Nursalami Ng'oma
Member
- Jan 9, 2014
- 13
- 3
Heshima kwenu wote,
Mimi na mke wangu hatuna furaha kabisa kutokana maendeleo ya mtoto wetu. Mpaka sasa hivi ana miaka 3 ajabu hawezi kuongea wala kula mwenyewe.Chakula analishwa na anakula vizuri, kama akiwa na njaa sana na chakula kikawekwa chini tayari kwa kuliwe,yeye husogea pale na kuanza kula kwa mdomo na sisi kama wazazi wake tunachofanya ni kumpiga ili asizoee tabia hiyo.
Kwa kweli yeye mwenyewe ni mjanja na mchangamfu anapenda sana kutembea usipo mwangalia vizuri huwa mara nyingi anatutoroka nyumbani.
Wakati anazaliwa alizaliwa kwa matatizo, yaani alichelewa kuzaliwa, ilitakiwa mama yake aende thieta kwa ajili operation kutokana na kushindwa kazaa katika njia ya kawaida, lakini kabla maamuzi rasmi hayajatolewa dactari alikuja na akasema mke wangu anaweza akazaa kawaida bila kwenda thieta isipokuwa ataongezwa njia tu.
Mchakato wa kumwongeza njia ulifanyika na hatimae mke wangu akajifungua mtoto.Yule mtoto wakati anazaliwa hakulia akapigwa mabao sana kisha akaanza kulia,pia aliwekwa kwenye oven lile la watoto.
Kutembea pia amechelewa sana, ameanza kutembea akiwa na miaka 2.1 kwa sasa anatembea tu vizuri. Tatizo liko kwenye uongeaji na ulaji. Mikono yake iko vizuri tu,vitu anavyopenda yeye kunyanyau huwa ananyanyua kwa mikono yake lakini ukimshikisha kitu huwa ataki kabisa kushika,ukimlazimisha analia.
Naombeni msaada wenu nifanyeje juu ya huyu mtoto maana mtoto mwenyewe ni wa kwanza hatujui chochote mpaka tunachanganyikiwa.
Asanteni sana
Mimi na mke wangu hatuna furaha kabisa kutokana maendeleo ya mtoto wetu. Mpaka sasa hivi ana miaka 3 ajabu hawezi kuongea wala kula mwenyewe.Chakula analishwa na anakula vizuri, kama akiwa na njaa sana na chakula kikawekwa chini tayari kwa kuliwe,yeye husogea pale na kuanza kula kwa mdomo na sisi kama wazazi wake tunachofanya ni kumpiga ili asizoee tabia hiyo.
Kwa kweli yeye mwenyewe ni mjanja na mchangamfu anapenda sana kutembea usipo mwangalia vizuri huwa mara nyingi anatutoroka nyumbani.
Wakati anazaliwa alizaliwa kwa matatizo, yaani alichelewa kuzaliwa, ilitakiwa mama yake aende thieta kwa ajili operation kutokana na kushindwa kazaa katika njia ya kawaida, lakini kabla maamuzi rasmi hayajatolewa dactari alikuja na akasema mke wangu anaweza akazaa kawaida bila kwenda thieta isipokuwa ataongezwa njia tu.
Mchakato wa kumwongeza njia ulifanyika na hatimae mke wangu akajifungua mtoto.Yule mtoto wakati anazaliwa hakulia akapigwa mabao sana kisha akaanza kulia,pia aliwekwa kwenye oven lile la watoto.
Kutembea pia amechelewa sana, ameanza kutembea akiwa na miaka 2.1 kwa sasa anatembea tu vizuri. Tatizo liko kwenye uongeaji na ulaji. Mikono yake iko vizuri tu,vitu anavyopenda yeye kunyanyau huwa ananyanyua kwa mikono yake lakini ukimshikisha kitu huwa ataki kabisa kushika,ukimlazimisha analia.
Naombeni msaada wenu nifanyeje juu ya huyu mtoto maana mtoto mwenyewe ni wa kwanza hatujui chochote mpaka tunachanganyikiwa.
Asanteni sana