Kikojozi
JF-Expert Member
- Mar 24, 2009
- 331
- 2
Heshima kwenu wanajamii.
Katika jitihada za kuongeza ufanisi sekta ya utumishi wa umma, nilikua napendekeza watumishi wote wa umma wapewe mikataba ya ajira inayomwezesha muajiri na wateja/wadau wote wa mashirika ya umma na ofisi za serikali kutathmini utendaji wao.
Hii ni tofauti na utaratibu wa sasa ambapo mtu anaajiriwa serikalini kwa 'permanent and pensionable terms'. Wakisha kamata ajira wenyewe wanasema mpaka kufukuzwa yaani uwe "umeboronga sana". Kwahiyo hata kama mtu hafanyi kazi kwa uadilifu anaendelea tu kuwepo kwenye ajira huku vijana wengi wanaomaliza vyuoni na wana uwezo wanakosa kazi. System ya sasa inavumilia mno uzembe na rushwa.
Ajira za serikali na mashirika ya umma iwe ya mikataba isiyozidi miaka mitano na ku-renew itategemea kama utendaji wa mtu unaridhisha.
Wadau mnalionaje suala la 'performance contracts' kwa watumishi wa umma?
Katika jitihada za kuongeza ufanisi sekta ya utumishi wa umma, nilikua napendekeza watumishi wote wa umma wapewe mikataba ya ajira inayomwezesha muajiri na wateja/wadau wote wa mashirika ya umma na ofisi za serikali kutathmini utendaji wao.
Hii ni tofauti na utaratibu wa sasa ambapo mtu anaajiriwa serikalini kwa 'permanent and pensionable terms'. Wakisha kamata ajira wenyewe wanasema mpaka kufukuzwa yaani uwe "umeboronga sana". Kwahiyo hata kama mtu hafanyi kazi kwa uadilifu anaendelea tu kuwepo kwenye ajira huku vijana wengi wanaomaliza vyuoni na wana uwezo wanakosa kazi. System ya sasa inavumilia mno uzembe na rushwa.
Ajira za serikali na mashirika ya umma iwe ya mikataba isiyozidi miaka mitano na ku-renew itategemea kama utendaji wa mtu unaridhisha.
Wadau mnalionaje suala la 'performance contracts' kwa watumishi wa umma?