DOKEZO Watumishi wa St Marys Secondary Mbezi hawana mikataba ya kazi

DOKEZO Watumishi wa St Marys Secondary Mbezi hawana mikataba ya kazi

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
A

Anonymous

Guest
Habari JamiiForums, nimekuwa mdau wa muda mrefu lakini pia nimekuwa napata malalamiko mengi sana kutoka kwa rafiki yangu mmoja hivi naomba langu lisitajwe.

Watumishi wa shule ya St Marys Secondary Mbezi wanaishi katika mazingira Magumu sana, watumishi hao wote hawana mikataba ya kazi. Huyu mtu wangu wa karibu tangu aajiriwe pale hana mkataba hadi alipoondoka pale alikosa stahiki zaje zote na hivyo kukosa base ya kuanzia maisha baada ya kutoka pale.

Utaratibu haujulikani ni upi unafukuzwa kazi tuu kama ulivyokuja na unaondoka hujui haki zako za msingi, kiukweli hii inaumiza, mamlaka husika zifanyie suala hilo kazi.

Mtu kafanya kazi miaka mitano unamfukuza bila utaratibu wowote bila kosa, mishahara hailipwi kwa wakati na mingi wanadai mfano mshahara wa mwezi wa 10, 11, 12, 01 katika hiyo miezi wamelipwa miezi miwili tuu haijulikani ni mwezi gani NSSF zao hazijulikani makato yao yapoje
Barua za ajira hawana
Barua za mikataba ya kazi hakuna
Wapo wapo tu.
Naomba kupaza sauti watumishi hao wasaidiwe.

images-2.jpeg
 
Watanzania nije thamani
Unafanyaje kazi bila mkataba
Hamkuongelea hata maslahi
 
Watakuwa wamekubaliana na hali hiyo ndio maana wanafanya kazi kwa zaidi ya miezi mitatu bila mkataba. Walitakiwa wazingue na kuacha kazi mara moja wanaponyimwa kusaini mikataba pindi probation period inapoisha.

Kuhusu michango yao kupelekwa/kutopelekwa NSSF, watumie account zao kucheki na kama haipelekwa kwa zaidi ya miezi mitatu, wafungue malalamiko kwa mwajiri wao na NSSF kama ni wanachama tayari.
 
Habari JamiiForums, nimekuwa mdau wa muda mrefu lakini pia nimekuwa napata malalamiko mengi sana kutoka kwa rafiki yangu mmoja hivi naomba langu lisitajwe.

Watumishi wa shule ya St Marys Secondary Mbezi wanaishi katika mazingira Magumu sana, watumishi hao wote hawana mikataba ya kazi. Huyu mtu wangu wa karibu tangu aajiriwe pale hana mkataba hadi alipoondoka pale alikosa stahiki zaje zote na hivyo kukosa base ya kuanzia maisha baada ya kutoka pale.

Utaratibu haujulikani ni upi unafukuzwa kazi tuu kama ulivyokuja na unaondoka hujui haki zako za msingi, kiukweli hii inaumiza, mamlaka husika zifanyie suala hilo kazi.

Mtu kafanya kazi miaka mitano unamfukuza bila utaratibu wowote bila kosa, mishahara hailipwi kwa wakati na mingi wanadai mfano mshahara wa mwezi wa 10, 11, 12, 01 katika hiyo miezi wamelipwa miezi miwili tuu haijulikani ni mwezi gani NSSF zao hazijulikani makato yao yapoje
Barua za ajira hawana
Barua za mikataba ya kazi hakuna
Wapo wapo tu.
Naomba kupaza sauti watumishi hao wasaidiwe.

View attachment 3230000

Siwalaumu kufanya kazi katika mazingira hayo lakini niwajuze tu hakuna kada inayodharauliwa kama kada ya ualimu na walimu wenyewe Kwa ujumla. Waajiri wana vibuli sana ukidai haki zako unaambiwa kwanza Kuna walimu wengi mtaani, kwa hiyo walimu masikini waliosota kitaa wanaamua kuishi katika maisha ya mateso, dhulma, na kila aina ya manyanyaso.

Na wanafanya hivyo wanaamini kazi ya ualimu anaweza kufanya mtu yeyote. Suluhisho ya tatizo Hili kuundwa Kwa bodi ya walimu kama ilivyo kwa baadhi taasisi, huwezi kutoa huduma kama wewe hauna leseni. Hivyo basi itapunguza wimbi la walimu wasio na mafunzo, lakini pia Serikali inapoteza Kodi kubwa sana ambayo inakwepwa na waajiri kama hao ambao hawataki kutoa mikataba Kwa wafanyakazi wake.

Lakini sasa Cha ajabu wanapiga vita sana uundwaji wa bodi hiyo ya walimu, na wapingaji wakubwa ni walimu waliopo serikalini pamoja na chama chao Cha walimu CWT.

Ila tumshukuru rais Samia kwa kuzindua sera mpya ya elimu ya 2014 ambayo inalazimishwa kuundwa Kwa bodi ya walimu. Tofauti na hapo manyanyaso yataendelea haki za walimu zitaporwa na waajiri wasio na huruma, utaondolewa kazini kwa majungu na hauna pa kwenda.
 
Habari JamiiForums, nimekuwa mdau wa muda mrefu lakini pia nimekuwa napata malalamiko mengi sana kutoka kwa rafiki yangu mmoja hivi naomba langu lisitajwe.

Watumishi wa shule ya St Marys Secondary Mbezi wanaishi katika mazingira Magumu sana, watumishi hao wote hawana mikataba ya kazi. Huyu mtu wangu wa karibu tangu aajiriwe pale hana mkataba hadi alipoondoka pale alikosa stahiki zaje zote na hivyo kukosa base ya kuanzia maisha baada ya kutoka pale.

Utaratibu haujulikani ni upi unafukuzwa kazi tuu kama ulivyokuja na unaondoka hujui haki zako za msingi, kiukweli hii inaumiza, mamlaka husika zifanyie suala hilo kazi.

Mtu kafanya kazi miaka mitano unamfukuza bila utaratibu wowote bila kosa, mishahara hailipwi kwa wakati na mingi wanadai mfano mshahara wa mwezi wa 10, 11, 12, 01 katika hiyo miezi wamelipwa miezi miwili tuu haijulikani ni mwezi gani NSSF zao hazijulikani makato yao yapoje
Barua za ajira hawana
Barua za mikataba ya kazi hakuna
Wapo wapo tu.
Naomba kupaza sauti watumishi hao wasaidiwe.

View attachment 3230000
Wamuandikie barua Pope, maana hapa inaonyesha Askofu mkuu, Paroko na Kadinali lau Moja
 
Habari JamiiForums, nimekuwa mdau wa muda mrefu lakini pia nimekuwa napata malalamiko mengi sana kutoka kwa rafiki yangu mmoja hivi naomba langu lisitajwe.

Watumishi wa shule ya St Marys Secondary Mbezi wanaishi katika mazingira Magumu sana, watumishi hao wote hawana mikataba ya kazi. Huyu mtu wangu wa karibu tangu aajiriwe pale hana mkataba hadi alipoondoka pale alikosa stahiki zaje zote na hivyo kukosa base ya kuanzia maisha baada ya kutoka pale.

Utaratibu haujulikani ni upi unafukuzwa kazi tuu kama ulivyokuja na unaondoka hujui haki zako za msingi, kiukweli hii inaumiza, mamlaka husika zifanyie suala hilo kazi.

Mtu kafanya kazi miaka mitano unamfukuza bila utaratibu wowote bila kosa, mishahara hailipwi kwa wakati na mingi wanadai mfano mshahara wa mwezi wa 10, 11, 12, 01 katika hiyo miezi wamelipwa miezi miwili tuu haijulikani ni mwezi gani NSSF zao hazijulikani makato yao yapoje
Barua za ajira hawana
Barua za mikataba ya kazi hakuna
Wapo wapo tu.
Naomba kupaza sauti watumishi hao wasaidiwe.

View attachment 3230000
Ugumu wa maisha ndio unaleta haya. Watu wanakaa miaka mingi bila ajira wala kuwa na shughuli yoyote ya kumuingizia kipato hivyo inafika point anakuwa yupo tayari kufanya lolote ili aweze kujikimu. Wengi wanaoteseka ni watoto wa masikini. Unaweza kuwalaumu hao wafanyakazi kama hujawahi kupitia kipindi kigumu kabla ya ajira rasmi
 
Back
Top Bottom