Uchaguzi 2020 Watumishi wa umma tuiondoe CCM madarakani

Ketoka

JF-Expert Member
Joined
Sep 23, 2015
Posts
1,117
Reaction score
1,966
Huu Uzi maalumu kwa ajili ya watumishi wa umma wenye salary slip na check no ambao kwa miaka 5 tumedhulumiwa haki yetu

Serikali ya ccm haina muda na watumishi, increments kwa watumishi zimetupiliwa mbali

Watumishi tumejikuta tunafanya kazi nyingi na ngumu kisa serikali haijiri,hili linawakumba walimu na kada ya afya

Nyongeza ya mishahara ndo hivyo tena, wastaafu kupata mafao yao mpaka mungu ashuke.

Madaraja kupanda ilikuwa miaka 3 ila sasa imepelekwa hadi miaka 4, ambapo sisi watumishi tunajua daraja ndo mshahara,sasa kama madaraja hayapandi mbona mishahara yetu ina hali ngumu,na pamoja kuongeza miaka ya kupanda daraja, ukifika hata hawapandishi tena wale ambao wangepanda mwaka huu ndo hivyo tena.

Ukienda masomoni tena inakuwa dhambi kubwa ya kujiendeleza,ccm hawataki watumishi wajiendeleze ndo maana waliokuwa masomoni hawakupandishwa madaraja

Vyama vya wafanyakazi hawana sauti, hawafurukuti.

Pamoja na matatizo mengi tuliyonayo bado serikali imeshindwa kutuweka mazingira mazuri kwa wafanyakazi

Tukiwa kama wapiga kura na wengine watakuwa wasimamizi na tukiwa na hazina ya wanaotutegemea huko nyuma kura zetu zinatosha kuonyesha serikali hii kuwa hatuitaki.

Kwa wale ambao watasimamia uchaguzi kwa niaba ya Tume lazima tuje kufanya yetu.

Watumishi wa umma njoo tuiondoe serikali hii madarakani.
 
Usiwastue, Utakapobahatika kusimamia kituo chako hakikisha ccm haitoki. Na kwa taarifa yako vyama kama chadema kimekuwa mtetezi wa wafanyakazi miaka yote. Hakuna chama kibaya kama ccm, kimetufanya tuwe maskini na hatukopesheki kabisa, na bodi ya mikopo wanatukata biala hata majadiliano 15%, lengo lao tuendelee kuwa maskini.
 
Usitufokee
Tunajua la kufanya hata wenyewe wanajua tutafanya nini
Wala hawahitaji kufanya kampeni huu ni wakati wa Sisi walau kujimwambafy
 
Mkowangapi?,ukishapata idadi yenu gawa kwa vyama vitano vikuu vya upinzani.
alafu njoo kwa kundi moja tu la machinga,ambao wanaimani na JPM kwa jinsi alivyowapigania machinga.na kwa jinsi Lissu anavyo pinga uhalali wa id za mchinga id ambazo zimewapa uhuru machinga kufanya kazi zao kwa uhuru.
 
Mwenye nchi alishawaambia wafanyakazi kuwa kama mnaona mishahara midogo nendeni mkalime kwani yapo mapori mengi sana Tanzania.
 
pole sana ila mlikua na nafasi ya kuitoa ccm 2015 but now its too late and its becomming never,
 
Tuko pamoja mkuu tumepita magumu sana na huu utawala...
 
Tupo laki tano nukta 5 ongeza wategemezi laki 5 tunapata 1 milioni point 5 ongeza vijana jobless mitaani kama million 1.5 tunapata 3 kura hizi zikitua kwa CHADEMA ccm mtanyooka tu mwaka huu

Na bado hatujafanya manuva kama maafisa wa Tume
 
ccm sio machinga sio nani nyie sera zenu kutufanya masiki ili uwe mtaji wenu kisiasa makundi yote tumestuka jiandae kuachia lissu ikulu mlifiki lissu awatania kurudi nyumba mkazidisha ukandamizaji sasa kaisha fika Disco kaingia masai
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…