Mkalukungone mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 862
- 1,755
BAADHI ya wafanyabiashara wanaouza maji wanayohifadhi katika matangi ya kubebwa na magari maarufu maboza, mkoani Dar es Salaam, wamelalama hali ni mbaya kibiashara kutokana na maji kuadimika.
Katika mazungumzo na Nipashe, wafanyabiashara hao wamedai kuwa kuadimika kwa bidhaa yao hiyo kunawapa wakati mgumu kwa kuwa ndio tegemeo lao kujipatia kipato cha kuendesha familia.
"Juzi, kutwa nzima maji hayakuwapo. Hapa si unaona hata ukingaji ulivyo, sivyo ambavyo huwa yanakingwa kwenye gari, huo mpira ulipaswa kuingizwa kwa juu kule, yana presha ndogo, hapa sina uhakika kama boza langu litajaa," alilalama Ezron Mmari, aliyejitambulisha amefanya biashara hiyo kwa miaka 20 sasa.
Soma Pia: Waziri wa Maji ingilia kati DAWASA, hali ya maji Dar ni mbaya sana
Akiwa kioski cha kujaza maji cha Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) kilichoko Mbezi TANESCO, Mmari alisema kuwa kipindi hiki ni kigumu kwao, hata wanalazimika kwenda kutafuta maji mbali, ikiwamo Kibamba, hivyo gharama zinakuwa kubwa tofauti miaka iliyopita.
Katika mazungumzo na Nipashe, wafanyabiashara hao wamedai kuwa kuadimika kwa bidhaa yao hiyo kunawapa wakati mgumu kwa kuwa ndio tegemeo lao kujipatia kipato cha kuendesha familia.
"Juzi, kutwa nzima maji hayakuwapo. Hapa si unaona hata ukingaji ulivyo, sivyo ambavyo huwa yanakingwa kwenye gari, huo mpira ulipaswa kuingizwa kwa juu kule, yana presha ndogo, hapa sina uhakika kama boza langu litajaa," alilalama Ezron Mmari, aliyejitambulisha amefanya biashara hiyo kwa miaka 20 sasa.
Soma Pia: Waziri wa Maji ingilia kati DAWASA, hali ya maji Dar ni mbaya sana
Akiwa kioski cha kujaza maji cha Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) kilichoko Mbezi TANESCO, Mmari alisema kuwa kipindi hiki ni kigumu kwao, hata wanalazimika kwenda kutafuta maji mbali, ikiwamo Kibamba, hivyo gharama zinakuwa kubwa tofauti miaka iliyopita.