Wauguzi na Wakunga watakiwa kuwasimamia watarajali waliopo mafunzo ya vitendo

Wauguzi na Wakunga watakiwa kuwasimamia watarajali waliopo mafunzo ya vitendo

Wizara ya Afya Tanzania

Official Account
Joined
Oct 1, 2020
Posts
58
Reaction score
127
Wauguzi na Wakunga wametakiwa kuwasimamia wauguzi na wakunga watarajali (interns) waliopo mafunzoni kwa vitendo na kuhakikisha wanafundishwa vizuri ili kuweza kutoa huduma bora kwa wagonjwa.

Wito huo umetolewa na Mkurugenzi wa Huduma za Uuguzi na Ukunga kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi. Ziada Sellah alipokuwa akizungumza na wauguzi na wakunga katika Mkoa wa Lindi.

"Interns hawa tuliowapata tuwasimamie kwenye kazi zao, tusiwaache wafanye kazi peke yao" amesema Bi. Ziada kwenye kikao kazi hicho kilichofanyika katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Lindi.

Amesema wagonjwa wanatakiwa kupewa huduma bora ambazo kwa asilimia kubwa wakiwa hospitalini huwa wanahudumiwa na wauguzi hivyo si sahihi 'interns' hao wakiachwa peke yao kuwahudumia wagonjwa.

Aidha Bi. Ziada amewataka watarajali hao kuwaheshimu wakufunzi wao ambao ni wauguzi na wakunga wenye uzoefu wa kutosha ili waweze kujifunza vizuri na kuweza kutoa huduma nzuri.
IMG_20201015_181055_356.jpg
IMG-20201015-WA0008.jpg
IMG_20201015_181055_357.jpg
 
Wauguzi na Wakunga nchini wametakiwa kuepuka kutoa lugha zisizofaa kwa wagonjwa kwani kufanya hivyo ni kinyume cha maadili na miiko ya taaluma hiyo.

Mkurugenzi wa huduma za Uuguzi na Ukunga kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ziada Sellah ameyasema haya leo jijini Dar es Salaam wakati wa kikao kazi na wauguzi na wakunga wa mkoa huo.

Mkurungezi huyo amesema kumekuwa na tabia chafu ya baadhi ya wauguzi na wakunga kutoa lugha zisizofaa kwa wagonjwa jambo linaloharibu taswira ya taaluma hiyo.

Aidha Ziada ametoa wito kwa wauguzi kujiendeleza kielimu ili waweze kujiongezea maarifa katika utaalamu wao wa kutoa huduma bora na zenye tija kwa wagonjwa.

Pia amewaasa watumishi wa sekta hiyo ya afya kufanya kazi kwa umoja na mshikamano wakizingatia suala la uwazi.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Dr. Rashid Mfaume ametoa wito kwa wauguzi kuheshimiana na kuthaminiana katika mazingira ya kazi.
 
Wito huo umetolewa na Mkurugenzi wa Huduma za Uuguzi na Ukunga kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi. Ziada Sellah alipokuwa akizungumza na wauguzi na wakunga katika Mkoa wa Lindi.

"Interns hawa tuliowapata tuwasimamie kwenye kazi zao, tusiwaache wafanye kazi peke yao" amesema Bi. Ziada kwenye kikao kazi hicho kilichofanyika katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Lindi.
Awe makini katika kutoa matamko wakati huu maana hali ya hewa haisomeki graphs zimevurugika waweza kusema jambo kwa nia njema ile unakaa unapigiwa makofi Gerson Msigwa kaachia "Taarifa kwa umma"
 
Back
Top Bottom