, 2011
Posts
5,096
Reaction score
8,234
Wote wamepewa fedha sawa kwa darasa moja (Mil 20). Ninavyosikia (Sina uhakika), vifaa vya ujenzi (Nondo, bati, Cement) DSM ni nafuu zaidi kulinganisha na mahali kama Bukombe kutokana na umbali kutoka viwandani. Lakini nikiangalia viwango vya madarasa katika picha hapa chini inaonesha kabisa madarasa na madawati ya DSM yapo chini ya kiwango kuliko yale ya Bukombe.

Rais ulisema utawapima Wateule wako kutokana na kazi zao, nadhani chujio lako la kwanza kwa Wakuu wa Mikoa na Wilaya, pamoja na Wakurugenzi wao litokane na jinsi gani wamesimamia ipasavyo ujenzi wa madarasa haya. Hilo litakuwa ni fundisho kubwa sana kwao and next time wakitakiwa kusimamia mradi wowote hawataleta utoto utoto.

Hongereni sana Bukombe na Mkuu wenu wa Mkoa kwa kazi nzuri.

"Wahuni" aliosema Polepole ndio hawa wa Kigamboni, wanatakiwa wamalizwe sasa.

Madarasa ya Kigamboni (DSM)







Madarasa ya Bukombe (Geita)





 
Hao wanaccm waliokalia hivyo viti kila mmoja anamgawo wake hapo
 
Huo ubora umeupimaje???
Ninavyojua mm kwa uzoefu wangu wa miaka michache niliyokaa Govt.
Huwa kuna ratio kwenye ujenzi, Armani na BOQ wajenzi wote wanapaswa kujenga kwa kutumia hizo categories bila kuangalia ujenzi unafanyika wapi???
 
Huo ubora umeupimaje???
Ninavyojua mm kwa uzoefu wangu wa miaka michache niliyokaa Govt.
Huwa kuna ratio kwenye ujenzi, Armani na BOQ wajenzi wote wanapaswa kujenga kwa kutumia hizo categories bila kuangalia ujenzi unafanyika wapi???
Kuna vitu vingi hapo unaweza kucompare vinavyoonekana kwa macho, kuanzia sakafu, madawati, rangi za kuta, gypsum na madirisha!! Ratio haipimwi kwa macho
 
Mimi naona tofauti ni rangi tu....wale wamepaka rangi chafu, hawa wamepaka rangi safi
 
Bukombe darasa lina marumaru ila Daslam chini pako plain. Inafikirisha kidogo
 
Mi nipo Ushirombo Kilimahewa,mzee tuonane tuyajenge
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…