Wauza mafuta Tanzania wanatengeneza faida za ajabu

geomaipa

New Member
Joined
Nov 28, 2012
Posts
4
Reaction score
3
takribani mwaka mmoja toka leo bei ya mafuta kwa pipa moja katika soko la kimataifa lilikuwa zaidi ya $120. leo hii bei ya pipa moja la mafuta ni chini ya $36. mara ya mwisho bei ilikuwa chini hivi miaka 11 iliyopita. ndani ya mwaka mmoja bei ya mafuta imeshuka kwa asilimia 75. kipindi bei ya mafuta kwa pipa ikiwa zaidi ya $120 tanzania bei ya petroli ilikuwa zaidi ya tshs 2200. mwaka mmoja baadae bei mpya za ewura bado zinatupa mashaka ni taasisi hiyo. wasomi wa hii nchi wako wapi. EWURA ni jipu. tujiulize swali moja bei ingependa kwa asilimia 75 badala ya kushuka ingekuwa hivi hivi?
 
Wafanyabiashara wa TZ wameiweka serikali mfukoni,hapo ukiwauliza watakwambia bado wanamzigo wa zamani,ila yakipanda siku hiyo hiyo nao wanapandisha EWURA wapo kwaajili ya kulipwa mshahara na si kusimamia kazi zao.
 
Tuzidi kumuombea nguvu na afya tele rais wetu alioko madarakani maana amehapa kupigania haki na unyonyaji kama huu na kuweka mambo sawa sawa. tusubili majipu yatobolewe vizuri na kutatuliwa.
 
Mimi nadhani tatizo ni kodi za serikali!
 
Nadhani utafutwe utaratibu wa kila mtu aagize mafuta yake mwenyewe.

Au TIPPE ifufuliwe makampuni yakanunue mafuta tipper.
 

YAANI MUDA HUU PERTOL IWE TSH 660? NGOJA TUWASUBIRIE WAHUSIKA KAMA WATAFANYA JAMBO HAPO.
 
Hizi bei ni za mafuta ghafi (crude oil)
 
Hizi bei ni za mafuta ghafi (crude oil)
hata kama ni ghafi,lazima kuwe na uwiano mwisho wa siku,we jiulize mafuta ghafi yangepanda kwa asilimia 75 bei ingekuwa sh ngap saivi?
 
Hawawezi kurudisha tazama coz wana malori yao ya kusafirishia wese...
Hapo ndio mitihani ndio maana warioba na mwalimu walitambua athari za mwanasiasa kuwa mfanyabiashara.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…